Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametoa wito kwa wapiganaji 
wote katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria kuacha mapigano 
kwa ajili ya kuthamini ubinaadamu.

Ban ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kukusanya fedha 
kiasi bilioni 1.5 kwa ajili ya wakimbizi wasyria, unaofanyika nchini 
Kuwait. Amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa zaidi ya wasyria milioni 4
 wanahitaji msaada wa dharura,na kwamba raia wa kawaida wanateseka 
kupita kiasi, hivyo wanahitaji kupatiwa msaada sahihi. Umoja wa Mataifa 
unapanga kuwapatia mahitaji ya msingi raia milioni 4 waliyoko ndani ya 
Syria, na zaidi ya wakimbizi 650,000 waliyoyakimbia makaazi yao kutokana
 na mgogoro huo unaokaribia miaka miwili.
 
 
                        Mfalme wa Kuwait, Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah.
Kuwait yatoa dola milioni 300
Wawakilishi kutoka mataifa zaidi ya 60 wanahudhuria mkutano huo wa 
kimataifa kusikia maombi ya Umoja wa Mataifa ya kuchangisha dola bilioni
 1.5. Maafisa wa umoja huo wanasema wana kiasi kidogo tu cha fedha 
zinazohitajika, ingawa ahadi kutoka mataifa na mashirika mbalimbali 
ziliongezeka kabla ya kuanza kwa mkutano huo. Umoja wa Ulaya na marekani
 ziliahidi kutoa jumla ya dola milioni 400.
Mfalme wa Kuwait Sheikh Sabah al-Ahmad al-Saba, naye ametangaza leo kuwa
 atachangia dola milioni 300. Sheikh al-Saba ameuambia mkutano huo kuwa 
taarifa za kutisha juu ya vurugu zinazoendelea nchini Syria,zinazua 
maswal ijuu ya mustakabali wa Syria, na kuongeza kuwa juhudi za msaada 
zinapaswa kuongezwa mara mbili. Umoja wa Falmeza Kiarabu nao ulitarajiwa
 kutoa kiasi cha dolamilioni 300.
Brahimi alitaka baraza la usalama kuchukua hatua sasa
Mjumbe wa kimataifa wa amani katika mgogoro wa Syria, Lakhdar Brahimi 
alisema vita nchini Syria vimefikia kiwango cha kutisha ambacho 
hakijawahi kushuhudiwa, baada ya wanaume kadhaa kukutwa wakiwa 
wamechinjwa. Brahimi aliliambia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa 
jana Jumanne, kuwa linapaswa kuchukua hatua sasa hivi kukomesha mauaji 
ya kutisha, kama yanayoshuhudiwa hivi sasa ikiwa ni pamoja na yale ya 
wanaume wasiyopungua 78, kilamoja wao akiwa ameuawa kwa kupigwa risasi 
moja na kisha kutupwa mtoni katika mji wa Aleppo.
 
 
Mama akimshika mtoto wake aliyejeruhiwa akisubiri matibabu katika hospitali nchini Syria.
Baada ya miezi 22 tangu kuanza kwa mgogoro huo, watu zaidi ya elfu 60 
wameuawa kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.Brahimi alisema uhalali wa 
utawala wa Assad umeharibika kabisaa kiasi cha kutokarabatika,lakini 
alionya kuwa bado unaweza kuendelea kun'gan'gania madarakani. Brahimi 
alisema vikosi vya serikali na waasi wote wanatenda uhalifu katika 
mgogoro huo.
Baraza la usalama bado limegawanyika
Lakini balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Suzan Rice, alisema 
masuala ambayo yamekuwa yakiligawa baraza la usalama yameendelea kuwepo 
na hivyo hakuna njia rahisi ya kusonga mbele.Baraza la usalama la Umoja 
wa Mataifa limekabiliwa na mkwano juu ya Syria kwa zaidi ya mwaka 
moja.Urusu na China zimetilia guu maazimio matatu ya Baraza hilo 
yaliolenga kulaani ukandamizaji unaofanywa na utawala wa rais Assad.
Urusi inazishtumu nchi za magharibi kwa kutaka kubadilisha utawala 
nchini Syria kwa nguvu,na inasisitiza kuwa haiwezi kumlaazimisha Assad 
kuachia madaraka. Marekani na washirika wake wanaunga mkono msimamo wa 
upinzani,kuwa hakuwezi kuwa na mazungumzona Assad.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment