EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 17, 2012

SIRI MPYA ZAFICHUKA SAKATA LA NDOA YA DK.SLAA NA JOSEPHINE


                   
Dk. Willibroad Slaa na mchumba wake, Josephine Mshumbushi.
Josephine na Mahimbo siku ya ndoa yao.

Hati ya talaka kati ya  Josephine Mshumbushi na Aminieli Mahimbo.
Na Makongoro Oging’
SAKATA la ndoa ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa na mchumba wake, Josephine Mshumbushi limefichua siri mpya kuhusu maisha yao ya kimapenzi.
Siri hiyo, inahusu historia ya mateso aliyowahi kuyapata Dk. Slaa kutoka kwa mwanamke ambaye jina lake linahifadhiwa, kabla ya kuamua kuinua mikono na kudondokea kwa Josephine.
Imebainika kuwa wakati Slaa analo lake la kuteswa na mwanamke wake, Josephine naye ana siri inayomuumiza kutokana na yale aliyotendewa na mwanaume wake (jina tunalo), aliyekuwa naye kabla ya kutua kwa mwanasiasa huyo.

Josephine, amekiri wazi kwamba mwanaume wake aliyepita, alimtesa na kumdhalilisha kiasi cha kumfanya kuchangia mapenzi na wasaidizi wa kazi za nyumbani (ma-house girl).
Dk. Slaa, alipozungumza na mwandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwake, Tegeta, Dar es Salaam, alikiri kuteswa na mwanamke aliyewahi kuwa naye kabla ya Josephine kisha akaelekeza kila kitu kuhusu maisha yao na uhusiano wao, kizungumzwe na mchumba wake huyo.
Akieleza mambo kwa mtindo wa kuchambua, Josephine alisema, haoni sababu ya kutoolewa na Dk. Slaa, kwani anampenda kupita kiasi na kwamba kiongozi huyo alikutatanaye Dodoma akiwa amekondeana kwa mawazo kutokana na mateso ya mwanamke huyo (jina bado tunalihifadhi).

“Mimi na Dk. Slaa tulikutana bungeni. Mimi nilikuwa pale kama mtumishi wa bunge, yeye alikuwa pale kama mbunge wa Jimbo la Karatu. Uhusiano wetu ulianza kule. Sasa nimemtunza na amenenepeana watu wanaanza kumtamani. Huyu ni wangu.
“Watu wamuone Dk. Slaa hivi sasa, hapo kabla alikuwa anateseka. Hakuwa na mwili huu ambao watu wanamuona nao. Mwanamke wake wa zamani alikuwa anamnyanyasa, kila siku baba wa watu anashinda na kukesha kwa mawazo, sasa hivi katulia. Nampa huduma nzuri, nampikia mapochopocho ndiyo maana ananawiri,” alisema Josephine.

Aliendelea kusema, kama kuna watu wanaamini yeye hatafunga ndoa na Dk. Slaa, wanajidanganya, kwani wanazo haki za kimsingi za kutimiza azma yao.
“Mimi najua Slaa ana watoto aliozaa na mwanamke mwingine, hata mimi nimeishi na Slaa miaka minne na tumezaa mtoto mmoja. Nimeishi na Slaa bila ndoa kwa muda mrefu na sasa tumeamua tufunge ndoa Julai 21, mwaka huu,” alisema Josephine.
Aliendelea kusema: “Nitafurahi sana nikishatimiza hii azma ya kuolewa na Slaa. Ni mume mzuri hasa, namuomba Mungu akamilishe malengo yetu. Unajua huko nyuma niliwahi kuteswa na mwanaume, niliishi na mwanaume asiyejua thamani ya mke.

“Huyo mwanaume alikuwa anasababisha nichangie mapenzi na ma-house girl, kwani kila house girl niliyemuajiri, alitembea naye. Sasa hivi yote hayo yamekwisha. Dk. Slaa anajiheshimu, sina tena vurugu za mwanaume wangu kutembea na house girl.”

Kuhusu matarajio ya kimaisha, Josephine alisema kuwa anaamini panapo majaliwa baada ya kufunga ndoa na Dk. Slaa, wataishi raha mustarehe kwa sababu wanaelewana vizuri.
“Raha ya maisha ya ndoa ni kuelewana, ndiyo maana nasema sioni sababu ya mimi na Dk. Slaa kutofunga ndoa. Tunapendana na kuelewana sana. Dk. Slaa akiondoka kwangu, hatapata mwanamke atakayeelewana naye kama mimi. Hata mimi siwezi kumpata mwanaume wa kuelewana naye kama ilivyo kwangu na Slaa.

“Jambo pekee ninaloweza kuwaomba Watanzania ni kutuombea tufunge ndoa yetu salama, atukinge na maradhi ili tuendelee kuishi raha mustarehe na tuendelee kutetea masilahi yao,” alisema.
Aliongeza kuwa maandalizi ya ndoa yao yamekamilika na kilichobaki kwa sasa ni siku ifike ili watawazwe rasmi kuwa mke na mume.

KILICHOPO JUU YA DAWATI
Wakati Josephine na Slaa, wakieleza mipango yao ya ndoa, kwa upande mwingine, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Mkoa wa Manyara, Rose Kamili, amewasilisha pingamizi mahakama kuu, akidai kuwa, Dk. Slaa ni mume wake halali.
Rose ambaye ni mzazi mwenza wa Dk. Slaa, aliwasilisha hati ya pingamizi Mahakama Kuu, akitaka pia alipwe fidia ya shilingi milioni 550.

Alitaka Dk. Slaa amlipe shilingi milioni 50 kwa kitendo chake cha kumtelekeza na watoto, akaomba pia Josephine amlipe shilingi milioni 500 kwa kitendo cha kumsababishia maumivu makali baada ya kumchukulia mume wake.
Mbunge huyo alidai kuwa yeye na Dk. Slaa walifunga ndoa ya kimila tangu miaka ya 1980, baada ya katibu huyo wa Chadema kuachana na ukasisi wa Kanisa Katoliki (Upadri), hivyo yeye ni mke halali mwenye stahili zote.

UNAKUMBUKA SAKATA LA MAHIMBO?
Awali, ilionekana kwamba pingamizi la ndoa ya Dk. Slaa na Josephine lingetoka kwa mwanaume anayeitwa Aminieli Mahimbo.
Mahimbo, alikuwa mume wa ndoa wa Josephine na ndoa yao ilifungwa mwaka 2002.
Hata hivyo, Uwazi limenasa talaka inayowatenganisha rasmi Josephine na Mahimbo, iliyotolewa na Mahakama ya Mwanzo, Manzese, Dar es Salaam, Aprili 16, mwaka huu, hivyo kuthibitisha kwamba hakuna kizuizi tena upande huo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate