EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 31, 2013

Tanzania yateleza katika orodha ya Maripota wasiokuwa na Mipaka

Shirika la Maripota wasiokuwa na Mipaka limechapisha ripoti yake kuhusu uhuru wa vyombo vya habari kwa mwaka 2012.Barani Afrika Somalia inatajwa kuwa nchi hatari zaidi kwa waandishi habari.

Ripoti ya Maripota wasiokuwa na mipaka inaitaja Somalia kama mahala hatari kabisa kwa waandishi habari mnamo mwaka 2012 : waandishi habari 18 waliouliwa nchini humo,naiwe kwa kujikuta mahala mabomu yalikokuwa yanaripuliwa au kwa kulengwa makusudi na wauwaji .Taifa hilo la pembe ya Afrika limeorodheshwa nafasi ya pili ya nchi hatari kwa waandishi habari baada ya Syria.
 
Nchini Eritrea,inayoburura mkia pia katika orodha hiyo kwa mwaka wa sita mfululizo,hakuna mwandishi habari aliyeuliwa lakini kuna baadhi walioachwa jela hadi kufa.Kuna waandishi habari wasiopungua 30 korokoroni nchini humo hali inayoifanya nchi hiyo iangaliwe kama jela kubwa kabisa ya waandishi habari barani Afrika.Kati ya wafungwa 11 wanaoshikiliwa jela tangu mwaka 2001,sabaa wameshafariki dunia kutoana na hali mbaya katika jela hizo au kwa kujiuwa wenyewe.

Afrika Mashariki pia inaangaliwa kama eneo la mchujo wa habari na kuandamwa waandishi habari.Sudan ya Omar al Bashir ambako magazeti yanazidi kufungwa na kamata kamata ya waandishi habari kuendelea msimu wa kiangazi,inashikilia nafasi ya 170 mkiani,huku Djibuti ambayo pia haina vyombo huru vya habari na inayomshikilia ripota wa kituo cha matangazo cha La Voix de Djibuti,ikikamata nafasi ya 167.

Licha ya kuachiwa huru waandishi habari wawwili wa kutoka Sweden,Ethiopia inakamata nafasi ya 137 kutokana na sheria zake za ukandamizaji zilizopitishwa mwaka 2009 na kwasababu ya kuendelea kuwashikilia kizuwizini baadhi ya waandishi habari wa kienyeji.
Tanzania imeangukia nafasi ya 70
 
  Christian Mihr , mwenyekiti wa shirika la Maripota wasiokuwa na mipaka nchini Ujerumani
Christoph Dreyer wa shirika la Maripota wasiokuwa na mipaka kutoka Berlin anachambua hali ya mambo akisema:"Afrika mashariki hali ni tofauti.Maendeleo mabaya yameripotiwa Tanzania nchi ambayo hadi sasa ilikuwa ikisifiwa sana.Lakini katika mwaka 2012 imepoteza nafasi 36 na kuteleza hadi nafasi ya 70 kutokana na vifo viwili vya waandishi habari.Mmoja alikutikana amekufa,yadhihirika ameuliwa na mwengine ameuwawa wakati wa maandamano.Hii si hali nzuri kwa vyombo vya habari."
Wimbi la mageuzi halikuzisaidia sana nchi za kiarabu
 
Nembo ya Maripota wasiokuwa na Mipaka-tawi la Ujerumani
Miaka miwili baada ya wimbi la mageuzi katika nchi za kiarabu uhuru wa vyombo vya habari bado ni tete katika nchi nyingi ikiwa ni pamoja na Misri ambako waandishi habari na wanablogi bado waaendelea kuhujumuiwa ,kukamatwa na kufikishwa mahakamani.Nchini Tunisia waandishi habari wanazidi kushambuliwa na serikali inakawia kutia njiani sheria mpya kuhusu vyombo vya habari.Libya baada ya kung'olewa madarakani utawala wa muammar Gaddafi inaonyekana kufanya vyema na kuchupa nafasi 23 hadi kuifikia nafasi ya 131.
Miongoni mwa nchi za Ulaya, Ujerumani inashikilia nafasi ya 17: Tatizo hapa linatokana na ukosefu wa fedha uliosababisha baaadhi ya vyombo vya habari kufungwa.Sababu nyengine inatokana na ile hali kwamba wajasiria mali uwekeza katika vyombo vya habari ili kuweza kuwa na usemi katika kile kinachoandikwa.
                                   CHANZO CHA HABARI NA DW

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate