EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 22, 2013

WEMA, JOKATE WAMPONZA DIAMOND


Gumzo kubwa kwenye harusi ya staa wa dunia katika Kundi la P-Square wanaotarajiwa kuangusha shoo Bongo kesho, Peter Okoye mwishoni mwa wiki iliyopita, ni mwaliko wa msanii pekee wa Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye alipondwa kwa kuvaa suruali ‘njiwa’ (ya ajabuajabu).
Wema Isaac Sepetu.
Ishu hiyo ilijiri huko Lagos, Nigeria ilikofanyikia sherehe hiyo ambapo Peter alifunga ndoa ya kimila na mrembo wa haja, Lola Omotayo huku Diamond akipata fursa ya kukutana na baadhi ya mastaa wakubwa duniani, kasoro pekee ikawa kwenye mavazi.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo, Diamond alichemka kwa kuvaa kivazi hicho kifupi miguuni kikiwa na mistari myeupe na myeusi hivyo kusababisha kutukanwa mitandaoni.

WEMA, JOKATE KIVIPI?
Huku wakitumia picha za waliowahi kuwa wapenzi wa Diamond, Wema Isaac Sepetu na Jokate Mwegelo wakiwa wamevaa ‘taiti’ kama ‘kisuruali’ cha mwanamuziki huyo, walieleza kuwa inawezekana wao ndiyo walimdizainia hivyo kumsababishia matusi ya nguoni katika mitandao ya kijamii.
Jokate Mwegelo.
“Mafashenista wengi wanamtukana Diamond lakini inawezekana na zile nguo kadizainiwa na Wema au Jokate kwa sababu ni staili zao. Nao wana nguo kama hizo, hebu cheki kwenye picha,” alisema mmoja wa wachangiaji wa mada hiyo katika mitandao ya Naija huku akitundika picha za Wema na Jokate wakiwa wamevaa kama Diamond.

“Ni kweli Diamond amepata nafasi kubwa ya kukutana na mastaa wakubwa na kutangaza muziki wake kimataifa lakini kitu kimoja hakikwenda sawa.
“Ni juu ya nguo aliyokuwa ameivaa, mashabiki wengi wa muziki nchini Nigeria walisema kachemka,” ilisomeka sehemu nyingine ya maoni ya mashabiki wa muziki nchini humo.
Hata staa wa Nigeria aliyekuwa mmoja wa wenyeji wa Diamond, Iyanya alipoposti picha akiwa na Diamond pamoja na jamaa mwingine, ‘polisi jamii’ wa masuala ya mitindo waliendelea kugongea msumari wa moto kuwa Diamond akubali kuwa kachemka.

STAILI YA MICHAEL JACKSON?
“Iyanya, nani huyo kavaa suruali kama (marehemu) Michael Jackson? Mungu nisamehe kwa kukutenda dhambi lakini ukweli hicho kivazi hakiendani na mwili wake,” alifunguka shabiki mwingine kwenye ukurasa wa Iyanya wa Instagram.
Mwingine alisema: “Najua amekopi kwa mtu wake anayemhusudu (Wema), alionekana amependeza alipovaa hivyo walipokuwa China. Ukweli (Diamond) hakupendeza au labda kachukulia kwa Jokate wa Kidoti?”

ANGEENDA KUBADILISHA
Baadhi ya mashabiki hao walidai kuwa Diamond alipaswa kugundua kuwa yupo tofauti na mastaa wengine ili arudi hotelini mara moja akabadilishe nguo.
“Sijui alifikiria nini alipovaa hivyo, ona sasa amewaangusha na kuwadhalilisha mastaa wa Tanzania huko Afrika Magharibi.
“Ukweli ni kwamba kama alimuiga Wema na Jokate kachemsha, ona sasa wamemponza kwa kuvaa njiwa ya zebra kama wao.
“Diamond anajua kuvaa sana lakini anapaswa kuwa na dizaina wa kumpa ushauri wa mavazi kabla ya kwenda kwenye shughuli kubwa kama ile,” aliandika Mtanzania aishie Nigeria.

KAPATA ‘KIKI’?
Katika kujitetea huku akiamini kapata ‘kiki’ nchini Nigeria, Diamond alitumia ukurasa wake wa Instagram kwa kutundika picha yake akiwa na kisuruali hicho akiambatanisha na mastaa wakubwa wa Marekani kama akina Wiz Khalifa wakiwa wamevaa njiwa kama yeye kuonesha kuwa ni fasheni ya ‘mbele’.
Hata hivyo, hiyo haikusaidia kwani mashabiki hao waliendelea kumponda na kumtaka kujipanga zaidi siku akipata fursa kama hiyo kwani mastaa aliojifananisha nao walivaa hivyo katika ‘iventi’ tofauti na harusi.

MAMODO WANASEMAJE?
Ijumaa lilizungumza na baadhi ya mamodo maarufu wa Kibongo ambao walishuhudia vazi hilo ambapo walikuwa na haya ya kusema:
“Sijui ni nani aliyemdizainia lakini kilichofanyika ni kwamba alimvalisha Kimarekani, akasahau kuwa alitakiwa amvalishe Kiafrika au Kitanzania. Unajua harusi yenyewe ilikuwa ya kimila haikutaka Umarekani hata kidogo ndiyo maana watu walimponda Diamond. Naamini wakati mwingie aliyemvalisha atafanya vizuri,” alisema modo maarufu wa Kiume Bongo, Martin Kadinda.
“Unajua mitindo ya mavazi unaweza ukatulia, ukadizaini kitu lakini ukifika mbele za watu wakakushangaa, hiyo ndiyo fasheni ilivyo. Simlaumu Diamond wala sisemi alitakiwa ashone khanga au kitenge lakini iwe changamoto kwa mamodo wetu waongeze ubunifu,” alisema modo mwingine.
Pamoja na mambo mengine, safari ya Diamond nchini humo ililenga kwenda kufanya kolabo na mastaa wawili wa Nigeria, Davido na Iyanya.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate