EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 21, 2013

WATANI KUAMUA NANI JEMBE LEO


Mashabiki wa timu ya Yanga Fc.
WATANI wa jadi katika soka nchini, timu za Yanga na Simba, leo zinashuka katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuhitimisha majigambo ya ‘Nani Mtani Jembe’ baina yao katika mechi kali inayofanyika chini ya uratibu wa mdhamini wao, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
                                                   Mashabiki wa timu ya Simba Fc.
Mbali ya wapenzi na mashabiki wa timu hizo kusubiri kuona ‘nani mtani jembe’ kati yao, pia watapata fursa ya kushuhudia nyota wapya waliosajiliwa kupitia dirisha dogo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu na Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema maandalizi ya mechi hiyo ya aina yake yamekamilika.

Wambura alisema vikosi vya ulinzi na usalama katika mechi ya leo vimekamilika kila idara na kwamba Barabara ya Taifa inayoanzia Keko-Maghorofani hadi Barabara ya Mandela, itafungwa kuanzia saa 12 asubuhi kupisha hekaheka za mtifuano huo.

Alisema magari hayataruhusiwa kuegeshwa kuanzia eneo la Baa ya Minazini hadi msikiti unaotazamana na Uwanja wa Uhuru, hivyo magari yote yataegeshwa nje ya Uwanja wa Ndani wa Taifa – kando ya Barabara ya Mandela.

“Magari yatakayoruhusiwa kuingia maeneo hayo na hata ndani ya Uwanja wa Taifa ni yatakayokuwa na stika zilizotolewa na TFF. Tunawaomba wadau na mashabiki wa soka kuheshimu na kutii maagizo ya vikosi vya ulinzi,” alisema Wambura.

Aliongeza kuwa milango ya kuingilia uwanjani itakuwa wazi kuanzia saa sita mchana ambapo baada ya mauzo ya tiketi ya jana, zoezi hilo litaendelea leo nje ya uwanja huo kabla ya mechi ili kuwapa mashabiki fursa ya kukata na kuingia moja kwa moja.

Pambano la leo linasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka wanaohitaji sio tu kuona nyota wapya waliosajiliwa na klabu hizo, pia kujua ‘nani jembe’ ndani ya uwanja kwani kwa nje ya uwanja, Yanga ni kama imeshinda kutokana na kuwa kwenye mazingira mazuri kisaikolojia.

Nje ya uwanja, Nani Mtani Jembe ilihusisha vita baina ya mashabiki wa kila klabu ‘kupora’ mamilioni ya mwingine kupitia shindano la kinywaji cha Kilimanjaro Premium Lager ambapo Simba ilizidiwa na Yanga kwa kiasi kikubwa cha pesa.

Ukiondoa shangwe ya mashabiki wa Yanga kumpata mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi akitokea SC Villa ya Uganda na Juma Kaseja, Simba leo itakuwa na makipa waliowahi kudaka Jangwani kwa vipindi tofauti, Ivo Mapunda na Yaw Berko.

Nyuma ya majina hayo makubwa, Yanga ilinasa saini ya kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu Shooting ya Pwani, wakati Simba iliwasainisha kwa mpigo kiungo mchezeshaji Awadh Juma Issa kutoka Mtibwa Sugar ya Morogoro na Ally Badru Ally kutoka Canal Suez ya Misri.

Kila timu ilishajichimbia kambini kunoa makucha kuelekea pambano hilo ili kusawazisha makosa yaliyowafanya watani hao kutoka sare ya 3-3 katika mechi ya raundi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa Oktoba 20.

Uwepo wa nyota wapya kwa kila upande ambao watashirikiana na wakali wengine, unalifanya pambano la leo liwe lenye mvuto wa aina yake ambapo kiingilio cha chini ni sh 5,000 kwa viti vya kijani.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu, kiingilio ni sh 7,000; viti vya rangi ya chungwa sh 10,000; VIP C ni sh 15,000; VIP B sh 20,000 huku VIP A sh 40,000.

Kwa upande wa waamuzi, kati atasimama Ramadhan Ibada ‘Kibo’ wa Zanzibar, atakayesaidiwa na Ferdinand Chacha wa Bukoba na Simon Charles wa Dodoma huku Israel Nkongo wa Dar es Salaam akiwa mezani. Kazi ya kutathimini utendaji wa waamuzi wote itakuwa chini ya Soud Abdi wa Arusha.

MECHI TANGU 2010

Rekodi ya watani hawa inaonyesha kuwa mechi ya leo ni ya tisa tangu mwaka 2010 na katika mechi nane, Yanga imeshinda tatu, Simba mbili na wamekwenda sare tatu.

Aprili 18, 2010: Simba 4, Yanga 3

Oktoba 16, 2010: Yanga 1, Simba 0

Machi 5, 2011: Yanga 1, Simba 1

Oktoba 29, 2011: Yanga 1, Simba 0

Mei 6, 2012:  Simba 5, Yanga 0

Oktoba 3, 2012: Yanga 1, Simba 1

Mei 18, 2013: Yanga 2, Simba 0

Oktoba 20, 2013: Simba 3, Yanga 3

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate