EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, May 21, 2015

WEMA; HATA MIMI NINGEKUWA AUNT EZEKIEL NINGEGOMBANA NA WEWE


Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu.
Oscar ndauka
LICHA ya kupatana, habari ya mjini kwa sasa ni ugomvi mkali, wenye visa  vya kushangaza kati ya mastaa wawili wa sinema za Bongo, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel.Hii ‘kapo’ siku za karibuni, ilikuwa nzuri kwa maana ya urafiki wao mkubwa.Urafiki wa Wema na Aunt ulianza pale Wema alipoutengua urafiki wake na staa mwingine wa fani hiyo, Kajala Masanja.
Wema Sepetu akiwa na Aunt Ezekiel.
Kuna visa lukuki kuhusu chanzo cha ugomvi wa Wema na Kajala, lakini ‘kuchukuliana’ bwana ndiyo kulitajwa sana!
Ikumbukwe kuwa, Kajala naye alirithi kijiti cha urafiki kwa Wema kutoka kwa msanii wa filamu na Mbongo Fleva, Snura Mushi.
TUREJEE KWA AUNT
Katika urafiki ambao ulionekana ungedumu zaidi ni kati ya Wema na Aunt kwa vile, Aunt alionekana kama mkomavu wa mambo ya ukaribu kuliko wengine, Snura na Kajala.Sasa siku za hivi karibuni, Magazeti Pendwa ya Global Publishers (ambayo huwa ya kwanza kufichua mambo ya siri ya mastaa), yaliandika kuhusu uhasama ulioibuka kati ya wawili hao chanzo kikiwa ni mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Mpenzi wa sasa wa Diamond, Zarinah Hassan ‘Zari’ aliandaa shoo aliyoiita Zari All White Party iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar.
UGOMVI ULIANZA KWENYE PROMO
Inajulikana kwamba, mtu anapoandaa shoo, kikubwa ni kuipigia ‘debe’ kwa maana ya kwamba, watu wajue kuna shoo kubwa ili waweze kuhudhuria kwa wingi na ndiyo mafanikio ya mwenye kuandaa! Wakati shoo hiyo ikipigiwa debe na vyombo mbalimbali vya habari sambamba na wadhamini, Aunt aliandika ujumbe wa kuisifia, kwamba itakuwa ya nguvu na si ya kukosa, akaitupia kwenye mtandao wake wa Instagram.
AUNT MNAFIKI?
Habari zilimfikia Wema kwamba, Aunt ametupia kwenye ukurasa wake akiisifia shoo ya Zari All White. Hapo ndipo pakawa pabaya kwa Wema akitafsiri kwamba, kitendo hicho kwake ni kibaya kwa sababu Zari yupo na Diamond ambaye yeye alikuwa mpenzi wake zamani, akammwaga! Tena hapa ieleweke sawa, Wema ndiye aliyemmwaga Diamond.
Kumbe Wema anaishi na kinyongo cha Zari kwa sababu amemchukua ‘wa zamani’ wake, Diamond. Kwa hiyo ana bifu! Akitokea mtu akampa 5 Zari, kwa Wema mtu huyo anakuwa adui kama ilivyokuwa kwa Aunt Ezekiel ambaye ameonekana ni mnafiki! Anachekaje na Zari wakati Zari na yeye ni maadui?! (eti).
KWA NINI AUNT ALIFANYA VILE LAKINI?
Aunt alikuwa na kila sababu ya kuifagilia shoo ile kwa sababu moja kubwa sana! Ameshamwanika mpenzi wake wa sasa kwamba anaitwa Moses Iyobo! Huyu dogo ni dansa kwenye kundi la Diamond. Kwa hiyo shoo za Zari ilitegemea sana madansa wa Diamond.
Hivyo, Aunt alitumia nafasi hiyo kuwataka watu wafike kwa wingi, ukumbi ujae kutokana na kiingilio na waonesha shoo, akiwemo Iyobo walipwe vizuri, ili maisha yake na Aunt ambaye kwa sasa ni mjamzito, yaendelee. Sasa Wema alitakaje? Aunt aseme; ‘msiende shoo ya Zari, itakuwa mbaya sana’! Halafu ‘mzee’ (Iyobo) aende kula za uso? Ni akili kweli?
HUU NI UTOTO!
Mimi nauona huu ni utoto uliopitiliza! Katika hilo la Wema kumwona Aunt ni msaliti au mnafiki, hata mimi kama ningekuwa Aunt ningegombana na Wema na wala moyoni nisingeona nimepoteza chochote!
AUNT NA IYOBO
Naamini Aunt na Iyobo bado wapo sana kimaisha kuliko Aunt na Wema. Mbaya zaidi ukizingatia Wema mwenyewe kila rafiki anayempata anampoteza kwa uadui! Maana yake nini sasa!
Mimi namshauri (Wema) akae chini na kutafakari kwa mapana mwenyewe, na si kwa kushauriwa na akina Petit Man au Martin Kadinda, ajiulize ni kwa nini yeye! Na si kujiuliza ni kwa nini marafiki zake wengi humaliza nao vibaya!
Anaweza kuamini ana nuksi kumbe si nuksi bali ni maisha ya ubinafsi! Cha kwake anataka akiendeshe yeye na cha wenzake pia anataka akiendeshe yeye, hayo si maisha Wema bwana! Chenji!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate