EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 26, 2013

Askari wanaswa kwa ujambazi.

Wamo pia wafanyabiashara wakidaiwa kushiriki mauaji

JESHI la Polisi katika mikoa ya Iringa na Mbeya, limewakamata watu 29 wakiwemo askari wawili wanaotuhumiwa kuwa majambazi hatari waliohusika na matukio ya mauaji na uporaji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman, aliwaambia waandishi wa habari kuwa miongoni mwa waliokamatwa ni askari Samuel Balumwina (31) mwenye namba MT 85393 kutoka kikosi cha JKT Itende (844KJ) na PC Samuel Kigunye (27) namba G.9101.
Askari hao wanatuhumiwa kuazimisha sare za majeshi hayo kwa majambazi. Na kuongeza kuwa polisi atashtakiwa kijeshi na kuunganishwa na wengine kwa makosa ya mauaji na uporaji wa mali.

Watuhumiwa hao wa ujambazi wanadaiwa kuhusika katika matukio makubwa likiwemo la mauaji ya askari polisi G 68 PC Japhary aliyepigwa risasi ubavuni akiendesha gari la namba PT 0665 lilipokuwa doria Mkwajuni, wilayani Chunya.

Athuman alisema wananchi wa eneo la Mkwajuni wilaya ya Chunya wakiwa na silaha za jadi kwa hasira ya kuuawa kwa askari Japhary, walimshambulia dereva wa gari la majambazi Shaban John (33) ambaye kabla hajafa aliwataja wenzake alioshirikiana nao.
Alisema uporaji huo waliufanya katika kituo cha mafuta cha Matundasi ambapo walipora kiasi cha sh milioni 2.2.

Kamanda Athuman aliwataja watuhumiwa waliomuua PC Japhary kuwa ni Master, Emmanuel Mdendemi, Mashaka Hongole, Manase Kibona, Mashaka George, John Mahenge (39) na Norasco Mabiki(32) ambao licha ya kutuhumiwa kwa mauaji pia wameshiriki katika uporaji kwa kutumia silaha kwa masista eneo la Wanging’ombe, mkoa wa Njombe.

“Mtandao wa watuhumiwa hawa ni wa hatari sana na unaungana na wale kutoka mikoa ya Iringa na Dar es Salaam,” alisema na kuongeza kuwa watu hao pia wanatuhumiwa kuteka na kuwaua Festo Afwilile Kyando (45) mmiliki wa gari lenye namba T586 AGX aina ya Mitsubishi Fuso na utingo wake, Jamali Msangu (26) na miili yao kutupwa porini Februari 2, mwaka huu.

Alitaja watuhumiwa waliowateka, kuwaua na kisha kupora mali kuwa ni Rajabu Mbilinyi (25) mkazi wa jijini Dar es Salaam, Gregory Charles (25), mkazi wa Sabasaba Mbeya na Ghati Mbilinyi (32) mkazi wa Mwanjelwa ambaye inadaiwa gari lake lenye namba za usajili T464 BLX aina ya Noah ndilo lililotumika kufanya mauaji na alikuwa akitumia sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na zile za polisi.

Wengine ni Japhet Ng’ang’ana (24) mkazi wa Makambako anayedaiwa kutunza silaha zilizokamatwa na mfanyabiashara wa Makambako na ndugu wawili Hilary Ng’ang’ana (30) na Claud Ng’ang’ana (36) wakazi wa Nyololo, Mafinga wakishirikiana na Francis Sanga (30) mkazi wa Tunduma anayetuhumiwa kupokea mali za wizi baada ya mauaji ya Mafinga.
Silaha zilizokamatwa zikidaiwa kutumika katika matukio ya ujambazi ni bunduki aina ya shortgun iliyofutwa namba, gobore moja lililokamatwa kwenye gari la Gathi Mbilinyi T464 BLX Noah na bastola tatu zilizotengenezwa kienyeji zinazotumia risasi za shortgun zilikamatwa Makambako na Mbeya kwa Hilary.
Polisi pia imekamata risasi 155 zikiwemo 31 za SMG/SAR na 99 za short gun na 25 za bastola, magari matano na sare za majeshi zinazotumiwa kwenye vitendo vya ujambazi.
Kamanda Athuman alisema majambazi tisa waliohusika na mauaji ya Mafinga watasafirishwa chini ya ulinzi mkali kwenda mkoani humo ili kufikishwa mahakamani.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate