Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi-Zanzibar
Jeshi la Polisi Zanzibar linawashikilia wafanyakazi sita wa meli ya MV Skagit akiwemo mmiliki wake Bw. Said
Abdulrahman pamoja na Nahodha wa meli hiyo Bw. Mussa Makame Mussa na wanahojiwa kufuatia tukio la ajali ya meli hiyo
iliyosababisha vifo vya baadhi ya abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda Bandari ya
Zanzibar.
Watuhumiwa hao walikuwa wakihojiwa katika Ofisi za Upelelezi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi mjini Zanzibar ambapo Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, ACP Yusuph Ilembo, amesema watuhumiwa hao wawataweza kufikishwa
mahakamani kujibu mashtaka yanayowakabili.
Kamanda Ilembo amesema kuwa Makachero wa Jeshi la Polisi wanaendelea na uchunguzi na kutafuta taarifa nyingine
zinazohusiana na tukio hilo.
Hata hivyo, Nahodha wa zamu siku ya tukio hilo la kupinduka na kuzama kwa meli hiyo ya MV Skagit, Bw.Mussa Makame
Hata hivyo, Nahodha wa zamu siku ya tukio hilo la kupinduka na kuzama kwa meli hiyo ya MV Skagit, Bw.Mussa Makame
Mussa, ameelezea kwa ufupi jinsi ajali hiyo ilivyotokea na namna yeye alivyonusurika katika ajali hiyo.
Amesema kuwa ajali hiyo ilitokea baada ya kupigwa na dharuba na mawimbi yaliyoambatana na upepo mkali, ambapo yeye
alinusurika kufa maji baada ya kuruka kwa kutumia mlango wa mbele wa meli hiyo na kuanza kuogelea ambapo
alijichanganya pamoja na na abiria wengine walionusurika na kuokolewa na vyombo vya uokozi.
Wakati huo huo, Wapiga mbizi wa Vikosi vya Ulinzi na usalama siku ya jana wamefanikiwa kuzupata maiti ngingine za watu watano
Wakati huo huo, Wapiga mbizi wa Vikosi vya Ulinzi na usalama siku ya jana wamefanikiwa kuzupata maiti ngingine za watu watano
akiwemo mwanamke mmoja na wanaume wanne.
Katika upekuzi wa maiti hizo, Makachero wa Polisi walibaini kitambulicho cha kupigia kura kutoka kwa mmoja ya mwili
wa marehemu kitambulicho kilichokuwa na jina la Philip John Busiya aliyezaliwaq mwaka 1977 katika kijiji cha
Mapilinga kilichopo katika Kata ya Igokelo wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

No comments:
Post a Comment