EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, February 3, 2013

YANGA 1-1 MTIBWA SUGAR

Young Africans imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya Mtibwa Sugar kutoka Morogoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika  leo jioni katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. 

Katika mchezo wa leo Young Africans  imeshindwa kuondoka na ushindi kutokana na washambuliaji kushindwa kutumia nafasi nyingi za wazi hali iliyopelekea mchezo kuwa mgumu kwa kipindi chote cha mchezo.

Didier Kavumbagu na Jerson Tegete  walikosa nafasi za mabao ya wazi zaidi ya tano katika kipindi cha kwanza, kwani umahiri wa mlinda mlango  Sharrif  Cassilas wa mtibwa uliweza kuwafanya waonekane bora muda wote wa mchezo.
Dakika ya 45, Shaban Kisiga aliipatia Mtibwa Sugar bao la kwanza kwa kichwa akimalizia mpira wa kona uliopigwa na Said Mkopi na mpira huo kumkuta mfungaji akiwa peke yake na kuukwamisha mpira kwa kichwa.


Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans 0 - 1 Mtibwa Sugar.
Kipindi cha pili kilianza kwa Young Africans kufanya mbadiliko ambapo Said Bahunuzi, Hamis Kiiza na Nurdin Bakari waliingia kuchukua nafasi za Frank Domayo, Didier Kavumbagu na Athumani Idd.

Mbadiliko hayo yaliongeza uwezo wa kumiliki mpira kwa timu ya Young Africans kwani eneo la kiungo walilitawala vizuri hali iliyoplelekea kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Mtibwa Sugar lakini umakini wa washambuliaji bado ulikua ni tatizo.
Hamis Kiiza aliipatia Young Africans bao la kusawazisha dakika ya 86 akimaliza shuti kali lilopigwa na Said Bahanuzi kutoka upande wa kulia na kumkuta Kiiza aliyeukwamisha mpira huo wavuni na kuwa bao la kusawazisha.

Young Africans ilikosa tena mabao ya wazi dakika za lala salama kupitia kwa washambuliaji wake Tegete, Msuva, Kiiza na Bahanuzi ambao walikosa mabao hayo hali iliyopelekea wapenzi na wanachama wa Young Africans kukosa raha kutokana na nafasi hizo.
Mpaka mwisho wa mchezo Young Africans 1- 1 Mtibwa Sugar.

Kocha Mkuu wa Young Africans  Ernest Brandts amesema kikosi chake hakikucheza vizuri katika mchezo wa leo, wachezaji walipata nafasi nyingi za wazi lakini hawakuwa makini hali hiyo ndio iliyopelekea mchezo kuisha sare ya mabao 1-1.

Young Africans: 1.Ally Mustafa 'Barthez', 2.Mbuyu Twite, 3.Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani, 6.Athumani Idd/Nurdin Bakari, 7.Saimon Msuva, 8.Frank Domayo/Said Bahanunzi, 9.Didier Kavumbagu/Hamis Kiiza, 10.Jerson Tegete, 11.Haruna Niyonzima

Mtibwa Sugar: 1.Hussein Sharrif, 2.Said Mkopi,3.Issa Rashid, 4.Rajab Mihamed, 5.Salum Sued, 6.Shaban Nditi, 7.Vicent Barnabas, 8.Rashid Gumbo, 9.Hussein Javu, 10.Shaban Kisiga, 11.Ally Mohamed

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate