EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, May 28, 2013

NAMBA YA FREEMASON YAZUA HOFU KATIKA JAMII.

 
Na Makongoro Oging'
HOFU imezuka nchini baada ya namba ya simu inayotajwa kuwa ni ya jamii ya watu wasiomwamini Mungu, Freemason kuhusishwa na umwagaji damu na kafara kutumika kuwapigia watu mbalimbali, Uwazi lina taarifa hii kwa ukamilifu.

Taarifa ambazo Uwazi limezipata, zinaeleza kwamba namba hiyo ni ya Freemason na kwamba, mpigiwaji akijaribu kupokea na kuzungumza, atakuwa ameunganishwa kwenye kafara hiyo.
Baada ya namba hiyo ya kutatanisha kuzuka na kuwapigia watu mbalimbali, inaelezwa kwamba iligundulika kuwa ni ya jamii hiyo na hivyo kusambazwa meseji ya kuwaonya watu wasipokee simu hiyo.
 
NI NAMBA GANI?
Namba hiyo ni 0800226655 ambayo Uwazi limejiridhisha kuwa si namba ya mtandao wowote wa simu nchini wala nje ya mipaka ya Tanzania, maana hakuna namba kama hiyo.
Ukiachilia mbali kujichanganya kwake, kwa kawaida namba za nje ya nchi huja na alama ya jumlisha, ikifuatiwa na namba za utangulizi za nchi husika, tofauti na namba hiyo.
ONYO LATOLEWA
Kutokana na hofu hiyo, watu wengi wanasambaza ujumbe wa onyo wa kuwataka watu wasijaribu kupokea namba hiyo kabisa ili wasijiunganishe na kafara hiyo.
Uwazi limeambiwa kwamba, ujumbe huo umeanzia makanisani baada ya wachungaji kuwataka waumini wao wasipokee namba hiyo ya kishetani.
Ujumbe wenyewe unasomeka: “Naomba uwe makini kupokea simu. Usipokee endapo utaona namba usiyoijua hasa hii 0800226655 kuanzia leo yaani siku uliyopata ujumbe huu hadi Agosti 17, mwaka huu kwani Freemason wanatoa kafara kwa kusikia sauti tu endapo utapokea simu yao. Siyo utani, tafadhali wajulishe na  wengine uwapendao.”
Uwazi na lenyewe limepata kutumiwa ujumbe huo.
 
VINGOZI WA DINI
Baada ya yote hayo, mwandishi wa habari hizi aliwatafuta viongozi mbalimbali wa dini akitaka kusikia maoni yao ambapo walitoa ushirikiano wa kutosha.
Sheikh Jumaa wa Dar es Salaam (ameomba msikiti wake usitajwe) alikuwa na haya ya kusema: “Nimesikia kuhusu huo ujumbe na sisi kama viongozi tumewakataza waumini wetu si tu wasipokee hiyo namba bali waache kabisa kupokea namba wasizozijua.
“Tumesema hivyo kwa sababu hawa jamaa wanaweza kubadilisha na kutumia inayofanana na za mitandao ya hapa kwetu Tanzania. Hata hivyo, kubwa zaidi tumewataka kuzingatia zaidi ibada, hiyo ni njia kubwa zaidi ya kukabiliana na madhara hayo.”
 
ASKOFU JOHN SAID
Askofu wa Kanisa la Victoria lililopo Mabibo External, John Said alisema: “Freemason ni dini ya nguvu za giza, wakati Ukristo ni nuru hivyo hawataweza...kwanza wanaogopa namba zetu kwa kuwa wanajua hawana uwezo wa kutudhuru.”
 
NABII FLORA PETER
“Ni namba ambazo ni za mashetani, hazina nguvu kwa wale wanaomwamini Mungu. Kikubwa ni kusimama katika imani. Siku zote Mungu ana nguvu kuliko shetani. Ni vyema watu wakabaki kwenye imani sahihi.”
PAROKO KAGABA
Paroko wa Kanisa Katoliki Tabata, Cyprian Kagaba alisema: “Huo ujumbe haujatumwa kwenye simu yangu lakini hata kama ukitumwa, nitapuuza kwa sababu najua ni mambo ya kibiashara tu. Wenyewe wanajua kama ukiwatumia na wengine watanufaika.”

Credit to GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate