EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 27, 2014

AUNT WA NDOA, AUNT WA BILA NDOA MULEMULE

Katika jamii pana inafahamika kuwa mwanamke akiingia kwenye ndoa huwa anatulia na kujipanga kwa ajili ya familia na maendeleo kwa jumla.
Hali ni tofauti kabisa kwa staa wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson Jujuman.
Aunt ana utofauti mkubwa na wanandoa wengine kwani maisha anayoishi tangu aingie kwenye ndoa na Sunday Demonte, hayana tofauti na yale aliyokuwa akiishi kabla hajaingia kwenye ndoa miaka miwili iliyopita.
Aunt amekuwa akijiachia sehemu mbalimbali za starehe bila kujali kama ni mke wa mtu na amekuwa akikumbwa na skendo lukuki.
Hali hiyo imekuwa ikiwashangaza wengi na kujiuliza kweli ni mke wa mtu?
Katika makala haya utaona matukio mbalimbali ambayo Aunt amewahi kuyafanya tangu aingie kwenye ndoa ambayo si kitu cha kawaida kwa mwanandoa.
KUKAA NUSU UTUPU JUKWAANI
Siku chache baada ya kufunga ndoa, mwaka 2012, Aunt alikwenda kwenye shoo ya Fiesta mjini Dodoma akiwa ameambatana na Wema Isaac Sepetu na kufanya kituko cha mwaka.
Akiwa kwenye shoo hiyo, Aunt alipanda jukwaani akiwa nusu utupu ambapo alipigwa picha ambazo zilizua gumzo kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Ishu ilikuwa iweje mke wa mtu afanye hivyo bila aibu?
Skendo hiyo ilimfanya Aunt na Wema kutengwa na Shirikisho la Filamu (TAFF) lakini baadaye waliomba msamaha na kupewa onyo wasirudie kuvaa hivyo na endapo wangerudia wangeondolewa kabisa kwenye listi ya wasanii wa Tanzania.
KUPIGWA CHUPA
Mwaka jana ndani ya Klabu ya Bilicanas iliyopo Posta, Dar, Aunt alipasuliwa na chupa mkononi baada ya kumkosakosa usoni na aliyetekeleza unyama huo ni mwanadada aliyejulikana kwa jina la Yvonne Maximilian ambaye kabla ya Aunt kuingia kwenye ndoa walikuwa wakimgombea mwanaume aitwaye Geofrey.
Japokuwa Aunt alishaingia kwenye ndoa bado skendo hiyo ya kutembea na huyo mwanaume ilikuwa ikimsumbua Yvonne akihisi kwamba mwanadada huyo anaendelea na Geofrey, jambo ambalo Aunt alisema siyo kweli na waliachana muda mrefu kabla hata hajaingia kwenye ndoa.
SKENDO YA KUJIUZA
Hivi karibuni Aunt alikumbwa na skendo ya kujiuza baada ya kwenda jijini Arusha akiwa ameambatana na Wema na Kajala Masanja ambako walienda kwenye shoo ya kumtambulisha msanii wa Bongo Fleva, Mirrow kutoka kampuni ya Wema ya Endless Fame Films.
Ilidaiwa kwamba nyuma ya ziara hiyo kulikuwa na mabilionea waliowaita jijini humo ambao pia walifurika kwenye shoo hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Tripple A.
KUPIGANA
Mapema mwaka huu, Aunt alijikuta akizichapa na mwanamke aitwaye Sarah Mwakapala ambaye miaka kadhaa iliyopita waliwahi kugombea naye penzi  la mwanaume aliyejulikana kwa jina la Mwilu Mwilola ‘Silva’.
Chanzo cha wawili hao kuzichapa hadi kuvuana mawigi hakikueleweka lakini Aunt alishtuka baada ya kuvamiwa na mwanadada huyo wakiwa katika sherehe kwenye Ukumbi wa Letasi Lounge uliopo Victoria, Dar.
Aunt anapaswa kubadilika na kuonesha sifa za mke wa mtu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate