EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, September 2, 2013

MAKOSA 10 WANAWAKE HUYAFANYA WAKIWA FARAGHA.

Kitanda kina kanuni zake. Kuna makosa mengi hufanywa na wanawake, vilevile yapo ambayo wanaume huyafanya. Si sawa kuyaacha yaendelee kuwepo kwa sababu faragha ni hatua muhimu katika ukamilishaji wa kitu kinachoitwa penzi.

Uhusiano wa kimapenzi una wigo mpana. Kuna mambo mengi ambayo yakifanywa huufanya mwili uwe na afya. Hata hivyo, suala la faragha halipaswi kusahaulika, kwa maana ni chachandu madhubuti.
Tendo la faragha lina nguvu sana katika kuuweka hai uhusiano. Wapo watu ambao picha zilikuwa haziendi katika maisha ya kawaida lakini kila wakikutana kitandani, kila mmoja alimvulia kofia mwenzake.

Hii ina maana kuwa inawezekana mwenzi wako akawa dhaifu katika maeneo mengine lakini ‘maujuzi’ yake faragha, yakakufanya uwe mtulivu kwake.

Vivyo hivyo, nawe hakikisha unampatia mwezi wako katika eneo fulani ili hata akikufanyia visa, basi uwe na ukurasa wako ambao akiufikia ni lazima akuvulie kofia. Faragha ni uwanja huru ambao ambao hudhaniwa ni mgumu lakini ni rahisi sana.

Haihitaji msuli mkubwa wala nguvu kama za samba. Usidanganyike kwenda kutumia madawa ya kuongeza nguvu wala kwenda kwa waganga eti ndiyo wakuboreshee mvuto wako. Tuliza kichwa, soma kitendo chenyewe halafu hakikisha hufanyi makosa.

Katika makosa mengi ambayo wanawake huyafanya wakiwa faragha, ndani ya mada hii, nimeyaunganisha na kuyafanya yasomeke 10. Nikuhakikishie kuwa ukiyaepuka na kufuata mwongozo sahihi, utakuwa bora sana.

Mambo mengi hayahitaji taaluma, ni suala la kuushirikisha ubongo ili uamue kinachotakiwa. Mathalan; kuzungumza na mwenzi wako kumuuliza nini umfanyie ili afurahie tendo au kumwelewesha cha kufanya aweze kukupatia, haihitaji maarifa mengi au uwezo wa juu kiakili.
 
Kujifanya unajua sana husababisha wengi kuchemka. Achana na tabia ya kuhisi wewe umekamilika na kujidanganya kwamba unafahamu kila kinachotakiwa katika uwanja mahsusi wa faragha. Inakugharimu kiasi gani kuzungumza naye ili akujuze mahali hisia zake zilipolalia?
 
Yupo mwanamke ambaye tangu anazaliwa mpaka anakua, amekariri kwamba ukiwa faragha dawa ni kuzungusha ‘bakuli’ mwanzo mwisho. Matokeo yake, anakutana na mwenzi wake, badala ya kusoma mahitaji yake, yeye akili, nguvu na ujuzi wake wote anauelekeza katika nyonga tu. Mauno mtindo mmoja.
 
Hajui kwamba pengine mwenzi wake hapendi purukushani za kupanda na kushuka. Inapotokea wewe ni mtaalamu wa kucheza juu ya msumari (wana wa unyago mnaelewa), dakika 90 hushushi mzigo chini, ukidhani unamfurahisha, kumbe unageuka kero kwa mwezio.
 
Inaweza kutokea umekariri kuwa ukiwa katika utekelezaji wa sanaa ya faragha lazima uporomoshe mayowe. Japo ni nzuri katika kupata mrejesho (feedback) wa tendo lenyewe lakini si ajabu mwenzako hafurahii hilo. Zungumza naye tafadhali.
 
Hekima za tendo zinakataa ububu, lazima muwe mnaambiana mara kwa mara. Kama siku hajakutendea haki, mweleze waziwazi kwamba hajakufikisha. Ukimwacha afanye anachotaka na anachojisikia yeye, mwishowe haitakuwa na msisimko kwako.
 
Tengeneza utofauti wa makutano ya mbuzi na binadamu. Maana beberu huwa hajui maana ya kumwandaa jike. Anapojisikia kupanda anafanya hivyo na anapotosheka anashuka. Wewe na mwenzi wako hamna budi kuwa na nidhamu. Hisia ziheshimiwe.
 
Ikiwa mtatenda kwa makubaliano, kila mmoja akifuata maelekezo ya mwenzi wake, akitilia mkazo yale maeneo ambayo yametajwa katika mazungumzo kwamba ndiyo huleta raha, basi raha huwa raha kweli. Zingatia mambo 10 yafuatayo;
Itaendelea wiki ijayo.

1 comment:

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate