EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 17, 2012

Waziri atishiwa kuuawa ....Asema ni baada ya kubomoa nyumba za vigogo

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Terezya Huvisa, amesema ametishiwa kuuawa endapo ataendelea na zoezi la kubomoa nyumba za watu zilizo kwenye maeneo oevu.
Madai hayo aliyatoa jana mjini hapa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema amepigiwa simu za vitisho hivyo kwa lengo la kukwamisha jitihada zake za kuwashughulikia wanaovunja sheria.
Alisema baada ya kupata vitisho hivyo, aliamua kuwapigia simu lakini simu hizo hazikupatikana jambo lililomfanya kuvipuuzia vitisho hivyo.

“Sijaviripoti polisi vitisho, najua lengo lao lilikuwa kunitisha ili nisiendelee na mkakati wa kuwabomolea nyumba wale waliojenga kwa kukiuka sheria, wanajidanganya nitaendelea kuwabomolea,” alisema.
Alisema mtu yeyote mwenye jambo lenye tija na masilahi kwa taifa kamwe asingesita kumpigia simu na ikiwezekana kwenda kumuona juu ya bomoabomoa lakini waliompa vitisho hivyo ni ‘feki’.
Waziri huyo aliongeza kuwa Mwanasheria la Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira (NEMC), Heche Manchare, naye alipewa vitisho pamoja na kupigwa na watu waliokuwa wamevalia vitambaa usoni kwa lengo la kuficha sura zao.

Alibainisha kuwa tukio hilo waliripoti kwa Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, ambaye aliwaambia walifikishe polisi lifanyiwe uchunguzi zaidi.
Aliongeza kuwa pamoja na vitisho hivyo kamwe wizara yake haitarudi nyuma katika zoezi la kuwabomolea nyumba, hoteli au wawekezaji wowote wale waliojenga kwenye maeneo oevu.
“Hili ni zoezi gumu sana linalohitaji ujasiri na umakini mkubwa sana, sisi hatutamuonea mtu yeyote, tumedhamiria kufanya kazi zetu kwa nguvu hatarudi nyuma,” alisema.
Wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya Ndani, Emanuel Nchimbi, aliwataka viongozi na wananchi wote wanaopata vitisho kuwasiliana na polisi ili hatua zichukuliwe.

Katika hatua nyingine, serikali imeeleza kupata hasara ya sh bilioni 50 kwenye utekelezaji wa zoezi la bomoabomoa katika fukwe za kawe na mbezi jijini Dar es Salaam.
Waziri Huvisa, alisema kuwa kiasi hicho cha fedha ambacho serikali imekitumia ni kikubwa sana na kitalipwa na wamiliki wa nyumba hizo ambao walijenga kinyume cha sheria na watazigawanya kwa viwango mbalimbali kutokana na kila nyumba ilipokuwa imefikia.

Alisema kuwa wizaya yake ilishirikiana na Maliasili na Utalii, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Manispaa ya Kinondoni ambapo jumla ya nyumba saba na uzio nane zilibomolewa na ujenzi uliokuwa unaendelea kwenye mkondo wa mto umebomolewa.
Alisema kuwa ubomoaji huu ni utekelezaji wa sheria ya mwaka 2004 kutokana na wananchi hao kukaidi na kutokutekelezwa kwa maagizo mbalimbali ya kutoendelea na ujenzi yaliyotolewa kwa wahusika.

“Nawataka wale wote waliojenga na wanaoendelea kujenga kwenye vyanzo vya maji, kando kando ya bahari, maziwa, mito na mabwawa na misitu inayolindwa kisheria kuondoka mara moja na endapo watakiuka maagizo hayo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao,” alisema waziri huyo.
Alifafanua kuwa hatua zitakazochukuliwa dhidi yao moja wapo ni kuwabomolea nyumba zao na kuwaondoa katika maeneo hayo na kwamba watatakiwa kulipia gharama zote zitakazohusu ubomoji huo.
Waziri alisema kuwa agizo hilo pia linawahusu wakulima na wafugaji wanaofanya shughuli zao katika vyanzo vya maji.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate