Shirika la Maripota wasiokuwa na Mipaka limechapisha ripoti yake kuhusu 
uhuru wa vyombo vya habari kwa mwaka 2012.Barani Afrika Somalia inatajwa
 kuwa nchi hatari zaidi kwa waandishi habari.
Ripoti ya Maripota wasiokuwa na mipaka inaitaja Somalia kama mahala 
hatari kabisa kwa waandishi habari mnamo mwaka 2012 : waandishi habari 
18 waliouliwa nchini humo,naiwe kwa kujikuta mahala mabomu yalikokuwa 
yanaripuliwa au kwa kulengwa makusudi na wauwaji .Taifa hilo la pembe ya
 Afrika limeorodheshwa nafasi ya pili ya nchi hatari kwa waandishi 
habari baada ya Syria.

Nchini Eritrea,inayoburura mkia pia katika orodha 
hiyo kwa mwaka wa sita mfululizo,hakuna mwandishi habari aliyeuliwa 
lakini kuna baadhi walioachwa jela hadi kufa.Kuna waandishi habari 
wasiopungua 30 korokoroni nchini humo hali inayoifanya nchi hiyo 
iangaliwe kama jela kubwa kabisa ya waandishi habari barani Afrika.Kati 
ya wafungwa 11 wanaoshikiliwa jela tangu mwaka 2001,sabaa wameshafariki 
dunia kutoana na hali mbaya katika jela hizo au kwa kujiuwa wenyewe.
Afrika Mashariki pia inaangaliwa kama eneo la mchujo wa habari na 
kuandamwa waandishi habari.Sudan ya Omar al Bashir ambako magazeti 
yanazidi kufungwa na kamata kamata ya waandishi habari kuendelea msimu 
wa kiangazi,inashikilia nafasi ya 170 mkiani,huku Djibuti ambayo pia 
haina vyombo huru vya habari na inayomshikilia ripota wa kituo cha 
matangazo cha La Voix de Djibuti,ikikamata nafasi ya 167.
Licha ya 
kuachiwa huru waandishi habari wawwili wa kutoka Sweden,Ethiopia 
inakamata nafasi ya 137 kutokana na sheria zake za ukandamizaji 
zilizopitishwa mwaka 2009 na kwasababu ya kuendelea kuwashikilia 
kizuwizini baadhi ya waandishi habari wa kienyeji.
Tanzania imeangukia nafasi ya 70
 
 
 
Christian Mihr , mwenyekiti wa shirika la Maripota wasiokuwa na mipaka nchini Ujerumani
Christoph Dreyer wa shirika la Maripota wasiokuwa na mipaka kutoka 
Berlin anachambua hali ya mambo akisema:"Afrika mashariki hali ni 
tofauti.Maendeleo mabaya yameripotiwa Tanzania nchi ambayo hadi sasa 
ilikuwa ikisifiwa sana.Lakini katika mwaka 2012 imepoteza nafasi 36 na 
kuteleza hadi nafasi ya 70 kutokana na vifo viwili vya waandishi 
habari.Mmoja alikutikana amekufa,yadhihirika ameuliwa na mwengine 
ameuwawa wakati wa maandamano.Hii si hali nzuri kwa vyombo vya habari."
Wimbi la mageuzi halikuzisaidia sana nchi za kiarabu
 
 
Nembo ya Maripota wasiokuwa na Mipaka-tawi la Ujerumani
Miaka miwili baada ya wimbi la mageuzi katika nchi za kiarabu uhuru wa 
vyombo vya habari bado ni tete katika nchi nyingi ikiwa ni pamoja na 
Misri ambako waandishi habari na wanablogi bado waaendelea kuhujumuiwa 
,kukamatwa na kufikishwa mahakamani.Nchini Tunisia waandishi habari 
wanazidi kushambuliwa na serikali inakawia kutia njiani sheria mpya 
kuhusu vyombo vya habari.Libya baada ya kung'olewa madarakani utawala wa
 muammar Gaddafi inaonyekana kufanya vyema na kuchupa nafasi 23 hadi 
kuifikia nafasi ya 131.
Miongoni mwa nchi za Ulaya, Ujerumani inashikilia nafasi ya 17: Tatizo 
hapa linatokana na ukosefu wa fedha uliosababisha baaadhi ya vyombo vya 
habari kufungwa.Sababu nyengine inatokana na ile hali kwamba wajasiria 
mali uwekeza katika vyombo vya habari ili kuweza kuwa na usemi katika 
kile kinachoandikwa.
                                   CHANZO CHA HABARI NA DW 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment