EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, May 5, 2013

BOMU LAKATISHA UZINDUZI WA KANISA LA MT. JOSEPH – OLASITI ARUSHA.

Habari na 2JIACHIE-  www.2jiachie.com

 
                                 Parokia mpya ya Mt. Joseph  iliyopo Olasiti jinni Arusha.
Parokia mpya ya Mt. Joseph  iliyopo Olasiti jinni Arusha imekumbwa na tukio kubwa ambalo si la kawaida kutokea katika makanisa,misikitini, na hata kuzoea hali hii katika maisha ya kawaida ya watanzania,
Tukio hilo lililotokea majira saa nne na dk kadhaa baada ya maandamano yaliyoanzia nje ya eneo la kanisa  yakielekea kanisani.
Baada ya kuingia eneo la kanisa kwa nje kabla ya kuingia ndani ya kanisa,  ndipo  palipotokea mlipuko wa bomu wakati  baba Askofu Francis Pandilla na balozi wa papa kutoka Vatican wakijiandaa kubariki maji ya Baraka ili wabariki waamini na kubariki kanisa hilo jipya kabla ya kuingia ndani ya kanisa na kuanza misa takatifu.
 
                                 Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akiwa eneo la tukio.
Huku waumini wa kanisa katoliki  nchini wakiwa makini kusikiliza Redio Maria  ambayo ndio iliyokuwa inarusha matangazo ya moja kwa moja  kutoka kanisani hapo  ilikatisha matangazo ya kawaida na kuanza kutangaza  tukio hilo live.
  
Huku watu wakiwa wemeshikwa na butwaa na kutojua maamuzi  ya haraka ya kufanya huku watoto wa maua hujulikana  kama  utoto wa yesu  wanaotanguliwa mbele  kupamba sherehe za wakatoliki  pamoja na vijana ndio waliokuwa waathirika zaidi wa tukio hilo.
Mwandishi  wetu alie kuwa eneo la tukio alishudia watu wakikimbia huku na huku kuokoa nafsi yake.
Mwandishi pia alishuhudia baadhi ya viongozi wa serikali waliopatwa na msituko. baada ya kupata taarifa ya mlipuko huo.
Mkuu wa mkoa wa Arusha akiwa njiani kuelekea eneo la tukio alikumbana na vikwazo njiani kutokana na wingi wa magari kuelekea eneo la tukio.
Viongozi hao akiwemo mkuu wa mkoa wa Arusha  Mh. Magesa Mulongo , Mh.Godbless Lema mbunge  wa jimbo la Arusha mjini, chadema  Mh. Joshua Nassari mbunge wa jimbo la Arumeru.
Mkuu wa wilaya  ya Arusha mjini Alitibua hali ya hewa pale pale alipowaambia waumini  pamoja na viongozi wa kanisa wa eneo la tukio kwa kusema. Tukio hili ni  la kawaida: waumini walionekana kuipokea  kwa mtazamo tofauti  kauli hiyo na kusababisha minong’ono ya hapa na pale kwa watu kutofarijika kwa maneno yake.
Mwandishi wetu aliondoka eneo la tukio na kuelekea Hosp ya ST ELIZABETH walikolazwa baadhi ya majeruhi , na kushuhudia baadhi ya majeruhi  wakiendelea  kupata huduma. 

Mwandishi wa 2jiachie akimpa pole mgonjwa.Alietoa baadhi ya maelezo hapo chini kwenye nukuu
Tuliongea na  na moja kati ya majeruhi hao  ambae alikuwa mbele kabisa na lilipotua bomu alisema yafuatayo:
  “ wakati tumesimama  tuu wakianza  kubariki maji, mimi nikaona kama jiwe limerushwa nikainama lisinipige wakati naendelea kuwauliza wenzangu mbona wanarusha mawe ghafla mlipuko, kumbe halikuwa jiwe ndio bomu lenyewe”
Pia mwandishi baada ya kutoka hapo alielekea hospital  ya Maunt  Meru  Ila hakupata nafasi ya kuingia  wodini kutokana wa kuzuiliwa kwa kutoa nafasi ya madaktari kutoa huduma ya haraka kwa majeruhi. Pamoja na kuongezewa damu majeruhi.
Mbunge wa Arusha mjini  Mh. Godbless Lema  Pia alijitolea Damu kwa kuwasaidia majeruhi.

moja kati ya kijana aliekuwa kwenye maandamano na kukutana na mlipuko. kama anavyoenekana amechafuka damu.
Hapa wana habari wa ITV wakiwa hewani eneo la tukio katika kanisa la Mt.Joseph Olasiti-Arusha.

Majeruhi waliolazwa katika hospitali ya ST. ELIZABETH  ARUSHA.
Gari ya Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema likiwa mbele ya eneo la hospitali ya Mount meru Arusha. Godbless Lema amejitolea damu siku ya leo kuwasadia majeruhi wa mlipuko wa bomu
 
Viongozi wa vijana wakatoliki jimbo la Arusha mjini wakiwa hospitali ya Mount Meru wakiwa tayari kuwafariji majeruhi kulia ni Sister mlezi wa vijana jimbo,John Masawe mwenyekiti jimbo na kulia ni Majegero Selecius mwana mipango wa kanda.



Habari na 2JIACHIE-  www.2jiachie.com

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate