EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, December 2, 2012

MALI ZA MAREHEMU SHARO MILIONEA ZAPATIKANA JIONEE KWA PICHA.

Baadhi ya vitu vya marehemu Sharo milionea vilivyokamatwa baada ya msako mkali baina ya Polisi na wananchi wa Kijiji Songa Kibaoni.

Na Mashaka Mhando,Tanga


WATU wanaosadikiwa kuiba vitu vya marehemu Hussein Mkiety maarufu kwa jina la 'Sharo Milionea' aliyefariki kwa ajali ya gari katika kijiji cha Songa Kibaoni wilayani Muheza Novemba 26 mwaka huu, wamesalimisha baadhi ya vitu hivyo kwa mwenyekiti wa Kijiji hicho huku wakiendelea kuishi mafichoni kuogopa kutiwa mbaroni.



Watu hao wamesalimisha vitu hivyo baada ya Mkuu wa wilaya ya Muheza Subira Mgalu ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama kuwatangazia kwamba wale wote waliomwibia marehemu watasakwa na kuchukuliwa hatua za kisheria kufutia kitendo walichokifanya kutokuwa cha kiungwana.


Mkuu huyo pamoja na jeshi la polisi wilayani humo waliendesha msako juzi usiku lakini hawakuweza kuwakuta watu baada ya kuzihama nyumba zao kuogopa kutiwa mbaroni na mkuu huyo kuwalazimsha baadhi ya familia walizozikuta kuendesha zoezi la kuwataja watu wanaohofiwa kwamba huenda watakuwa wamchukua vitu hivyo.


Kamanda wa polisi mkoani Tanga ACP Constatine Masawe, aliwaeleza waandishi wa habari ofisini kwake kuwa, usiku wa kuamkia juzi mwenyekiti wa kijiji hicho Abdi Zawadi alipelekewa vifaa mbalimbali ikiwemo nguo ambazo marehemu alikuwa amezivaa pamoja na spea tairi ambalo waliling'oa na kutokomea porini.



Kamanda huyo alitaja vitu vilivyokabidhiwa kwa mwenyekiti huyo kuwa ni pamoja na begi lake lililokuwa na 'viwaro' nguo zake, betri ya gari hilo lililokuwa na namba T 478 BVR aina ya Toyota Harrier, saa yake ya mkononi, simu yake aina ya Blackberry na redio ya gari iliyokuwa pia imeng'olewa na wezi hao.


Kamanda huyo alisema vitu hivyo vilipelekwa na mtu mmoja ambaye kwasasa jeshi hilo linashindwa kumtaja jina lake kwa vile alijitambulisha kwamba ana undugu na wezi hao ambao walimpa vitu hivyo avipeleke kwa uongozi wa kijiji hicho hatua ambayo alidai kwamba wanafanya uchunguzi ili kuwatia nguvuni wale wote waliohusika na tukio hilo.


Alisema waliweka mtego baada ya kusikia kwamba kuna mwizi mmoja wapo anaitafutia mteja simu ya mkononi ya marehemu lakini wakati wameweka mtego huo kijana huyo alipokuwa akijadiliana bei na mtu waliyemweka, alibaini na alipompa mkononi alikimbia vichakani kuogopa kukamatwa.


Kamanda huyo aliwashukuru baadhi ya wananchi wa kijiji hicho pamoja na Mkuu wa wilaya kuhakikisha wanashirikiana na jeshi hilo ili kuwabaini na kuwakamata wote waliohusika katika tukio hilo ambalo limetokea huku wananchi kadhaa wakiomboleza kifo cha msanii huyo ambaye alizikwa kijijini kwao Lusanga wilayani Muheza juzi.


Katika hatua nyingine kamanda huyo alisema katika matukio ya ajali yaliyotokea mwezi huu wa Novemba jumla ya ajali 10 zilitokea ambazo zimesababisha vifo ni 7 na zilizosababisha watu kujeruhiwa ni tatu, kati ya hizo watu 12 walipoteza maisha na wengine wanane walijeruhiwa.


Kamanda Masawe alisema jumla ya makosa 2,365 yalitendeka na kupigwa faini iliyosababisha serikali kujiingiza kiasi cha sh. 70,950,000 hatua ambayo kamnada huyo alisema haioneshi kwamba watumiaji barabara wamekuwa wakifuata wakitii sheria za usalama barabarani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate