London, England.
Mashabiki wa Arsenal na Manchester United walikuwa wakifuatilia kwa karibu uhamisho wa Mesut Ozil na Marouane Fellaini.
Taarifa iliyokuwa imetawala hadi tunakwenda
mtamboni ni kiungo wa Real Madrid, Mesut Ozil kufanyiwa uchunguzi wa
afya akiwa Ujerumani ili kukamilisha uhamisho wake wa kwenda Arsenal
baada ya kufikia makubaliano binafsi.Gunners walikubali kulipa euro 47 milioni kwa Real Madrid kufanikisha usajili wa kiungo huyo wa timu ya taifa ya Ujerumani.
Kocha Arsene Wenger pia alikuwa akiendeleza jitihada zake za kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Chelsea, Demba Ba pamoja winga Angel Di Maria wa Real kwa gharama ya euro 30 milioni.
Kwa kipindi cha msimu wa likizo na usajili wa wachezaji, Arsenal imeshindwa kuwasajili wachezaji wa kiwango anachokitaka Arsene Wenger kama mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez na Gonzalo Higuain, mchezaji mwingine wa Real Madrid.
Lakini kwa sasa yumkini Ozil anaelekea Uuwanja wa Emirates kufuatia usajili wa Gareth Bale kwa kitita kikubwa cha pauni milioni 85.3.
Kabla ya kujiunga na Real Ozil alikuwa akichezea klabu ya Werder Bremen alikosajiliwa na Real kwa takribani pauni 12.4 milioni na kuichezea Real mara 155.
Pia, Manchester United walikuwa tayari kulipa
pauni 30.5 milioni kwa ajili ya kiungo wa Athletic Bilbao, Ander
Herrera, kwa mujibu wa Sky Sports.
Manchester United pia walikubali kutoa pauni 24 milioni kwa ajili ya kiungo wa Everton, Marouane Fellaini.
Hadi jana mchana Liverpool ilikuwa klabu ya England iliyofanya usajili mkubwa zaidi katika siku ya mwisho ya usajili.
Kocha Brendan Rodgers ameongeza wachezaji watatu
Anfield, beki Mamadou Sakho, Victor Moses akitokea Chelsea kwa mkopo na
beki wa kati Tiago Ilori kutoka Sporting Lisbon.
Wakati huohuo; Barcelona bado inatafuta beki wa kati, ambapo
kocha Tata Martino anaendelea kujaribu kumshawishi beki wa Chelsea,
David Luiz kwa gharama ya euro 25 milioni.
Hata hivyo Chelsea wenyewe wanataka Euro 40 milioni ili kumwachia Luiz.
Mbali ya Mbrazil huyo nyota mwingine wa Chelsea, Juan Mata aliivutia PSG waliokuwa tayari kutoa fedha.
Uhamisho
England
Tiago Ilori (Sporting Lisbon – Liverpool)
Mamadou Sakho (PSG – Liverpool)
Victor Moses (Chelsea - Liverpool)
Morgan Amalfitano (Marseille – West Brom)
Marko Arnautovic (Werder Bremen – Stoke)
Jack Hunt (Huddersfield - Crystal Palace)
Massimo Luongo (Tottenham - Swindon)
Francisco Junior (Everton - Vitesse Arnhem)
Abdul Razak (Manchester City - Anzhi Makachkala)
Harry Bunn (Manchester City - Sheffield United)
Italia
Kaka (Real Madrid - AC Milan)
Luca Marrone (Juventus – Sassuolo)
Hispania
Denis Cheryshev (Real Madrid - Sevilla)
Lisandro Lopez (Benfica – Getafe)
Ufaransa
Emmanuel Mayuka (Southampton - Sochaux)

No comments:
Post a Comment