EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 28, 2012

DIAMOND, WEMA WANASWA HOTELINI



Wema.

Diamond.
NDIVYO ilivyokuwa, staa mkali wa filamu Bongo, Wema Sepetu na mwanamuziki wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa yupo juu, Nasibu Abdul a.k.a Diamond ‘Plantinum’ wamenaswa katika hoteli yenye hadhi ya nyota tano Giraffe iliyopo Mbezi, jijini Dar es Salaam.

MESEJI YA KWANZA KWENYE SIMU YA PAPARAZI
Asubuhi ya Juni 26, 2012, ujumbe mfupi wa maneno (sms) uliingia kwenye simu ya paparazi wetu ukidondosha madai mazito kuwa, mastaa hao waliowahi kuwa wachumba na baadaye kumwagana kinomanoma, wako kwenye hoteli hiyo ‘wakiponda raha kwani kufa kwaja’.
Meseji hiyo ikafafanua: “Tena wapo toka jana, Wema yeye yupo toka alipomaliza ile shughuli yake na Omotola yule mdada wa Naijeria (Nigeria).”

MAPAPARAZI WAINGIA MZIGONI
Baada ya kupata ujumbe huo, waandishi wetu walikaa kama kamati mbele ya mhariri wao, wakaandaa zana mbalimbali zikiwemo kamera na vifaa vya kurekodia kwa ajili ya kufuatilia ukweli wa meseji hiyo.

GARI LA DIAMOND NJE YA HOTELI
Waandishi wetu walifika hotelini hapo saa 3:46 ambapo nje ya hoteli hiyo, mapaparazi hao walianza kuamini Platinum yupo ndani baada ya kuliona gari lake aina ya Toyota Prado, lakini katika kuzungusha makengeza yao hawakuweza kulitia machoni gari la Wema.

MBELE YA MAPOKEZI YA HOTELI
Mbele ya kaunta ya mapokezi, waandishi waliomba kuonana na Wema Sepetu.
Mtu wa Mapokezi: Nimwambie nani?
Musa: Mwambie baby wake.
Mtu wa Mapokezi: Baby wake yupi?
Musa: Musa Mateja.
Mtu wa Mapokezi alimtwangia simu Wema ambapo alipoambiwa ni Musa Mateja aliamuru asubiri eneo hilo mpaka atakapoitwa kwenda chumbani.

DIAMOND HUYO!
Waandishi wakiwa wamepiga kambi wakisubiri kuitwa, ghafla Diamond alishuka akiwa mbiombio kuelekea kwenye gari lake kama mtu anayewahi. Mapaparazi wetu walimfuata hadi kwenye gari ambapo alikuwa ameshaingia.

MSIKIE ALICHOSEMA
Bila kupoteza muda alisomewa mashitaka yake ‘eituzedi’ ambapo alivuta pumzi kwa nguvu kisha akafunguka:
“Mimi hata sijui kama Wema yupo hapa hotelini, kwani yupo hapa? Chumba namba ngapi? Mimi nilikuja kwenye mambo yangu, kwa sasa natunga mashairi ya wimbo mwingine kwa hiyo nilikuja tangu jana ili kufanya kazi yangu kwa ufanisi, unajua napenda kuwa sehemu yenye utulivu mkubwa.
“Unajua nini, nilikuwa Morogoro, nimerudi jana, nikaja hapa kumfuata Jeff, si unajua yule mshikaji wangu sana? Kuna wakati pia huwa nakuja pale kwenye hoteli moja ipo jirani na ofisini zenu, pale napo pazuri sana, nimewahi kulala. Ha! Ha! Ha! Musa bwana!”

MENEJA WA WEMA
Meneja wa Wema, Martin Kadinda naye alikutana na waandishi wetu ambapo alishtuka kumwona Diamond kwenye gari lake.
Martin: Khaa! Diamond unaweza kuja hapa hotelini halafu unaondoka usinitafute wakati unajua mimi nipo na tuna ishu yetu?
Diamond: (kicheko tu).

WAANDISHI WARUDI MAPOKEZI, WAITWA KWA WEMA
Baada ya kumalizana na Diamond waandishi wetu walirudi mapokezi ambapo walipelekwa kwenye chumba alichomo supastaa mwenye chemchemi za skendo Bongo, Wema na kumkuta akiwa na rafiki yake kipenzi (lakini asiyekubalika na mama yake), Snura Mushi.
Wema, baada ya kusomewa mashitaka yake alishtuka sana na kuonesha mshangao kusikia Diamond alilala hotelini hapo.

Alisema kuwa yeye ndiyo kwanza yuko kitandani na alikuwa amelala na Snura, habari ya Diamond kuwepo hotelini hapo anasikia kutoka kwa mapaparazi lakini yeye hajui chochote.
“Jamani mnavyoniona mimi hapa ndiyo kwanza nimeamka, hata nje sijatoka na watu wa kwanza kuongea nao ni nyinyi, mimi sijui kabisa kama huyo mtu yuko hapa. Kwanza alifuata nini hapa jamani?”
Amani: Sisi tulivyosikia alikuwa na wewe, sasa wewe tena unatuuliza sisi, tutajua vipi? Si ndiyo maana tumekuja?
Wema: Jamani kusema kweli… (akachukua simu na kumpigia mwanaume aliyedai ni mpenzi wake) dady, wamekuja waandishi hapa wanasema wamesikia nimelala na Diamond, we si tumeongea hadi usiku sana?

MASWALI MAGUMU
Inawezekana Diamond akafika hotelini hapo bila Wema kuwa na taarifa?
Ni kweli kwamba, Wema aliweka kambi pale kwa lengo la kujipumzisha tu akiwa na shoga yake Snura?
Utulivu anaodai Diamond aliufuata pale hotelini ulikosekana sehemu nyingine yoyote (hasa nyumbani) ikiwemo ufukweni?
Kwa nini Wema aliharakisha kumpigia simu huyo aliyemuita mpenzi wake kumwambia kuhusu waandishi kufuatilia habari ya kulala na Diamond wakati akidai walizungumza hadi usiku sana?

UKWELI UPO KWA WEMA, DIAMOND
Kwa maelezo yao hayo, bado ukweli unabaki kuwa siri yao. Hata hivyo, penzi halina siri, kama wanaficha, mapaparazi wapo macho kuwafuatilia na kama ni kweli wanatoka, siku moja mambo yatakuwa hadharani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate