EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 30, 2012

Bob Junior: Nimempata kitu cha ukweli


                                                                        Halima Ally
 Nyota wa filamu kutoka visiwani Zanzibar Halima Ally ‘Imma’ ndiye anayetarajiwa kulamba shavu la kuwa mke halali wa Bob Junior.Taarifa kutoka visiwani humo zimesema kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia uhusiano wa muda mrefu uliokuwepo baina ya wawili hao.Hakuna mwingine ni Halima, siku zote Bob junior amekuwa akija huku tunawaona wako pamoja na istoshe Halima alituambia kuwa wakati wowote atakuwa mke wa mtu” kilisema chanzo Halima alikuwa mmoja wa mastaa walioshiriki filamu ya Royal Prince iliyotayarishwa visiwani humo chini ya kampuni kubwa El- Fahad Production

MSANII machachari wa Bongo Flava, Bob Junior a.k.a Rais wa Masharobaro, anaachana na kambi ya ukapera na kuanza maisha mapya atakapofunga ndoa kesho Jumapili.

Msanii huyo aliyetamba na nyimbo za 'Oyoyo', 'Andazi', 'Mapenzi ya Kweli' pamoja na 'Nichumu' zinazoendelea kusumbua katika vituo mbalimbali vya redio na runinga ndani na nje ya Tanzania, amesema ameamua kuvuta jiko kwani wakati wake umefika.

Akizungumza na Mwanaspoti, Bob alisema: "Huu ni muda wa kupata mwenzangu nitakayeshirikiana naye kwa kila jambo. Ninafanya hivi ili kujiepusha na anasa za dunia maana mambo ni mengi.

Anafafanua kuwa mwanamke anayetarajia kumwoa amekidhi vigezo ambavyo yeye binafsi anavihitaji kwa mke.

"Ndoa si kukurupuka. Nimekuwa makini mno kufikia uamuzi huu ili kuepusha migongano au migogoro ndani ya ndoa, nimechagua mwanamke ambaye naona kabisa amekidhi vigezo ninavyohitaji na mwenye tabia ambazo tunaendana, alisema.

Akivitaja vigezo hivyo anasema siku zote alihitaji kuwa na mke mwenye tabia njema, aliyelelewa katika maadili na misingi ya dini yake ya Kiislamu na mwenye kupenda kumcha Mungu.

Anasema ingawa katika hali ya kawaida ni ngumu kumpata mwanamke mwenye vigezo hivyo, lakini kwa upande wake amebahatika kumpata mwanamke huyo kutoka visiwani Zanzibar.
 
Nimelelewa katika misingi ya Kiislamu na ndiyo maana nahitaji mke ambaye pia atakuwa amejengwa vizuri katika misingi hiyo ili aweze kunisukuma niweze kumcha Mungu kama ilivyokuwa awali," alisema.

"Unajua kidogo siku hizi nimetawaliwa na mambo ya dunia sasa lazima kuwa na mtu atakayesaidia kuniweka sawa."

Anasema kutokana na hilo hapo kesho anatarajia kupanda boti mpaka visiwani Zanzibar ambapo ataenda kufunga ndoa na baadaye kumtambulisha rasmi mkewe kwa mashabiki wake kwenye shoo maalum itakayofanyika katika klabu ya Billicanas iliyopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
Nitapangilia kila kitu kwa muda wake kwani natakiwa nisiwanyime burudani mashabiki wangu na vilevile lazima niwajibike kwa mke wangu," aliongeza.

"Nina uhakika kwa kupanga ratiba vizuri, nitamudu bila wasiwasi wowote, naweza kusema ndoa itanipa changamoto ya kutafuta zaidi ili kuhakikisha familia ninayokwenda kuianzisha inapata mahitaji yote muhimu, mwanaume lazima uimudu familia.

Licha ya kuwa mwanamuziki, Bob Junior pia ni mtayarishaji wa muziki katika studio yake inayoitwa Sharobaro Records ambayo imefanikiwa kutengeneza nyimbo mbalimbali.

Miongoni mwa nyimbo zilizopita katika mikono yake ni pamoja na 'Lofa' ya Top C, 'Kamwambie' ya Diamond, 'Far Away' ya Big Jahman na nyinginezo kadhaa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate