Wimbo la utapeli limevamia kwa kasi ya ajabu katika mkoa wa Iringa
baada ya wananchi kutapeliwa kupitia ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo na Mkuu wa Mkoa wa
Iringa Dk Christine Ishengoma.
Matapeli hao wamekuwa wakiwapigia watu mbalimbali simu na kuwataarifu kuwa katika Ofisi hizo za viongozi wa Manispaa ya Iringa kuna pikipiki zimetolewa na Rais Jakaya kikwete kwa ajili ya maofisa ugani na kuwa wao wamebahatika kuzipata mbili hivyo wameamua kuziuza kwa bei ya Shilingi milioni 2.5 na kama mteja anahitaji afike ofisini hapo kulipa pesa hiyo ili apewe pikipiki na hati yake.
Inadaiwa kuwa baada ya wateja kufika
hapo, wamekuwa wakiambiwa watoe pesa hiyo nje ya Ofisi kisha
wakatafute usafiri wa kubeba pikipiki hizo. Hapo ndipo wanapokuwa
wametapeliwa na matapeli hao kutoweka. Waliotapeliwa wanaporudi ndipo
hukumbwa na mshangao.Matapeli hao wamekuwa wakiwapigia watu mbalimbali simu na kuwataarifu kuwa katika Ofisi hizo za viongozi wa Manispaa ya Iringa kuna pikipiki zimetolewa na Rais Jakaya kikwete kwa ajili ya maofisa ugani na kuwa wao wamebahatika kuzipata mbili hivyo wameamua kuziuza kwa bei ya Shilingi milioni 2.5 na kama mteja anahitaji afike ofisini hapo kulipa pesa hiyo ili apewe pikipiki na hati yake.
Matukio hayo yametokea kwa nyakati tofauti katika uzio wa Ofisi za Manispaa ya Iringa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambapo watu watatu wametapeliwa.
Kijana mmoja wa Kiwere alitapeliwa zaidi ya Shilingi laki mbili za mauzo ya nyanya kwa matapeli hao kujifanya ni maofisa wa polisi wanaofanya msako wa fedha za mzungu zilizoibwa jana, hivyo wanakagua fedha za kila mwananchi na hivyo kutaka fedha za mkulima huyo ili kuchunguzwa. Mtu huyo aliambiwa asubiri nje ya ofisi za Manispaa ya Iringa na hali akifanya hivyo, matapeli hao walitokea mlango wa pili na kukimbia.
No comments:
Post a Comment