EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, December 10, 2012

TAMKO LA DCPC JUU YA MWANDISHI KUPIGWA RISASI.


Kufuatia kupigwa risasi, kujeruhiwa begani na kulazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa mwandishi wa Tanzania Daima Bwana Shabani Matutu (30) ambaye pia ni mwanachama hai wa Dar City Press Club(DCPC), uongozi wa Klabu uliamua kufuatilia tukio hilo kwa karibu ili kujua na kuhakiki kwa kina yaliyotokea na sababu zilizopelekea hayo kutokea.

Kutokana na hayo DCPC imebaini yafuatayo. 

1. Ni kweli kwamba Shabaan matutu(30) alipigwa risasi na askari wa jeshi la Polisi mwenye namba F.8991 D/C Idrissa nyumbani kwa Shabaan kimakosa baada ya askari huyo na wenzake wanne kufungua kwa nguvu na bila ya kujitambulisha kwa mwenye nyumba (Shabaan na Mkewe) licha ya kuombwa kufanya hivyo kabla.

2. Kuna maelezo yanayokinzana katika kuelezea jinsi tukio hilo lilivyotokea kwa pande mbili zinazohusika yaani maelezo ya shabaan na ya polisi.

3. Kwamba sababu za askari polisi hao kufanya hivyo hazikuwa zimefanyiwa uchunguzi wa kutosha hadi kujiridhisha kuchukua hatua hiyo hivyo hata wao walikiri kukosea pamoja na kueleza kwamba Shabaan ndiye aliyeaanza kuwashambulia askari Polisi kabla ya wao kumjeruhi kwa risasi.

4. Shabaan mpaka sasa anaendelea na matibabu licha ya kuuguza majeraha aliyosababishiwa na polisi na kwamba ameshauriwa kitaalamu kupumzika nay eye binafsi ameomba asibughudhiwe ili afya yake irejee haraka na kwamba pindi atakapokuwa katika hali nzuri zaidi ya sasa kwa mujibu wa ushauri huo wa kitabibu, atawasiliana na yeyote wakiwemo polisi ambao wamekuwa wakimmghasi kwa kuja kumhoji mara kwa mara.

Kwa sababu hizo basi Dar es salaam City Press Club

1. Tunaiomba Serikali na mamlaka za juu zaidi ya jeshi la Polisi hususan Wizara ya mambo ya ndani ifanye uchunguzi wa kina na huru wenye kuhusisha taasisi wakilishi katika jamii juu ya tukio hilo na kulichunguza jeshi la polisi linavyofanya kazi zake kwa kuzingatia kanuni na sheria.

2. Tunalitaka Jeshi la Polisi liache mara moja kutuma askari wake kwenda kwa Shabaan kwa lengo la kumhoji ama kutaka atoe maelezo yake kwa viongozi wa jeshi hilo ilhari walishamtuhumu na kueleza kuwa aliwashambulia Polisi kwa Panga kabla ya wao kumfyatulia risasi. Tunasema hivi kwa kuzingatia kanuni za afya na haki za msingi za binadamu.

3. Tunalitaka Jeshi la Polisi liueleze umma bila kuficha ukweli na kwa jinsi ile ile ambayo lilitoa taarifa mara baada ya tukio, lieleze kwa nini linatumia habari na vyanzo dhanifu kujeruhi na kuhatarisha maisha ya raia wasio na kosa huku likitoa maelezo yasiyofanyiwa uchunguzi.

4. Mwisho tunalitaka jeshi la Polisi lenyewe lijitafiti na kujipanga upya ili liweze kufanya kazi kisayansi na weledi kama ambavyo viongozi wake wamekuwa wakijinadi mbele ya vyombo vya habari. Tamko hili limetolewa leo Tarehe 08/Desemba/2012.

Joseph Kayinga 
Katibu Mkuu-DCPC

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate