EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 24, 2013

HIRIZI ZATUMIKA MAKANISANI


SIRI nzito imefichuka! Baadhi ya maaskofu na wachungaji (baadhi lakini) wa makanisa ya kilokole nchini wanadaiwa kutumia hirizi ili kujaza waumini.

SEHEMU ZINAZOKAA HIZIRI
Kwa mujibu wa mfichua siri huyo, watumishi hao wa Mungu wanaojihusisha na ushirikina wamekuwa wakizifunga hiziri hizo sehemu ya juu ya mkono wa kulia na kufichwa na shati la mikono mirefu ambalo nalo huwa ndani ya koti la suti.
Ikadaiwa kuwa, wengine huficha sehemu ya siri ya nguo ya ndani kulingana na maelekezo ya waganga wanaowatengenezea hirizi hizo.

WAUMINI NAO WANENA
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mapaparazi wetu jijini Dar juzi, baadhi ya waumini wa makanisa hayo ya kiroho walisema wamegundua kuwa, wapo viongozi wa makanisa hayo ambao hutumia nguvu za giza ili kuvuta waumini wengi.

LENGO LA KUTUMIA HIRIZI
Waumini hao ambao walidai wana uhakika kuna watumishi wa Mungu feki wengi siku hizi, walisema maaskofu na wachungaji wanaotumia hiziri wana lengo la kujipatia ‘kondoo’ wengi hivyo kuwa na uhakika wa kukusanya sadaka nyingi.

NI WALE WENYE NIA YA UTAJIRI TU
Habari zaidi zinadai kuwa, watumishi wa Mungu waliotumbukia kwenye ushirikina huo ni wale wanaosaka utajiri tu na neno la Mungu kwao si kitu cha lazima.
Watumishi hao wanadaiwa kusema kwenye madhabahu ya makanisa yao kwamba wameokoka, wanatembea na Bwana Yesu, lakini ndani ya mioyo yao hakuna ulokole wala uinjilisti zaidi ya blaablaa tu.

ROMANI, KKKT, ANGLIKANA WALIA
Ikazidi kudaiwa kuwa, pigo kubwa la kuwepo na kutanuka kwa makanisa ya kiroho nchini ni kwa Romani Katoliki (chini ya Kaldinali Polycarp Pengo) Walutheri, KKKT (chini ya uongozi wa Alex Malasusa) na Anglikana (lililokuwa likiongozwa na Valentine Mokiwa) ambao miaka ya karibuni makanisa yao yamemegwa, baadhi ya waumini wamekimbilia katika makanisa ya kiroho.
Hata hivyo, si waumini wote waliokimbilia kwenye makanisa hayo wapo kwa watumishi wanaodaiwa kutumia hiziri, wengine wapo kwenye makanisa salama.

WATUMISHI WA MUNGU WASAKWA
Kufuatia kufichuka kwa siri hiyo, Uwazi liliwatafuta viongozi mbalimbali wa makanisa nchini ili kuzungumzia madai hayo.

Aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania  ambaye sasa ni Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Dk. Valentine Mokiwa alipoulizwa juzi na Uwazi kuhusu kuwepo kwa matumizi ya hirizi kwa baadhi ya watumishi wa Mungu, alisema:

“Watu wanasema kuwa nguvu za giza hutumika katika baadhi ya makanisa ya kiroho, lakini kwa upande wangu sijaujua ukweli wala sijathibitisha kwa sababu ni mambo ya kishetani.
“Siku hizi dini imekuwa kama soko  kwani wengi hutumia uongo kanisani  kwa lengo la kuwajaza watu.”

Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo katika Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam, Josephat Gwajima kwa upande wake alisema wingi wa waumini katika makanisa mbalimbali ya kilokole hutokana na huduma nzuri na mafundisho mema yanayotolewa na wasimamizi wa makanisa hayo.

Kwa upande wake Kiongozi wa Kanisa la Huduma ya Maombezi,  Mbezi Salasala jijini Dar es Salaam, Nabii Flora Peter alisema mtumishi wa Mungu  kutumia hirizi katika kuendesha Neno la Mungu ni dhambi kubwa katika utumishi.

“Mungu hapendi, kama kuna  mtu wa namna hiyo  basi huyo hafai kuongoza kanisa  kwa sababu dini ni imani ya mtu, sasa haiwezekani utumikie  mabwana wawili,” alisema Nabii Flora.
Makamu wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Magnus Muhiche  yeye alisema hajawahi kuona ila anachokijua wingi wa watu katika makanisa ni sawa  na biashara.

Askofu John Said  wa Kanisa la Victoria lililopo Mabibo External jijini Dar es Salaam alipoulizwa kuhusu hilo  hakupenda kuchangia kitu chochote.
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi la Ubungo Kibangu jijini Dar, Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’  alipigiwa simu, hakupokea, akatumiwa ujumbe wa simu wa meneno (SMS) hakujibu licha ya ujumbe huo kurudiwa mara mbili kwa saa tofauti.

Mwaka 1993, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel & Bible Fellowship, Zakaria Kakobe alifanya mkutano wa Injili kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi, Gangilonga, Iringa ambapo baadhi ya wachungaji wa makanisa wa mkoa huo walifika kumshuhudia.
Baada ya mkutano kumaliza, wachungaji hao walisikika wakisema kuwa, walifika kwa lengo la kuthibitisha kwa macho yao uvumi ulionea kwamba, Kakobe anatumia hirizi kuhubiri, hasa wakati wa kuponya wagonjwa akiwa ameishika mkononi.

Wachungaji hao walishangaa mpaka mwisho wa mahubiri, Kakobe hakuwa ameshika hirizi na kumpongeza kwamba, kumbe maneno ya watu juu ya mtumishi huyo wa Mungu hayakuwa na ukweli hasa kwa jinsi alivyoliitia jina la Yesu kuponya watu.
CREDIT GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate