 Mkuu
 wa Wilaya ya Kilolo,Mh.Gerald Guninita akifungua kikao cha DCC katika 
ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya,Kushoto ni Mkurugenzi Ruukia Muwango na 
Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya,kikao kilichofanyika 
mwisho mwa wiki katika ukumbi wa halmashauri hiyo.
Mkuu
 wa Wilaya ya Kilolo,Mh.Gerald Guninita akifungua kikao cha DCC katika 
ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya,Kushoto ni Mkurugenzi Ruukia Muwango na 
Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya,kikao kilichofanyika 
mwisho mwa wiki katika ukumbi wa halmashauri hiyo.
WANAFUNZI 1725  WASHINDWA KURIPOTI SHULENI WILAYA YA KILOLO
JUMLA
 ya wanafunzi 1725 waliotakiwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza 
katika shule mbalimbali zilizoko katika Wilaya ya Kilolo wameshindwa 
kuripoti kutokana na sababu mbalimbali.
 
Akizungumza katika kikao cha 
Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) kilichofanyika katika ukumbi wa 
halmashauri ya wilaya ya Kilolo mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mtendaji  
wa Halmashauri hiyo, Rukia Muwango  alisema wanafunzi wasioripoti kati 
ya hao wavulana walikuwa 788 na wasichana 937 sawa na asilimia 56.1
Muwango alisema wanafunzi waliochaguliwa 
kwa halmashauri ya wilaya ya Kilolo ni wanafunzi 3101 wavulana 1442, 
wasichana 1658 kati ya hao wavulana 10 na wasichana 10 wamechaguliwa 
katika shule za bweni.
Alisema wanafunzi waliopangwa kwenda katika
 shule za ufundi walikuwa wavulana 6 na hakuna msichana aliyechaguliwa 
na wanafunzi 3074 walipangwa katika shule za serikali katika halmashauri
 ya wilaya ya Kilolo.
Aliongeza kuwa wanafunzi walioripoti hadi 
Januari 23 mwaka huu walikuwa wanafunzi 1349 wakiwemo wavulana 638 na 
wasichana 711 sawa na asilimia 43.
Muwango alizitaja shule ambazo zina 
asilimia ndogo ya wanafunzi walioripoti shuleni kuwa ni shule ya 
Sekondari Mawambala (5.2%), Mlafu (14%), Lukosi (19.3%),Udekwa (21%) na 
Mtitu yenye asilimia 29 ya wanafunzi walioripoti.
Aliwataka walimu wa wakuu shule za 
sekondari wawasilishe majina ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2014 
waliojiunga katika shule zao ili halmashauri iweze kujua na kujiridhisha
 kuwa wanafunzi wote wapo shuleni na kutoa taarifa kwa wanafunzi 
wanaokwenda shule za zisizo za serikali kupata takwimu sahihi.
Alisema kuwa halmashauri imeandaa mikakati 
kwa wanafunzi wasioripoti kwa kuwaandikia barua waratibu wote 
kuwafatilia wanafunzi  hao na kuwahimiza kuhudhuria katika shule 
walizopangiwa.
 
Kwa upande wa ke Mkuu wa Wilaya hiyo Gerald Guninita 
amewataka watendaji wawasisitize wazazi kuwapeleka watoto shule bila 
kujali suala la ada na sare za shule.
Aliwataka watendaji kupeleka ripoti ndani ya siku 24 kwa wanafunzi wote ambao hawajaripoti shuleni hadi sasa katika ofisi ya wilaya na kuwachukulia hatua wazazi wakaidi.
Aliwataka watendaji kupeleka ripoti ndani ya siku 24 kwa wanafunzi wote ambao hawajaripoti shuleni hadi sasa katika ofisi ya wilaya na kuwachukulia hatua wazazi wakaidi.
“Haki ya mtoto kupata elimu ni muhimu sana 
na tusiache wazazi wanaowaficha watoto ndani hivyo wabanwe wazazi wao 
kwa kuwaficha kuna kitu nataka kuwaambia kumpeleka shule mtoto ni 
kumwongezea thamani mtoto na mzazi mwenye katika maisha yetu ya kila 
siku hivyo nawsisitiza sana watendaji wabaneni  sana wazazi wote 
wasiotaka kuwapeleka watoto wa kike shule” alisema Guninita.
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment