EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 29, 2013

Watu 13 wafariki ajalini Kahama.

Kahama.
Watu 13 wamepoteza maisha papohapo akiwamo mtoto mchanga wa miezi saba, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugonga lori la mizigo lililokuwa limeharibika barabarani katika Kijiji cha Ngongwa, wilayani Kahama, Mkoa wa Shinyanga.
 
Ajali hiyo ilitokea juzi saa 2:30 usiku wakati gari aina ya Toyota Hiace lilipoligonga lori.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kihenya Kihenya, alisema Hiace hiyo ilikuwa ikifanya safari zake kutoka mjini Kahama kwenda mji mdogo wa Ushirombo, katika Wilaya ya Bukombe, mkoani Geita.

Kihenya alisema watu 11 akiwamo dereva ambaye pia ni mmiliki wa gari hilo, Ezekiel Werema, walifariki dunia papohapo na wengine wawili walifariki dunia wakiwa katika 
Hospitali ya Wilaya ya Kahama kwa matibabu.

Alisema polisi wanahangaika kutafuta majina ya marehemu na majeruhi, ili ndugu na jamaa zao waweze kutaarifiwa.

Pia, Kihenya aliwashukuru wananchi wa kijiji hicho kwa ushirikiano walioonyeshwa kwa polisi baada ya ajali kutokea na kuongeza kuwa, hadi sasa baadhi ya watu tayari wamejitokeza Hospitali ya Wilaya ya Kahama kutambua maiti.

Kamanda Kihenya alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi, huku akitoa wito kwa madereva kuwa makini wanapoendesha magari hasa nyakati za usiku.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi Hospitali ya Wilaya ya Kahama, Dk Joseph Fwoma alithibitisha kupokea maiti 11 kutoka eneo la ajali na kwamba, majeruhi wawili walifariki dunia wakipatiwa matibabu hospitalini hapo.

Wakati huohuo, Bakari Kiango anaripoti kuwa, polisi Kanda katika Maalum ya Dar es Salaam, wanawashikilia watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kwa tuhuma za kufanya uhalifu wakitumia sare za JWTZ na JKT.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Suleiman Kova alisema watuhumiwa hao walikamatwa usiku wa kuamkia jana katika maeneo ya Temeke.

Alisema kukamatwa kwao kulikuja baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu watu hao kupanga kufanya uhalifu. Hilo ni tukio la nne kutokea ndani ya Agosti mwaka huu.

“Tutakomesha tabia hii ya watu kutumia sare hizi kwani imekuwa ikiwachanganya wananchi ambao wengi wao wakiwaona watuhumiwa hawa wanajua ni askari wa ukweli kumbe ni wahalifu,” alisema Kova.
Alisema walipopekuliwa watuhumiwa walikutwa na bunduki moja aina ya Shortgun ikiwa imekatwa kitako ,maganda matano ya risasi za SMG na bastola moja aina ya Browing ikiwa na risasi tano.
Hali kadhalika mkasi wa kukatia vyuma, kitambulisho cha JWTZz na sare mbili za Kampuni ya Ulinzi ya Ultimate.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate