Ndugu
 zangu waandishi wa habari, awali ya yote naomba niwasalimie na 
niwapongeze kwa kufika -mwaka mpya 2014, pia naomba niwapongeze kwa kazi
 kubwa ambayo mmekuwa mkiifanya hasa kuhakikisha watanzania wanapata 
habari kwa kila jambo linaloendelea kila kona ya taifa letu la Tanzania.
Ndugu 
waandishi wa habari nimewaita hapa ili kuzungumza nanyi na mnisaidie 
kufikisha ujumbe kwa watanzania hasa kuhusu jambo hili ambalo limekuwa 
gumzo kwa watanzania wengi la mbio za urais 2015 kwa baadhi ya watu 
ndani ya chama changu cha mapinduzi (CCM), kilichonisukuma zaidi na 
kupata hamu ya kuongea nanyi ni baada ya kumsikia -na kumuona kijana 
wetu ndani ya chama cha mapinduzi bwana Paul Makonda akiwa na ujasiri wa
 kukemea vitendo mambo haya yanayofanywa na baadhio ya viongozi bila 
uwoga wowote naomba tuchukue fursa hii kumpongeza sana kijana huyu.
Nadiriki
 kusema nampongeza kijana huyu hasa kwa kauli zake nzito na za kijasiri 
kwa maslahi ya chama changu cha CCM ili chama kiendelee kupendwa na 
kuchaguliwa na watanzania.
Pia 
itakuwa si busara kama sitawapongeza vijana wangu katibu mkuu wa chama 
ndugu ABDULRAHMAN KINANA na NAPE NNAUYE kwa juhudi zao za dhati za 
kujenga chama na kuendelea kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya 
chama cha mapinduzi (CCM) kwa kuwakemea viongozi wasiofaa bila kujali 
cheo na umaarufu wao ndani ya chama na serikali, nawaomba waendelee -na 
juhudi zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watru 
wanaowabeza naomba wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ndani ya 
chama na serikali ni msingi wa chama chochote kilichounda serikali.
Aidha 
nawaomba watanzania wenzangu wazalendo wasikubali kukatishwa tama na 
kikundi cha watu wachache wasio na mapenzi mema na taifa letu ambalo 
limekuwa mfano wa kuigwa kwa amani, upendo, utulivu na mshikamano urithi
 tulioachiwa na baba yetu wa taifa mwalimu julias kambarage nyerere 
ndani na nje ya mipaka ya bara letu la afrika.
Ndugu 
zangu waandishi wa habari naomba niwaambie kuwa msemaji wa UVCCM kijana 
wetu Paul Makonda namuunga mkono kwa -kitendo chake cha ujasiri cha 
kumkemea ndugu EDWARD NGOYAI LOWASSA bila uwoga kwa jinsi anavyokivuruga
 chama chetu kwa lengo la kutaka urais 2015 huku secretariet ya chama 
ikiwa imekaa kimya wakati inajua kuwa muda wa kuanza mbio hizi bado na 
kufanya hivi kwa sasa ni kukiuka misingi na katiba -ya chama. Hapa 
najiuliza kuwa ile misingi imara ya uongozi ndani ya chama chetu cha 
mapinduzi iko wapi? Mpaka tumuachie mototo ndio akemee haya? Je, hapa 
chama kiko wapi?
Ukweli
 ni kwamba wanachama wetu na vijana wamekuwa njia panda huku wakitamani 
kusikia tamko au karipio la chama juu ya suala hili la harakati za urais
 2015 bila mafanikio.
Naomba
 niseme kuwa bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia 
pesa zao hadharani kwa lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa 
vijana ili kupata madaraka wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi 
iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya chama.
Kinachonisikitisha
 zaidi ni kuona juhudu za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni
 pamoja na sekretarieti inayoongozwa na katibu mkuu ABDULRAHMANI KINANA 
na katibu mwenezi NAPE NNAUYE za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga.
Ninaomba
 juhudi hizi zisibezwe na watu wenye nia njema na chama. Ukweli ni 
kwamba vijana hawa wamekuwa na juhudi kubwa sana ya kujenga na 
kuimarisha chama chetu -kwa wananchi kila pembe ya taifa letu kwa 
kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. Swali: Je! Chama hakioni 
haya mpaka vijana ndio waone?
Kwa 
hili ni lazima tubadilike ili kujenga chama chetu na naishauri 
-secretariet ya chama lazima ichukue hatua mara moja, kijana huyu paul 
makonda asingesema haya yote kama hana uhakika wa ushahidi wa wa haya 
aliyoyasema na nampongeza sana.
Vijana
 na wanachama wengi wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka 
kujua msimamo wa chama chao bila mafanikio na ndio sababu ya baadhi 
ya-wengine kupoteza mwelekeo.
Sisi 
tulikijenga chama hiki kwa taabu sana hapakuwa hata mtu mmoja 
aliyediriki kutumia fedha zake kutaka madaraka. Nidhamu, busara na 
uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa maslahi ya wananchi ndio 
vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi ndani ya chama na 
serikali, ndio maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka kutekwa na 
wenye fedha kwa uchu wa madaraka, mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi 
pesa wanatoa wapi? Na haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa 
maslahi ya nani? Huku watanzania wakiendelea kuwa maskini.
Mfano 
hivi karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana 
kwenye vyombo vya habari,vitendo hivi havina tija kwa chama na wala 
havileti umoja na mshikamano ambao umedumu ndani chama kwa muda mrefu.
Mwisho
 Ninaomba sekretarieti ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu 
makonda na kweli kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi 
kwamba utaleta kutokuelewana ndani ya chama kusiko kuwa na lazima.
JOHN SAMWELI MALECELA
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
 
 
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment