EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 27, 2015

UCHAGUZI MKUU 2015 WASANII BONGO WANAUZUNGUMZIAJE?

Laurent Samatta
Habari ya mjini kwa sasa ni Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba, 2015 ambapo Watanzania wote watatumia haki yao ya msingi ya kupiga kura, kuwachagua viongozi wanaowataka.
Showbiz Plus imewatafuta wasanii wa tasnia tofauti Bongo na kuwauliza mtazamo wao juu ya uchaguzi huo na hali ya upepo wa kisiasa Bongo ambapo wamefunguka kama ifuatavyo:
MRISHO MPOTO ‘MJOMBA’
 Mkali huyu wa kughani na tungo za Kiswahili, yeye amefunguka:
“Kwanza kabisa uchaguzi umegawanyika sehemu mbili, kuna viongozi ambao wanahitaji madaraka na kuna wengine wanahitaji kufanya biashara.
“Vilevile hata wapiga kura nao wapo wanaojiandaa kufanya biashara kwa kujua kwamba wakimpigia kura kiongozi fulani, watanufaika na kitu fulani, tofauti na zamani ambapo utii na nidhamu kwa viongozi na wapiga kura ulikuwa mkubwa.“Sasa hivi hata wasanii nao wanafanya biashara kwa kutazama mgombea gani ana fedha ndiyo wanaenda kumfanyia kampeni, kwa hali hii tutegemee kuwa uchaguzi utakuwa wa kibiashara na si kutafuta kiongozi bora kwa taifa.”
EMMANUEL ELIBARIKI ‘NAY WA MITEGO’
Msanii huyu wa Bongo Fleva ameeleza mtazamo wake kuelekea uchaguzi mkuu:
“Uchaguzi wa mwaka huu unaweza kuwa mgumu sana kwa sababu watu wameelimika tofauti na zamani ambapo watu walikuwa wanafanya mambo bila kujielewa. Vijana na watu wengine wameelimika na kujua kiongozi gani anafaa na nani hafai.“Ule ujanja wa kusema baadhi ya vyama vitaiba kura nadhani hilo litakuwa gumu sana mwaka huu kwani kila mtu anapiga kura akiwa anajua haki zake za msingi.”
KHADIJA KOPA ‘MALKIA’
Malkia huyu wa mipasho, ambaye pia ana uelewa mkubwa kwenye mambo yanayohusu siasa alisema: “Kwa kweli mi naona mwaka huu utakuwa mzuri kwa upande wa wanawake kwa sababu katiba inayopendekezwa ikipitishwa kutakuwa na usawa katika kila nafasi ya uongozi kati ya wanaume na wanawake.
BABY MADAHA.
“Nawasihi wanawake kama wapo wanaoweza kuongoza nafasi mbalimbali wajitokeze kupigania nafasi hizo kuanzia urais, ubunge mpaka udiwani. Naamini tutaweza kufika mahali ambapo na sisi tutajivunia kuwa na viongozi wengi wanawake.”

KULWA KIKUMBA ‘DUDE’
Msanii huyu wa filamu alisema “Mtazamo wangu kwa kweli mi naona uchanguzi wa mwaka huu utakuwa mgumu kuliko changuzi zote zilizowahi kutokea ndani ya taifa hili, kwa sababu watu wengi wameamka na wanajua nini wanafanya.
“Lakini pia wananchi wanaanza kuwakataa baadhi ya vigogo wanaokuja mtaani kwa mbwembwe na baada ya kupata kile wanachokitaka wanakimbia na kujali maslahi yao binafsi, kwa hali hii baadhi ya vigogo wataanguka sana kwenye nafasi zao, tumeona kwenye Serikali za Mitaa mambo yalivyokuwa, tusubiri lakini uchanguzi utakuwa mgumu sana, vijana wengi walikuwa hawapigi kura lakini sasa wamejua maana halisi ya kura zao”.
AMINI MWINYIMKUU
Msanii huyu wa muziki wa Bongo Fleva naye alifunguka: “Uchaguzi wa mwaka huu mimi naona utakuwa mzuri kwa sababu kila chama kina mashabiki na wapenzi wake na kikubwa ambacho kinaonekana ni kwamba wananchi wengi wameelewa nini maana ya kupiga kura kwa lengo la kupata viongozi ambao wataleta maendeleo ndani ya taifa letu.”
EMmANUEL ELIBARIKI ‘NAY WA MITEGO’.
AMRI ATHUMANI ‘KING MAJUTO’
Mkali huyu wa komedi Bongo, naye alikuwa na mawazo yake: “Mwaka huu uchaguzi utakuwa wa raha na starehe maana tunahitaji kiongozi bora na kama inavyojulikana kwamba CCM ni chama kizuri hivyo kila kitu kitakuwa sawa na watu watafurahi, nadhani kila jambo halitakuwa gumu katika kufanikisha hili kuanzia ngazi ya urais, ubunge na hata udiwani.
BABY MADAHA
Mwanadada huyu anayefanya poa kwenye gemu la Bongo Fleva, alifunguka: “Naamini kuwa katika uchaguzi wa mwaka huu bado nafasi ya wanawake kwenye urais itakuwa ni ndogo lakini kwa upande wa nafasi za ubunge na udiwani wanaweza kufanya vizuri zaidi na watu wakashangaa kuona viti vingi vikichukuliwa na wanawake wenye kiu ya kuleta maendeleo ndani ya taifa letu. Mi naamini wanawake tunaweza.”
EMMA-NUEL SIMWINGA ‘IZZO BUSINESS’
Mkali huyu wa Bongo Fleva kutoka Nyanda za Juu Kusini, mkoani Mbeya, naye amefungukia uchaguzi mkuu kwa kueleza kuwa anaamini uchaguzi wa mwaka huu utakuwa wa amani na utulivu.
“Kuhusu mambo mengine kama vurugu na machafuko, hivyo havina nafasi kabisa,” alisema.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate