EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, December 16, 2012

Wananchi waua polisi wawili,Ni baada ya askari kumuua fundi pikipiki.

VITENDO vya wananchi kujichukulia sheria mikononi vinaendelea kushika kasi ambapo askari wawili wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, wanadaiwa kuuwa na wananchi wenye hasira kali jana.
Taarifa ambazo zililifikia Tanzania Daima Jumapili wakati tukielekea mitamboni jioni, zilisema kuwa mauaji hayo yalifanyika baada ya wananchi hao kuvamia na kukichoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani humo baada ya askari hao kudaiwa kumpiga risasi fundi wa pikipiki.
Kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo lilitokea mchana wakati askari kadhaa wa kitengo cha usalama barabarani walipofika kwa fundi pikipiki huyo na kutaka kuichukua pikipiki aliyokuwa akiitengeneza kwa madai kuwa ilikuwa na makosa.

Kwamba fundi huyo aligoma na kueleza kuwa asubiriwe mwenye pikipiki ili kuepuka kudaiwa chombo hicho cha usafiri.
Mmoja wa mashuhuda hao, aliyatambulika kwa jina moja la Libela, alidai kuwa baada ya mvutano wa muda mfupi, askari hao walifyatua risasi na kumpiga fundi huyo mguuni na kifuani, hivyo kusababisha kifo chake.
Aliongeza kuwa, tukio hilo liliwapandisha hasira wananchi na kuwafukuza askari hao waliokimbilia katika kituo hicho cha polisi.

 Lebela alifafanua kuwa, wananchi hao waliamua kukichoma moto kituo hicho hatua iliyosababisha askari waliokuwemo kutoka na kukimbia kila mmoja na muelekeo wake.
Alisema kuwa askari aliyetajwa kwa jina la Koplo Paschal alianguka wakati akijinusuru, hivyo kuvamiwa na wananchi waliokuwa na zana mbalimbali za jadi ambazo walitumia kumshambulia na kumuua papo hapo.
Wananchi hao pia wanadaiwa kumfuata askari mwingine anayetajwa kwa jina la Pc Alex aliyekuwa amekimbilia kwenye nyumba ya mwananchi mmoja na kumtoa kwa nguvu na kisha kuanza kumshambulia hadi kumuua.

Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku ya soko katika eneo hilo la Mugoma linalopakana na nchi jirani ya Burundi ambapo raia wa Tanzania na Burundi hukutana na kufanya biashara jirani na kituo hicho cha polisi.
Kutokana na kuchomwa moto kwa kituo hicho, nyaraka mbalimbali zinadaiwa kuteketea, huku pikipiki na baiskeli kadhaa zilizokuwa kituoni hapo nazo zikiteketea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi, hakuweza kupatikana kuthibitisha tukio hilo kutokana na simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa.Via TANZANIA DAIMA.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate