EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 5, 2013

Atuhumiwa kuua mfanyakazi kwa moto

POLISI Mkoa wa Kinondoni wanamshikilia mwanamke (jina tunalo) kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mlinzi wake aliyejulikana kwa jina la Isaac Banda baada ya kumchoma moto hadi kufa.

Mwanamke huyo, ambaye ni Mtanzania mfanyabiashara anayeishi New York, Marekani anadaiwa kufanya uhalifu huo baada ya kurudi nchini Januari 22 na kugundua upotevu wa mali zake zenye thamani ya Dola za Marekani 50,000 karibu Sh80 milioni za Tanzania katika nyumba yake iliyopo Upanga.

Habari zilizopatikana jana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela zinasema kuwa awali Banda ambaye anadaiwa kuwa ni raia wa Malawi alifika katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay na ndugu yake Festo Richard kutoa habari za kujeruhiwa na mwanamke huyo na akapatiwa fomu ya PF 3 kwa ajili ya matibabu.

“Banda na ndugu yake aliyejitambulisha kwa jina la Festo Richard juzi walifika katika Kituo cha Polisi Oysterbay ili kutoa taarifa za kujeruhiwa kwa kupigwa na kuchomwa moto na jalada la kujeruhi lilifunguliwa.Majeruhi huyo alikwenda kutibiwa katika Hospitali ya Mwananyamala.
Kenyela alisema baada ya kufikishwa hospitalini hapo hali ya Banda iliendelea kuwa mbaya na kuhamishiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH), lakini alipoteza maisha muda mfupi baada ya kufika hospitalini hapo.

Kenyela alisema maelezo ya awali yanaeleza kuwa Banda, ambaye alikuwa ameajiriwa kama mtunza nyumba na mlinzi wa nyumba ya mwanamke huyo akiwa kazini kwake Block 41, Kinondoni alishambuliwa na tajiri yake akiwa na watu wengine ambao bado hawajafahamika.

Banda alipigwa huku akiwa amefungwa kamba miguuni na mikononi na kisha kuchomwa moto.

“Saa 11 alfajiri, Januari 22, mlinzi huyo alifanikiwa kujiokoa na kukimbilia nyumbani kwa Festo akiwa na majeraha makubwa ya moto yaliyosababisha kifo chake,”alisema Kenyela.
Alisema hata hivyo haijafahamika mlinzi huyo aliwezaje kufika nyumbani kwa ndugu yake akiwa katika hali hiyo.

Kenyela alisema wakiwa katika upelelezi wa tukio hilo, Februari 2, mtuhumiwa alifika Kituo cha Polisi cha Oysterbay na kutoa taarifa za wizi wa mali zake lakini kabla hajamaliza mchakato huo walipewa taarifa za kifo cha mlinzi huyo kutoka Hospitali ya Muhimbili na yeye kugundulika kuwa ni mhusika hivyo kuwekwa ndani kwa tuhuma hizo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate