Parokia mpya ya Mt. Joseph
iliyopo Olasiti jinni Arusha.
Parokia mpya ya Mt. Joseph
iliyopo Olasiti jinni Arusha imekumbwa na tukio kubwa ambalo si la
kawaida kutokea katika makanisa,misikitini, na hata kuzoea hali hii katika
maisha ya kawaida ya watanzania,
Tukio hilo lililotokea majira saa nne na dk kadhaa baada ya
maandamano yaliyoanzia nje ya eneo la kanisa
yakielekea kanisani.
Baada ya kuingia eneo la kanisa kwa nje kabla ya kuingia
ndani ya kanisa, ndipo palipotokea mlipuko wa bomu wakati baba Askofu Francis Pandilla na balozi wa
papa kutoka Vatican wakijiandaa kubariki maji ya Baraka ili wabariki waamini na
kubariki kanisa hilo jipya kabla ya kuingia ndani ya kanisa na kuanza misa
takatifu.
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akiwa eneo la tukio.
Huku waumini wa kanisa katoliki nchini wakiwa makini kusikiliza Redio
Maria ambayo ndio iliyokuwa inarusha matangazo
ya moja kwa moja kutoka kanisani
hapo ilikatisha matangazo ya kawaida na
kuanza kutangaza tukio hilo live.
Huku watu wakiwa
wemeshikwa na butwaa na kutojua maamuzi
ya haraka ya kufanya huku watoto wa maua hujulikana kama
utoto wa yesu wanaotanguliwa
mbele kupamba sherehe za wakatoliki pamoja na vijana ndio waliokuwa waathirika
zaidi wa tukio hilo.
Mwandishi wetu alie
kuwa eneo la tukio alishudia watu wakikimbia huku na huku kuokoa nafsi yake.
Mwandishi pia alishuhudia baadhi ya viongozi wa serikali
waliopatwa na msituko. baada ya kupata taarifa ya mlipuko huo.
Mkuu
wa mkoa wa Arusha akiwa njiani kuelekea eneo la tukio alikumbana na
vikwazo njiani kutokana na wingi wa magari kuelekea eneo la tukio.
Viongozi hao akiwemo mkuu wa mkoa wa Arusha Mh. Magesa Mulongo , Mh.Godbless Lema
mbunge wa jimbo la Arusha mjini,
chadema Mh. Joshua Nassari mbunge wa
jimbo la Arumeru.
Mkuu wa wilaya ya
Arusha mjini Alitibua hali ya hewa pale pale alipowaambia waumini pamoja na viongozi wa kanisa wa eneo la tukio
kwa kusema. Tukio hili ni la kawaida:
waumini walionekana kuipokea kwa mtazamo
tofauti kauli hiyo na kusababisha
minong’ono ya hapa na pale kwa watu kutofarijika kwa maneno yake.
Mwandishi wetu aliondoka eneo la tukio na kuelekea Hosp ya
ST ELIZABETH walikolazwa baadhi ya majeruhi , na kushuhudia baadhi ya majeruhi wakiendelea
kupata huduma.
Mwandishi wa 2jiachie akimpa pole mgonjwa.Alietoa baadhi ya maelezo hapo chini kwenye nukuu
Tuliongea na na
moja kati ya majeruhi hao ambae alikuwa
mbele kabisa na lilipotua bomu alisema yafuatayo:
“ wakati
tumesimama tuu wakianza kubariki maji, mimi nikaona kama jiwe
limerushwa nikainama lisinipige wakati naendelea kuwauliza wenzangu mbona
wanarusha mawe ghafla mlipuko, kumbe halikuwa jiwe ndio bomu lenyewe”
Pia mwandishi baada ya kutoka hapo alielekea hospital ya Maunt
Meru Ila hakupata nafasi ya
kuingia wodini kutokana wa kuzuiliwa kwa
kutoa nafasi ya madaktari kutoa huduma ya haraka kwa majeruhi. Pamoja na
kuongezewa damu majeruhi.
Mbunge wa Arusha mjini
Mh. Godbless Lema Pia alijitolea
Damu kwa kuwasaidia majeruhi.
moja kati ya kijana aliekuwa kwenye maandamano na kukutana na mlipuko. kama anavyoenekana amechafuka damu.
Hapa wana habari wa ITV wakiwa hewani eneo la tukio katika kanisa la Mt.Joseph Olasiti-Arusha.
Majeruhi waliolazwa katika hospitali ya ST. ELIZABETH ARUSHA.
Gari ya Mbunge wa
Arusha mjini Godbless Lema likiwa mbele ya eneo la hospitali ya Mount
meru Arusha. Godbless Lema amejitolea damu siku ya leo kuwasadia majeruhi wa
mlipuko wa bomu
Viongozi
wa vijana wakatoliki jimbo la Arusha mjini wakiwa hospitali ya Mount
Meru wakiwa tayari kuwafariji majeruhi kulia ni Sister mlezi wa vijana
jimbo,John Masawe mwenyekiti jimbo na kulia ni Majegero Selecius mwana mipango wa kanda.
Habari na 2JIACHIE- www.2jiachie.com
No comments:
Post a Comment