EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, December 30, 2013

MJAMZITO AJIFUNGULIA KWENYE KOKOTO


Kichanga baada ya kuzaliwa.
Stori: Gordon Kalulunga, Mbeya
MASIKINI! Mama mjamzito aliyetambulika kwa jina la Sabina Mwakyusa (28), mkazi wa Kijiji cha Iwala, Kata ya Utengule Usongwe wilayani Mbalizi mkoani hapa anadaiwa kujifungulia nje kwenye kokoto.
Mama aliyejifungua katika kokoto akiwa na mwanaye.
INASIKITISHA
Tukio hilo la kufungia mwaka lilijiri nje ya Hospitali Teule ya Ifisi-Mbalizi hivi karibuni na kusababisha masikitiko makubwa kwa mashuhuda waliodai kuwa ishu hiyo ni kali ya kufungia mwaka 2013.
Akizungumzia tukio hilo muda mfupi baada ya kujifungua, Sabina alisema alifika hospitalini hapo Desemba 18, mwaka huu na alipimwa na manesi ambapo walimwambia kuwa hawamuoni mtoto tumboni mwake.
“Baadaye alikuja daktari na kunipima, akaniambia mtoto anaonekana vizuri na ningejifungua mtoto wa kike ndipo nikaendelea kusubiri uchungu zaidi,’’ alisema kwa masikitiko.

UCHUNGU
Alisema ulipofika usiku wa Desemba 19, mwaka huu, alianza kujisikia uchungu, ndipo manesi waliompima mwanzo wakamwambia anatakiwa apimwe tena, jambo ambalo alikataa kwa madai kuwa alikuwa akiumia.
Alidai alipokataa kupimwa ndipo wakamwambia aondoke hospitalini hapo kwa sababu ana kiburi.
KUMBUKUMBU MBAYA
Mama mzazi wa mwanamke huyo, Roda Mwakyusa (50), alisema anaumia akikumbuka yaliyomkuta mwanaye ikiwa ni uzao wake wa kwanza.
Alidai walipotoka wodini huku mwanaye uchungu ukimzidi, walifika getini akazidiwa na kuanza kujifungua ndipo walinzi wa kampuni ya Mult-Lion, wakamsaidia kumpeleka katika upenu wa duka la hospitali hiyo ili kukwepa kokoto zilizopo na mvua iliyokuwa ikinyesha.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo ya ulinzi, Kinanda Sanga, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alikiri kwamba lilitokea na wao wakatoa msaada.

Naye wifi wa Sabina, Prisca Nafred, alisema alimpeleka mtoto aliyezaliwa katika hospitali hiyo saa 7:00 mchana wa Desemba 20, kwa ajili ya chanjo, lakini hakupata chanjo kwa madai kuwa alikuwa amechelewa kufika.

Desemba 21, familia hiyo ilimpigia simu mwandishi wetu na kumueleza kuhusu maendeleo mabaya ya mtoto ambapo mwanahabari wetu alitoa taarifa kwa Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto, Mkoa wa Mbeya, Prisca Butuyuyu ambapo makubaliano yalifikiwa kuwa mtoto apelekwe Hospitali ya Rufaa, Kitengo cha Wazazi Meta.

MTOTO ANAENDELEAJE?
Mtoto huyo alipokelewa Meta na kuingizwa kwenye chumba cha joto kisha kuanza kupatiwa matibabu kwa kuwekewa dripu za maji hadi Desemba 23, mwaka huu hali yake ilipotengemaa na sasa anaendelea vizuri.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Louis Chomboko, alipopata taarifa, alichukua hatua ya kwenda kumuona mtoto huyo Meta na kuahidi kulifuatilia suala hilo.

KIKAO
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ifisi Mbalizi, Msafiri Kimaro, Desemba 23, mwaka huu, alipopata taarifa hizo, aliitisha kikao cha wauguzi wanne waliokuwepo siku ya tukio, muuguzi mkuu, muuguzi kitengo cha chanjo.
Alisema wanawake zaidi ya 300 wanajifungulia hapo lakini tukio kama hilo hakumbuki kuwahi kutokea.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate