EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 23, 2012

Hivi sasa wako Watanzania zaidi ya 100 katika jela za China - Balozi Marmo

UKAHABA na usafirishaji wa dawa za kulevya unaofanywa na baadhi ya Watanzania ni moja ya dosari zinazotia doa uhusiano kati ya Tanzania na China.

Watanzania zaidi ya 100 wako kwenye magereza ya China wakitumikia vifungo kwa makosa ya kukutwa na dawa za kulevya, huku wasichana wanane wakirejeshwa nyumbani siku chache zilizopita kutokana na ukahaba.


Balozi wa Tanzania nchini China, Philip Marmo alibainisha hayo mwishoni mwa wiki iliyopita katika mkutano uliofanyika nyumbani kwake jijini hapa.

Mkutano huo uliambatana na chakula cha mchana, ukiwa ni maalumu kwa ajili ya Watanzania waliokuwa wakihudhuria Mkutano wa Tano wa Mawaziri wa Ushirikiano kati ya China na Tanzania (FOCAC) uliofanyika Alhamisi na Ijumaa wiki iliyopita.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, John Haule na wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Balozi Herbert Mhango.

Aidha, walikuwapo watendaji wakuu kadhaa wa mashirika ya umma, taasisi za umma, sekta binafsi na wafanyabiashara wa Tanzania. Balozi Marmo alisema Tanzania inajivunia uhusiano wa muda mrefu na China tangu miaka ya sitini, ilipofungua ubalozi wake Aprili 26, 1964, lakini katika siku za karibuni umekumbwa na dosari hizo mbili. “Kwa kweli hili la dawa za kulevya, linaumiza vichwa sana.


Hapa ukiwa na dawa za kulevya hufiki popote, wako makini sana. Ukikamatwa hakuna msamaha, adhabu kubwa ni kifo, kwao ni kosa kubwa,” alisema.

Balozi Marmo aliongeza: “Dawa za kulevya kwao ni suala la usalama wa Taifa, ni vigumu kuanzisha mjadala katika suala hili. Katika siku za karibuni, kumekuwa na ongezeko la vijana wetu wanaoshughulika na mihadarati.”

Alisema cha kushangaza vijana hao wanapokamatwa, pasipoti zao huonesha kuwa hawatoki Dar es Salaam, bali katika miji mingine duniani.

“Halafu si kwamba hawa wanaokamatwa wanatoka Dar es Salaam, hapana … utakuta wanatoka Istanbul, Ankara, Rio de Janeiro, Pakistani; baadaye, ndio unajua wanasema tunatoka Kinondoni, Magomeni Mapipa, Tanga, Zanzibar na Kigoma,” aliongeza Balozi.

“Hivi sasa wako Watanzania zaidi ya 100 katika jela za China. Masikini wanatumiwa tu, wengine na wafanyabiashara wakubwa tu, wengine watoto wa wakubwa,” alibainisha zaidi Balozi Marmo. Alisema dosari nyingine katika siku za karibuni, ni wasichana kutoka Tanzania kujihusisha na biashara ya ukahaba China.


“Kuna hili la wanawake wetu kujihusisha na ukahaba … hapa haikubaliki, tayari wapo wanane wanarudishwa nyumbani, wamepewa siku nane za hifadhi kabla ya kuondoka,” alisema Balozi Marmo. “Wenyeji wanatuheshimu, wenzao wa Kenya na Uganda wamepewa siku tatu tu. Kwa kweli, hali hii inaharibu uhusiano wetu mzuri na China.”

Alisema Wachina wanaipenda sana Tanzania na wanaiona Tanzania kuwa sehemu nzuri ya kuwekeza na kufanya biashara, hivyo ni vyema fursa hiyo ikatumiwa vizuri badala ya kuchafua jina la nchi.


Alikerwa pia na alichoeleza kuwa ni biashara ndogo zinazofanywa na Watanzania, hasa wanawake kwa kubeba mabegi, badala ya kuchangamkia biashara kubwa na wenzao wa Taifa hili la Asia.

“Biashara tunazofanya ni ndogo sana, akinamama wanabeba mabegi tu, hii si biashara. Tulipaswa kufanya biashara ya makontena kupeleka nyumbani,” alieleza Balozi Marmo ambaye yuko Beijing takriban miezi mitatu sasa tangu ateuliwe kushika wadhifa huo.


Balozi Marmo aliwataka Watanzania kutumia urafiki na uhusiano mzuri kati ya Tanzania na China kufanya biashara kwa manufaa yao na Taifa. Mwito huo uliungwa mkono na mawaziri Membe na Teu ambao waliwataka wafanyabiashara hao na Watanzania kwa jumla, kuchangamkia fursa zinazopatikana China.

Katika miaka ya karibuni, China imekuwa mshirika mpya wa mataifa ya Afrika katika maendeleo, na imekuwa ikifadhili miradi mingi kuanzia elimu hadi masuala ya michezo na utamaduni.
via HabariLeo

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate