EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, August 11, 2013

YANGA YATUMA SALAMU AZAM, YAICHAPA SC VILLA 4-1

Kikosi cha Young Africans kilichoanza dhidi ya SC Villa
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans leo imetuma salaam kwa timu ya Azam ambayo watakutana siku ya jumamosi katika mchezo wa Ngao ya Hisani baada ya kuichapa Sports Club Villa ya Uganda  mabao 4-1.

Ikiwa na wachezaji wake wapya Yanga iliingia uwanjani kwa lengo la kuhakikisha inaendeleza wimbi lake la ushindi, ikizingatia ndio timu yenye kikosi bora kabisa kwa sasa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Mshambuliaji aliyerejea Yanga akitokea klabu ya Azam FC, msimu uliopita akichezea Simba SC Mrisho Ngassa aliipatia timu yake bao la kwanza dakika ya saba ya mchezo kwa shuti kali la kimo cha mbuzi lililomshinda mlinda mlango wa SC Villa Elugant Martin akiduwaa asijue la kufanya.

Dakika ya 18 ya mchezo mshambuliaji Ndaula Moses aliipatia SC Villa bao la kusawazisha kwa kichwa kufuatia krosi iliyopigwa na Ronald Muganga kumkuta mfungaji na kuukwamisha mpira wavuni huku walinzi wa Yanga wakitegeana na kumtazama mfungaji.

Nahodha wa timu ya Yanga Nadir Haroub 'Cannavaro' aliipatia timu yake bao la pili kwa mkwaju mkali kufuatia mpira wa adhabu aliosogezewa na Haruna Niyonzima kumshinda mlinda mlango wa SC Villa akiwa amesimama na mpira kujaa wavuni na kuhesabu bao la pili kwa watoto wa Jangwani.


Dakika tatu baaadaye dakika ya 30, mshambuliaji Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao tatu akimalizia mpira uliopigwa na Jerson Tegete kugonga mwamba wa juu na kumkuta Kavumbagu aliyeukwamisha wavuni mpira huo.
Mpaka timu zinakwenda mapumziko, Young Africans 3- 1 SC Villa.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na katika dakika ya 62 ya mchezo kiungo Haruna Niyonzima aliipatia Young Africans bao nne kwa ustadi wa hali ya juu akiitumia vizuri pasi aliyopewa na mshambuliaji Huseein Javu na kuufanya ubao wa matanagazo usomeke 4-1.

Yanga ilifanya mabadiliko amabapo waliingia Rajab Zahir, Hussein Javu, Bakari Masoud, Said Bahanuzi na Oscar Joshua kuchukua nafasi za Kelvin Yondani, David Luhende, Athuman Idd 'Chuji', Jerson Tegete na Haruna Niyonzima.

Hussein Javu nusura aiipatie Young Africans bao la dakika ya 72 ya mchezo baada ya mpira alioupiga kugonga mwamba wa juu kabla ya kuokolewa na walinzi wa SC Villa ya Uganda.
SC Villa ilijaribu kusaka mabao lakinu umakini wa walinzi wa Yanga ulikuwa kikwazo kwao muda wote wa mchezo huku golikipa Ally Mustapha 'Barthez' akikoa mabao mawili ya wazi kutoka kwa mshabuliaji Ronald Muganga.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 4 - 1 SC Villa.
Mara baada ya mchezo wa leo kikosi cha Young Africans kitaendelea na mazoezi kesho asubuhi katika viwanja vya shule ya sekondari Loyola kujiaanda na mchezo wake wa Ngao ya Hisani dhidi ya wana lambalamba timu ya Azam FC mchezo utakaochezwa tarehe 17.08.2013 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam 

Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.David Luhende/Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro' 5.Kelvin Yondani/Rajab Zahir, 6.Athuman Idd 'Chuji/Bakari Masoud, 7.Mrisho Ngassa, 8.Salum Telela, 9.Jerson Tegete/Hussein Javu, 10.Didier kavumbagu, 11.Haruna Niyonzima/Said Bahanuzi

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate