EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 31, 2013

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon wapiganaji Syria kuheshimu utu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametoa wito kwa wapiganaji wote katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria kuacha mapigano kwa ajili ya kuthamini ubinaadamu.
 Katibu Mkuu Ban Ki-moon.
Ban ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kukusanya fedha kiasi bilioni 1.5 kwa ajili ya wakimbizi wasyria, unaofanyika nchini Kuwait. Amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa zaidi ya wasyria milioni 4 wanahitaji msaada wa dharura,na kwamba raia wa kawaida wanateseka kupita kiasi, hivyo wanahitaji kupatiwa msaada sahihi. Umoja wa Mataifa unapanga kuwapatia mahitaji ya msingi raia milioni 4 waliyoko ndani ya Syria, na zaidi ya wakimbizi 650,000 waliyoyakimbia makaazi yao kutokana na mgogoro huo unaokaribia miaka miwili.

Mfalme wa Kuwait, Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah.  
                        Mfalme wa Kuwait, Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah.
 
Kuwait yatoa dola milioni 300
Wawakilishi kutoka mataifa zaidi ya 60 wanahudhuria mkutano huo wa kimataifa kusikia maombi ya Umoja wa Mataifa ya kuchangisha dola bilioni 1.5. Maafisa wa umoja huo wanasema wana kiasi kidogo tu cha fedha zinazohitajika, ingawa ahadi kutoka mataifa na mashirika mbalimbali ziliongezeka kabla ya kuanza kwa mkutano huo. Umoja wa Ulaya na marekani ziliahidi kutoa jumla ya dola milioni 400.
Mfalme wa Kuwait Sheikh Sabah al-Ahmad al-Saba, naye ametangaza leo kuwa atachangia dola milioni 300. Sheikh al-Saba ameuambia mkutano huo kuwa taarifa za kutisha juu ya vurugu zinazoendelea nchini Syria,zinazua maswal ijuu ya mustakabali wa Syria, na kuongeza kuwa juhudi za msaada zinapaswa kuongezwa mara mbili. Umoja wa Falmeza Kiarabu nao ulitarajiwa kutoa kiasi cha dolamilioni 300.
 
Brahimi alitaka baraza la usalama kuchukua hatua sasa
Mjumbe wa kimataifa wa amani katika mgogoro wa Syria, Lakhdar Brahimi alisema vita nchini Syria vimefikia kiwango cha kutisha ambacho hakijawahi kushuhudiwa, baada ya wanaume kadhaa kukutwa wakiwa wamechinjwa. Brahimi aliliambia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa jana Jumanne, kuwa linapaswa kuchukua hatua sasa hivi kukomesha mauaji ya kutisha, kama yanayoshuhudiwa hivi sasa ikiwa ni pamoja na yale ya wanaume wasiyopungua 78, kilamoja wao akiwa ameuawa kwa kupigwa risasi moja na kisha kutupwa mtoni katika mji wa Aleppo.
Mama akimshika mtoto wake aliyejeruhiwa akisubiri matibabu katika hospitali nchini Syria.
 
Mama akimshika mtoto wake aliyejeruhiwa akisubiri matibabu katika hospitali nchini Syria.
Baada ya miezi 22 tangu kuanza kwa mgogoro huo, watu zaidi ya elfu 60 wameuawa kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.Brahimi alisema uhalali wa utawala wa Assad umeharibika kabisaa kiasi cha kutokarabatika,lakini alionya kuwa bado unaweza kuendelea kun'gan'gania madarakani. Brahimi alisema vikosi vya serikali na waasi wote wanatenda uhalifu katika mgogoro huo.
Baraza la usalama bado limegawanyika
Lakini balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Suzan Rice, alisema masuala ambayo yamekuwa yakiligawa baraza la usalama yameendelea kuwepo na hivyo hakuna njia rahisi ya kusonga mbele.Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limekabiliwa na mkwano juu ya Syria kwa zaidi ya mwaka moja.Urusu na China zimetilia guu maazimio matatu ya Baraza hilo yaliolenga kulaani ukandamizaji unaofanywa na utawala wa rais Assad.
Urusi inazishtumu nchi za magharibi kwa kutaka kubadilisha utawala nchini Syria kwa nguvu,na inasisitiza kuwa haiwezi kumlaazimisha Assad kuachia madaraka. Marekani na washirika wake wanaunga mkono msimamo wa upinzani,kuwa hakuwezi kuwa na mazungumzona Assad.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate