
Kwa mujibu wa Mwana FA mwenyewe
ambaye jana ameachia wimbo wake mpya, Kama Zamani, hivi karibuni alipokea
malipo ya miezi mitatu kutoka kampuni moja ya kuuza miito ya simu aka
RBT yanayofikia shilingi za kitanzania milioni 18.
Akiongea leo kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, FA aliyekuwa wa
tatu kati ya wasanii waliopata fedha nyingi zaidi kwenye malipo hayo
chini ya Rose Mhando na Diamond, amesema ameamua kuweka wazi hilo ili
watu waondoe imani kuwa muziki wa hip hop hauuzi.
Tarehe 31 mwezi huu, Mwana FA ambaye jina lake halisi ni Hamis Mwinjuma atakuwa na show yake aliyoipa jina.
No comments:
Post a Comment