EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, April 20, 2013

Vigezo 5 muhimu vya mwanamke anayefaa kuwa mke thabiti.

Katika harakati za kusaka wenzi wa maisha, vijana wengi wamekuwa wakibabaika juu ya sifa za mwenzi ambaye anaweza kuwa sahihi katika maisha yake. Hili limekuwa tatizo sugu sana kwa vijana wengi!

Lakini vijana wa sasa huhadaika zaidi na mvuto wa sura na maumbile ya mtu wakifanya kama kipimo kikuu cha anayefaa kuwa mwenzi wa maisha, jambo ambalo ni makosa makubwa sana. Mvuto si kipimo cha mwenzi anayefaa kuingia kwenye ndoa.

Kudanganyika na uzuri wa nje pekee siyo kati ya sifa muhimu zaidi za kumfanya awe na vigezo vya kuwa mwenzi wako wa maisha. Zamani, wazee wetu walikuwa wanatizama kwanza heshima na uchapakazi kama vipimo vya awali kabisa vya kumpa sifa mwanamke kuolewa.

Siku hizi ni kunyume chake! Lakini inashauriwa kuwa makini sana na uchaguzi wako wa mke/mume kwani kufanya maamuzi yasiyo sahihi ni sawa na kujirudisha mwenyewe nyuma. Kuwa na msimamo, fanya uchaguzi ulio sahihi, ambao hautakufanya baadaye ujutie!

Ndoa ni agano, hivyo ni vyema ukawa umejihakikishia kwamba hujafanya makosa kabisa katika uchaguzi wako. Vipo vigezo muhimu zaidi, ambavyo unatakiwa kuviangalia kwa mwanamke ambaye unataka awe mkeo. Hebu tuanze kuviona.

JIULIZE, UNAMPENDA?
Kitu cha kwanza kabisa ambacho unatakiwa kuhakikisha unakifikiria ni juu ya mapenzi yako kwake! Sema na moyo wako ukupe ukweli juu ya hilo, usikurupukie mapenzi, usije ukamuona msichana siku moja amevaa suruali inambana kiasi cha kuonyesha umbile lake halafu ukamtamani ukadhani unampenda, utakuwa unapotoka!

Mapenzi ya kweli huanzia moyoni, jiridhishe kwanza ndipo ukubali kumwingiza katika moyo wako. Kumbuka kuwa unapoamua kufunga ndoa na mtu ni ahadi ambayo mmeahidiana mbinguni na duniani, ni ahadi ambayo inapaswa kutenganishwa na kifo tu, sio vinginevyo!

CHUNGUZA, ANAKUPENDA?
Jambo la pili ambalo unatakiwa kuliangalia ni kuhusu mapenzi yake ya kweli kwako. Wataalam wa Mambo ya Mapenzi wanasema, ingawa ni vizuri kuishi na mtu unayempenda lakini pia ni lazima awe anakupenda! Siyo vigumu sana kumfahamu mwenzi anayekupenda, lakini pia inawezekana ukaona anakupenda kumbe ni danganya toto!
Kimsingi katika hili ni lazima utumie akili yako yote uweze kutambua hilo. Katika makala zangu zilizopita nilianisha sifa za mpenzi mwenye mapenzi ya dhati, lakini kwa kuongezea ni kwamba, anayekupenda huwa mvumilivu, anayekusikiliza pia mwenye kuwajali ndugu, marafiki na jamaa zako, anayekuheshimu na kutambua thamani yako.

Mwanamke anatakiwa kujitoa kwako kikwelikweli na hapo ndipo utakapoingia kwenye ndoa yenye amani na furaha. Mwanamke anayetakiwa kuwa na wewe katika maisha ya ndoa ni lazima moyo wake uwe umejiachia kwako sawasawa.

ANA SIFA ULIZOTARAJIA?
Linaweza kuwa swali tata kwako, lakini kamwe lisikuchanganye akili yako, hapa unatakiwa kujiuliza juu ya uliyotarajia kwake, ni kweli unayapata yote? Hapa kuna vipengele viwili ndani ya hiki kimoja. Kwanza kabla ya uhusiano na pili, ndani ya uhusiano.

Nikianza na kabla ya uhusiano, hapa namaanisha kwamba, ana sifa zote ambazo ulikuwa unatarajia kwa mpenzi wako ajaye, ambaye ndiye huyo unayetarajia kuingia katika uhusiano naye. Ni kweli ana kila kitu kinachokuvutia kiasi kwamba hutathubutu kumsaliti?

Ukishajiridhisha na hilo, unaweza kuingia katika uhusiano lakini siyo kwa kasi kubwa, hapa namaanisha kwamba, unaingia katika kipindi cha urafiki ambacho huweki kila kitu wazi, hivyo katika kipindi hiki utaweza kujua kama unapata kile ulichotarajia.

Chunguza tabia zake kwa makini katika kipindi hiki, toka naye katika matembezi ya pamoja, huku ukiwa umemweka katika kipimo ambacho hata yeye mwenyewe atakuwa hafahamu. Lazima mwisho wa siku utaweza kugundua kwamba, chaguo lako lilikuwa sahihi au lah.

ANAJALI?
Hata kama ni mzuri kiasi gani, ana mvuto kiasi gani, anakubalika na marafiki zako kiasi gani, lakini vyote hivyo vinaweza kupoteza maana kama hataonyesha anavyojali thamani yako wewe kama mpenzi wake.

Ninapozungumzia kujali, nakuwa nimekwenda mbali zaidi, anavyojali familia yako, marafiki zako na hata wewe mwenyewe. Hutakiwi kuwa na mwanamke ambaye akili yake haiwazi chochote juu ya maisha. Mwanamke anapaswa kuwa makini, akili ziwe zinafanya kazi sawasawa na awe na mchango mkubwa wa mawazo kwenye familia.

MNYENYEKEVU
Sifa ya mvuto wake, inaweza kuharibiwa na kukosa uchangamfu na unyenyevu. Mwanamke hata kama ni mzuri kwa kiwango gani, akipoteza sifa hizi, uzuri wake ni kama unakuwa umepungua. Uchangamfu huu uanzie kwako, asiwe mwanamke mkimya kupitiliza, hali ambayo inaweza kutafsiriwa kwamba anaringa.

Lakini pia, uchangamfu huu anatakiwa auonyeshe hata kwa rafiki zako pamoja na ndugu zako. Mwanamke mwema ni yule mwenye unyenyekevu kwa mumewe pamoja na ndugu zake.

...Umenipata?
Uzuri wa mwanamke hauna maana ya ubora wa kuwa mke, siyo kila mwanamke anaweza kuwa mke! Mchunguze kwa makini sana mwenzi wako, hakikisha ana sifa nilizozitaja na zingine muhimu zaidi, lakini kubwa kuliko yote, mwanamke huyo lazima awe anakupenda kwa mapenzi ya dhati.

Kama hakupendi mtawezaje kuishi katika ndoa? Naweka kituo kikubwa hapa, nikiwataka tukutane wiki ijayo kwa mada nyingine nzuri zaidi. Nawatakieni week-end njema marafiki zangu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate