EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, November 17, 2013

SERIKALI YAWATAKA WAFANYABIASHARA, WAWEKEZAJI KUFUATA SHERIA ZA NCHI‏

IMG_4434
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko Maria Bilia akizungumza na waandishi wa habari kuhusu siku ya Viwanda Afrika ambapo alielezea mafanikio na changamoto katika sekta ya viwanda nchini na Afrika kwa ujumla. Kulia ni Afisa mipango wa Taifa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) Bw. Gerald Runyoro.
IMG_4451
Afisa Mipango wa Taifa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) Bw. Gerald Runyoro akizungumzia ushiriki wa shirika hilo katika kukuza viwanda nchini.
IMG_4459
Kaimu Mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda Nchini (CTI) Dr. Samwel Nyantahe akizungumzia umuhimu wa kuongeza thamani za bidhaa zinazozalishwa hapa nchini kwa minajiri ya kupambana na tatizo la ajira.
IMG_4483
Mkurugenzi wa Viwanda vidogo vidogo kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko Dakta. Consolatha Ishebadi (katikati) akifafanua changamoto wanazokutana nazo wafanyabiashara wazawa katika kutengeneza vifungashio vyenye ubora (Packaging) kwenye bidhaa zao.

IMG_4478
Mwandishi kutoka gazeti la The Citizen akiuliza swali wakati wa mkutano huo wa siku ya Viwanda Afrika.
IMG_4440
Sehemu ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali waliohudhuria mkutano huo.
Na Damas Makangale, Moblog
SERIKALI imesema haitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria wafanyabiashara wote kutoka nje wanaofanya biashara au kufungua viwanda vidogo vidogo bila kufuata taratibu, kanuni na sheria za nchi. Moblog inaripoti.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika kuadhimisha Siku ya Viwanda Afrika jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Bi. Maria Bilia amesema kuna baadhi ya wafanyabiashara toka nje ambao hawataki kufuata taratibu za uwekezaji na sheria za nchi.
“Matokeo ya kutokufuata sheria za nchi katika uwekezaji au ufanyaji wa biashara ni uanzishwaji wa viwanda vinavyozalisha bidhaa ambazo hazikidhi viwango na ni hatari kwa Afya za walaji,”
“Sheria za nchi zipo wazi kwamba lazima Kituo cha Uwekezaji (TIC) na Brela msajili wa biashara wahusishwe kwenye mchakato mzima wa uwekezaji au biashara yeyote ndani ya nchi,” Bilia amesema
Amesema vile vile Wizara ya Viwanda kwa kushirikiana na Wizara zingine na taasisi za Serikali wanaendelea kurahisisha urasimishaji wa biashara kwa wanyonge kupitia mradi wa Mkurabita Mkakati wa Kurasimisha Biashara kwa Wanyonge ili kuwawezesha wazawa kufanya biashara zenye tija kwao na taifa kwa ujumla.
Bi. Bilia aliendelea kusema kuwa siku ya viwanda Afrika ilianzishwa mwaka 1989 na Tanzania ilijiunga rasmi mwaka 1990 katika kuhamasisha ukuaji wa viwanda katika kukuza uchumi wa nchi za Afrika.
Amesema sekta ya viwanda ikishirikishwa na sekta zingine inaweza kufanya mabadiliko haraka katika maisha ya mtu mmoja mmoja hususani ajira na hutoa bidhaa bora kwa matumizi ya binadamu.
Alisisitiza kuwa mwaka huu Serikali imepanga kuwa na maonyesho ya wiki nzima yatakayofikia kilele tarehe 20 mwezi huu ambapo wafanyabiashara mbalimbali watapata fursa ya kuonyesha bidhaa zao katika ukumbi wa PTA saba saba.
Amesema kauli mbiu ya mwaka huu ni “ Ni Ajira na ujasiriamali, Fursa ya Kuharakisha Maendeleo ya Viwanda Afrika katika juhudi za kupunguza makali ya umaskini na tatizo la ajira kwa vijana.
Kwa upande wake, Kaimu Mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda Nchini (CTI) Dkt. Samwel Nyantahe amesema shirikisho la viwanda linaunga mkono juhudi za serikali katika kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ili kuongeza mapato ya nchi.
“Sisi Shirikisho la Viwanda kwa kushirikiana na serikali na watu binafsi tutaendelea kuhamasisha jamii umuhimu wa viwanda katika kuongeza thamani ya bidhaa na kupambana na tatizo la ajira nchini,” amesema
Bw. Gerald Runyoro kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) amesema umoja wa mataifa kwa kushirikiana na serikali na wadau wengine wataendelea kusisitiza watu kuwekeza na kufungua viwanda ili kuharakisha maendeleo ya kiuchumi Afrika.
Amesema wafanyabiashara lazima wawe na ujasiri wa kufungua biashara au kiwanda katika juhudi za kuongeza thamani bidhaa zitokazo Afrika na kutafuta fursa za uwekezaji nje ya Afrika.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate