EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, January 27, 2014

WANAFUNZI 1725 WASHINDWA KURIPOTI SHULENI WILAYA YA KILOLO

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo,Mh.Gerald Guninita akifungua kikao cha DCC katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya,Kushoto ni Mkurugenzi Ruukia Muwango na Kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya,kikao kilichofanyika mwisho mwa wiki katika ukumbi wa halmashauri hiyo.
Mkurugenzi wa wilaya ya Kilolo Rukia Muwango akisoma taarifa ya wilaya hiyo mbele ya wajumbe wa kamati ya wilaya katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa wilaya mwishoni mwa wiki.
WANAFUNZI 1725  WASHINDWA KURIPOTI SHULENI WILAYA YA KILOLO
JUMLA ya wanafunzi 1725 waliotakiwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza katika shule mbalimbali zilizoko katika Wilaya ya Kilolo wameshindwa kuripoti kutokana na sababu mbalimbali.
 
Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kilolo mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri hiyo, Rukia Muwango  alisema wanafunzi wasioripoti kati ya hao wavulana walikuwa 788 na wasichana 937 sawa na asilimia 56.1

Muwango alisema wanafunzi waliochaguliwa kwa halmashauri ya wilaya ya Kilolo ni wanafunzi 3101 wavulana 1442, wasichana 1658 kati ya hao wavulana 10 na wasichana 10 wamechaguliwa katika shule za bweni.
Alisema wanafunzi waliopangwa kwenda katika shule za ufundi walikuwa wavulana 6 na hakuna msichana aliyechaguliwa na wanafunzi 3074 walipangwa katika shule za serikali katika halmashauri ya wilaya ya Kilolo.

Aliongeza kuwa wanafunzi walioripoti hadi Januari 23 mwaka huu walikuwa wanafunzi 1349 wakiwemo wavulana 638 na wasichana 711 sawa na asilimia 43.
Muwango alizitaja shule ambazo zina asilimia ndogo ya wanafunzi walioripoti shuleni kuwa ni shule ya Sekondari Mawambala (5.2%), Mlafu (14%), Lukosi (19.3%),Udekwa (21%) na Mtitu yenye asilimia 29 ya wanafunzi walioripoti.

Aliwataka walimu wa wakuu shule za sekondari wawasilishe majina ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2014 waliojiunga katika shule zao ili halmashauri iweze kujua na kujiridhisha kuwa wanafunzi wote wapo shuleni na kutoa taarifa kwa wanafunzi wanaokwenda shule za zisizo za serikali kupata takwimu sahihi.
Alisema kuwa halmashauri imeandaa mikakati kwa wanafunzi wasioripoti kwa kuwaandikia barua waratibu wote kuwafatilia wanafunzi  hao na kuwahimiza kuhudhuria katika shule walizopangiwa.
 
Kwa upande wa ke Mkuu wa Wilaya hiyo Gerald Guninita amewataka watendaji wawasisitize wazazi kuwapeleka watoto shule bila kujali suala la ada na sare za shule.
Aliwataka watendaji kupeleka ripoti ndani ya siku 24 kwa wanafunzi wote ambao hawajaripoti shuleni hadi sasa katika ofisi ya wilaya na kuwachukulia hatua wazazi wakaidi.

“Haki ya mtoto kupata elimu ni muhimu sana na tusiache wazazi wanaowaficha watoto ndani hivyo wabanwe wazazi wao kwa kuwaficha kuna kitu nataka kuwaambia kumpeleka shule mtoto ni kumwongezea thamani mtoto na mzazi mwenye katika maisha yetu ya kila siku hivyo nawsisitiza sana watendaji wabaneni  sana wazazi wote wasiotaka kuwapeleka watoto wa kike shule” alisema Guninita.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate