EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, September 1, 2012

SENSA YASOGEZWA MBELE HADI JUMAMOSI YA TAREHE 8-09-2012


Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imeongeza mbele tarehe za kumaliza kazi ya sensa ya watu na makazi hadi Jumamosi ya tarehe 8 septemba mwaka huu ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi aliyebaki anahesabiwa.

Kauli hiyo imetolewa leo(jana) na Kamishna wa Sensa kutoka NBS Hajjat Amina Mrisho Said wakati akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu masuala mbalimbali yaliyohusu kazi nzima ya kuhesabu watu na makazi inaendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Alisema kuwa ni vema wananchi ambao hawajafikiwa na makarani wa sensa watoe taarifa katika Ofisi za Serikali za Mitaa au Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa ajili ya kuhesabiwa.

Hajjat Amina alisema taarifa zinazotakiwa ni pamoja na taarifa za wanakaya waliolala katika kaya yao usiku wa kuamkia tarehe 26 Agosti mwaka huu.

Alitoa wito kwa wale ambao hawajaandikishwa hadi hivi sasa wanatakiwa watume taarifa kwa namba 2122724, 0754583415, 2129622 ,0713335429,0713574622 na 0713312699 .

Hajjat aliongeza kuwa katika taarifa watakazopeleka ni vema wakaeleza mitaa au kijiji au kitongoji gani walipo ili iwe rahisi kwa NBS kutambua karani mhusika na kumwelekeza afanye kazi hiyo.

Aidha , Kamishna hiyo alisema kuwa malipo ya makarani yalishafanyika kwa awamu ya kwanza kulingana na mkataba na wanataraji kuwalipa awamu ya pili mara baada ya kazi zao kuhakikiwa na wasimamizi wao.

Aliongeza kuwa kwa wasimamizi watalipwa baada ya kazi zao kukamilika na kuhakikiwa na waratibu katika ngazi za wilaya.

Kuhusu malipo ya wenyeviti wa vijiji , vitongoji na mitaa ,alisema fedha zao wasishapelekwa siku nyingi na maelekezo ya namna ya kuzigawa yalipelekwa kwa waratibu wa Sensa wa mikoa na wilaya ambao walipaswa kuwa wameshalipa ili kuepuka manung’uniko.

Katika hatua nyingine Kamishna wa Sensa huyo amewaonya kuwa Karani yoyote atakayechakachua taarifa na ikathibitika hilo atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria na kuongeza kuwa NBS inafuatilia taarifa kutoka Dodoma eneo la Kisasa kuwa kuna Karani amekwenda kwenye kaya lakini alikuwa haulizi maswali.

Wakati huo huo Kamishna wa Sensa Hajjat Amina alisema kuwa wale viongozi wengi waliokuwa wakiwa hamasisha wenzao wasihesabiwe , wamehesababiwa kwa hiari baada ya kutoa ushirikiano wa kutosha ikiwemo kuacha taarifa muhimu zilizohitajiwa ikiwemo zile zilihitajika katika madodoso. Kwa wale ambao hawakuwakuta waliweka alama maalum ili wawarudie mara ya pili.
Na : Tiganya Vincent-  MAELEZO-Dar es salaam

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate