EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, August 7, 2013

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA... PICHA ZA WALIOMEZA ZANASWA


BAADA ya hivi karibuni Taifa la Tanzania kutikiswa na tuhuma nzito ya biashara ya madawa ya kulevya, picha za watu wanaosafirisha bidhaa hiyo haramu kwa njia ya kumeza almaarufu kwa jina la punda, zimenaswa.
Picha hizo zinazopatikana mtandaoni ambazo hazikujulikana mara moja ni za watu kutoka nchi gani, zinaonesha jinsi madawa hayo yanavyoweza kusafirishwa kwa njia ya kuyameza tumboni huku madhara ya kufanya hivyo yakiainishwa.

MADHARA
Madhara makubwa yaliyoanishwa ni vijana wengi kupoteza maisha kwa urahisi wakati wakihitaji utajiri wa haraka.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyoambatanishwa na picha hizo, watu wanaobeba madawa ya kulevya kwa njia hii wako katika hatari kubwa ya kuweza kuharibu utumbo na kusababisha vifo vya ghafla.
Hali hiyo huweza kutokea pindi madawa hayo yatakapokaa kwa muda mrefu tumboni na kupasuka kutokana na kuchelewa kutolewa.
Mfano watolewa
Katika maelezo ya picha hizo, inadaiwa mmoja wa watu waliokuwa wakifanya kazi hiyo ya ‘upunda’ alipasukiwa na madawa hayo tumboni na kujikuta akifariki dunia baada ya kuchelewa kuyatoa.
Mwingine ilidaiwa kuwa, aliumbuliwa na mashine zilizokuwa kwenye uwanja wa ndege (haukutajwa ni wa nchi gani) na ililazimika  kufanyiwa upasuaji kisha madawa hayo kutolewa.

SAFARI ZA NDEGE HUCHANGIA
Kitu kikubwa ambacho kimekuwa kikiwasababishia vifo wabebaji wengi ni kuahirishwa au kucheleweshwa kwa safari zao za ndege zinazosafiri katika mataifa mbalimbali duniani.
Hali hii huweza kutokea wakati wowote kutokana na hali ya hewa kuchafuka au dharura nyinginezo na kuwakuta wabebaji hao wakiwa hawana ujanja wa kuweza kukwepa  vifo.

WAFANYABISHARA, WANASIASA WATAJWA
Katika hili watu wanaotajwa kuwabebesha madawa ya kulevya vijana wa Kitanzania na kuwatuma kuyapeleka katika nchi mbalimbali duniani ni wafanyabishara wakubwa na wanasiasa.
Tuhuma hizi zimekuwepo kwa muda mrefu kwamba vigogo hao huwatumia vijana wa Kitanzania kuhatarisha maisha yao ilhali wao wakitajirika kwa kupata fedha nyingi.
Majina makubwa ya viongozi na watoto wa vigogo yamekuwa yakitajwa kuhusika kwa namna moja ama nyingine na biashara hiyo haramu na wengi hawajitokezi hadharani kukanusha.

PUNDA WAKUBWA NI WASANII
Punda wakubwa ambao wanatumika kwa ajili ya kubeba madawa ya kulevya ni wasanii wa filamu na wale wa muziki ambao mara kwa mara huonekana wakisafiri nchi mbalimbali duniani.
Inadaiwa wasanii hutumika kwa urahisi kufanya biashara hiyo kwa kuwa ni  vigumu kutiliwa shaka pindi wanapokuwa wanapita kwenye viwanja vya ndege huku wakiwa wamemeza madawa hayo.
Aidha, wasanii wanatumika kwenye biashara hiyo kwa kuwa ni watu wa kusafirisafiri sana kwa shughuli zao za kisanii na pia jamii duniani kote inawapenda, hivyo wana uwanja mpana wa kusaidiwa pindi wanapopata matatizo.
Mtego mwingine wa wasanii unaowafanya kuingia katika  biashara hiyo ni wengi wao kutaka kuishi kifahari tofauti na uwezo wao, hivyo hukubali kuwa punda ili kuweza kupata kipato zaidi  ya kile wanachokipata katika  kazi zao.

Masogange na mwenzake wawaumiza vigogo
Huku hali ikiwa ni ya sintofahamu, baadhi ya vigogo wanaodaiwa kuhusika na biashara hiyo hapa Bongo wanaumia vichwa hasa baada ya msanii, Agnes Gerald ‘Masogange’ (pichani) na mwenzake Melisa Edward kukamatwa nchini Afrika Kusini wakihisi wakati wowote wanaweza kuwataja.
Masogange na mwenzake huyo wanaendelea kuhudhuria mahakamani nchini huko na wakizidiwa wanaweza kuwataja watu waliowatuma kwa kuwa ni vigumu kwao kupitisha  madawa hayo Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar bila ya msaada wa vigogo wenye uzoefu wa biashara hiyo.

Iwe fundisho
Picha zinazowaonesha watu waliokufa kwa kumeza ili kusafirisha madawa ya kulevya na kupoteza maisha yao huku wengine wakiathirika kwa kiasi kikubwa, ziwe fundisho kwa vijana wa Kitanzania ambao wamekuwa wakifanya madili hayo na wale wanaotamani kufanya wajue kwamba kujiingiza huko ni kujitafutia vifo.

CHANZO NI GLOBAL PUBLISHERS.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate