MSANII wa muziki wa Bongo Flava, Ney wa Mitego,
amewashukia wasanii wanaounda kundi la Bongo Movie Stars kwa kusema kuwa
wameshindwa kutengeneza filamu zenye ujumbe, badala yake wanatumia
filamu hizo kuuza sura zao tu.
Bongo Movie hakuna kitu zaidi ya biashara zao, ndiyo maana mara nyingi utaona akina dada wakivaa vimini na nguo zinazowaacha wazi kwa ajili ya kuwachanganya wapenda wanawake," alisema.
"Kuna watu wanaweza kuwatetea, lakini mimi ni shahidi kuwa kuna rafiki zangu wengi wamefanya nao biashara ya mapenzi.
"Kwa sababu ni washikaji zangu siwezi kuwataja, mara nyingi nikiimba najua ukweli, kama wanaigiza waigize na kuachana na biashara nyingine.
Alisema kutokana na kutokuridhishwa na wasanii hao, ameamua kuingia rasmi katika tasnia ya filamu kwa kuandaa filamu itakayojulikana kwa jina X.
"Filamu hiyo itaelezea maisha ya vijana wa Manzese, Dar es Salaam na sehemu zingine ambazo kutokana na hali ya maisha kuwabana vijana, wamejikuta wakiingia katika biashara haramu bila kujua madhara yake," alisema.
Alipoulizwa kuhusu kuwashirikisha wasanii nyota ambao amewashutumu kuwa wameishiwa, alisema kuwa hana shaka na hilo kwa wale wasanii wa kazi atawatumia.
Alisema muswada wa filamu hiyo umekamilika na sasa kazi ya kurekodi itaanza hivi karibuni.
Bongo Movie hakuna kitu zaidi ya biashara zao, ndiyo maana mara nyingi utaona akina dada wakivaa vimini na nguo zinazowaacha wazi kwa ajili ya kuwachanganya wapenda wanawake," alisema.
"Kuna watu wanaweza kuwatetea, lakini mimi ni shahidi kuwa kuna rafiki zangu wengi wamefanya nao biashara ya mapenzi.
"Kwa sababu ni washikaji zangu siwezi kuwataja, mara nyingi nikiimba najua ukweli, kama wanaigiza waigize na kuachana na biashara nyingine.
Alisema kutokana na kutokuridhishwa na wasanii hao, ameamua kuingia rasmi katika tasnia ya filamu kwa kuandaa filamu itakayojulikana kwa jina X.
"Filamu hiyo itaelezea maisha ya vijana wa Manzese, Dar es Salaam na sehemu zingine ambazo kutokana na hali ya maisha kuwabana vijana, wamejikuta wakiingia katika biashara haramu bila kujua madhara yake," alisema.
Alipoulizwa kuhusu kuwashirikisha wasanii nyota ambao amewashutumu kuwa wameishiwa, alisema kuwa hana shaka na hilo kwa wale wasanii wa kazi atawatumia.
Alisema muswada wa filamu hiyo umekamilika na sasa kazi ya kurekodi itaanza hivi karibuni.
Chanzo cha habari ni Gazeti la mwanaspoti

No comments:
Post a Comment