EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 27, 2013

SNURA, MAJANGA HADI MWILINI?

KWA wasiomfahamu msichana huyu, wanamuona kama chipukizi aliyeukwaa ustaa ghafla, lakini wanaofuatilia mambo ya sanaa na burudani, wanamfahamu kitambo. Ninamzungumzia Snura Mushi, ambaye anatamba sana na kibao chake cha Majanga.
 
Ni mmoja kati ya wasanii wapambanaji, wakisaka mafanikio kwa kujaribu kila aina ya njia. Amejaribu kwa muda mrefu katika filamu, lakini hakuweza kufanikiwa ‘kuchomoka’. Kama angetambua tokea mapema kuwa angeweza kuibuka mara moja katika muziki, nadhani asingepoteza muda wake mwingi kwenye filamu.

Wimbo wake wa Majanga umeiteka familia ya muziki wa mduara, huenda kwa sasa ni mmoja kati ya wasanii wachache wanaopata nafasi ya kutakiwa sana katika majukwaa na hivyo kumfanya pia awe anapata hela za kutosha.
 

Katika uigizaji, alifanikiwa kucheza vizuri katika filamu kadhaa, ingawa kama ninavyosema mara zote, viwango vibovu vya sinema za Tanzania vilisaidia kumfanya asing’ae!

Wimbo wa Majanga imempandisha sana chati, kwani licha ya maneno yake yaliyopangiliwa vizuri, pia midundo yake imeongeza thamani ya kibao hicho.
 
Lakini kama kuna kivutio zaidi katika maonyesho ya Snura, hasa katika wimbo wake huu, basi ni yeye mwenyewe. Ni kivutio kwa sababu anacheza wimbo wake kwa namna ambayo, ni mchanganyiko wa mshangao na hamasa za kingono.

Licha ya kucheza kwa umahiri mkubwa huku akikitumia zaidi kiuno chake, hali huwa tete pale anapoyatingisha na kuyatetemesha makalio yake huku akiwa amewapa mgongo mashabiki wake ambao hulipuka kwa shangwe.
 
Uvaaji na uchezaji wake hauvutii machoni mwa watu wenye kuzingatia maadili ya Kitanzania, kwa maana ya tabia njema. Ni kweli anashangiliwa sana, lakini natia shaka kidogo kama kinachoshangiliwa ni muziki wake au ni namna anavyocheza.

Akili yangu inaamini anashangiliwa kwa namna anavyocheza. Na kama hivi ndivyo, basi si jambo la kujivunia hata kidogo. Uchezaji wa msanii huyu, haustahili mbele ya watoto wetu wanaoupenda muziki wake na wala haupendezi machoni mwa wanaharakati wa maadili.

Binafsi ninaamini Snura ameshauwezea aina ya muziki wake huu, ndiyo maana ameanza kupata washindani kama Shilole, ambaye naye kwa bahati mbaya, anaamini katika kukata mauno, uvaaji usiofaa na ufundi wa kuchezea viungo vyake!
 
Uchezaji na uvaaji wake unaonekana pia nchi nzima kupitia video yake. Ni wazazi wachache wanaoweza kufurahia kuutazama wakiwa na watoto wao.

Kuna wakati nilipata kumsikia akitangaza kusaka mtu wa kumuoa. Kwa uchezaji ule jukwaani, sidhani kama anaweza kumpata mume anayemhitaji, isipokuwa watu wengi wenye tamaa ya ngono wanaweza kujitokeza. Hakuna mume makini anayeweza kukubali mkewe acheze na kuvaa namna ile.

Labda kwa faida yake binafsi nimshauri kujitazama upya kwa sababu kubadilika ni sehemu ya maisha. Kama anafikiri uvaaji na uchezaji ule ndiyo unampatia mashabiki, mimi nakataa kwa sababu najua muziki wake umekubalika, anaweza kuvaa na kucheza kawaida na bado akaendelea kuwa juu.
 
Ni vyema wasanii wetu wakatambua kwamba ustaa wao unawafanya wawe mfano. Huenda zile shangwe zinazotoka kwa mashabiki siyo za kumsifu kwa uhodari wake, bali ni kumzomea kwa jinsi anavyojidhalilisha.

Na pengine ni wakati muafaka pia kwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kuanza kutembelea kumbi na matamasha ili kuwabaini na kujua namna gani wanaweza kushughulika na watu wa aina hii. Hatuwezi kujenga taifa lenye maadili kama kila mtu ataachiwa kufanya anachotaka kwa sababu tu ya ustaa wao.
Kama wameweza kupiga kelele hadi sasa waigizaji wa filamu wameanza kuvaa nguo zinazokubalika, hata huku kwenye muziki wa kizazi kipya inawezekana. BASATA inao uwezo wa kuzipiga marufuku video na nyimbo zisizoendana na utamaduni wetu.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate