EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, February 6, 2013

CUF, Chadema kuandamana

BARAZA la Vijana la Chadema (Bavicha), limesema linaungana na wakazi wa Mkoa wa Mtwara kupinga uamuzi wa serikali kusafirisha gesi kwa njia ya bomba kutoka mkoani humo kwenda Dar es Salaam.

Wakati Chadema wakisema hivyo, Jumuiya ya Vijana ya CUF, imesema itafanya maandamano makubwa kuunga mkono wananchi wa Mtwara kupinga gesi kusafirishwa kwenda Dar es Salaam.

Pia, Bavicha lilisema rasilimali zinazopatikana nchini, zisiposimamiwa ipasavyo zitakuja kugeuka kuwa laana badala ya neema.
Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa Bavicha, John Heche wakati akifungua mkutano wa wenyeviti wa Baraza hilo nchini uliofanyika Dar es Salaam.

Heche alisema hatua ya kusafirisha gesi kwenda Dar es Salaam wakati uwezekano wa kuizalisha mkoani humo ukiwapo, ni kuendelea kuwanyima fursa ya maendeleo wananchi wa Mtwara.

“Vijana wa Bavicha tunaungana na wakazi wa mkoa huo kuhakikisha wananufaika na gesi hiyo, kwani itasaidia kuinua hali ya maendeleo katika mikoa ya Mtwara na Lindi,” alisema Heche na kuongeza:
“Inawezekana viwanda vikajengwa mkoani humo, gesi ikazalishwa na ajira zitapatikana lakini ikipelekwa Dar es Salaam ajira zitapatikanaje huko.”
Hatua ya Heche imetokana na siku chache zilizopita maelfu ya wakazi wa Mtwara kufanya maandamano, wakipinga gesi kupelekwa Dar es Salaam.
Heche aliwataka wenyeviti wa mkutano huo kujadili kwa kina mambo mbalimbali yatakayojenga Baraza hilo.

“Vijana ndiyo msingi wa maendeleo popote duniani, kupitia mkutano huu tunatakiwa kuja na majibu ambayo yatasaidia kukijenga chama,” alisema Heche.
Naye Katibu Mkuu wa Bavicha, Deogratias Munishi alisema kikao hicho kitatoa nafasi ya kuangaliwa uhai wa chama hicho.

Munishi alisema Kamati Kuu ya Chadema imetangaza mwaka huu kuwa wa nguvu ya umma.
Mwenyekiti wa Vijana CUF, Katani Katani alisema wanashangazwa na kauli za viongozi wa Serikali ya CCM kwamba Mtwara wanataka gesi iwanufaishe wao wakati siyo kweli.

“Tunaomba ifahamike wananchi wa Mtwara wanataka uwekezaji unaotokana na gesi ufanywe Mtwara na Lindi kama ilivyokuwa kwenye viwanda vya sukari, miwa inalimwa Turiani, Mtibwa na Kilombero na uwekezaji wote upo maeneo hayo,” alisema Katani na kuongeza:

“Serikali ya CCM inapindisha jambo hilo sasa kwa kuwaunga mkono wananchi wa Mtwara tutafanya maandamano makubwa Dar es Salaam, ili kuhakikisha madai ya wananchi yanafanyiwa kazi siyo kuyapuuzia.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate