EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 1, 2014

MASKINI AFANDE SELE

SIKU chache baada ya kuzagaa kwa taarifa za kuachana na mkewe mama Tunda, mfalme wa Rhymes, Seleman Msindi ‘Afande Sele’ ameibuka na kusimulia mambo ya kusikitisha waliyopita katika safari ya maisha yao.
Mfalme wa Rhymes, Seleman Msindi ‘Afande Sele’.
Akizungumza na wanahabari wetu ndani ya Ukumbi wa Meeda, Sinza-Mori, Dar, juzi Afande alisema hadi kufikia hatua ya yeye kutangaza kuwa ameachana na mama Tunda ambaye amedumu naye kama mume na mke kwa zaidi ya miaka 10, alikuwa akivumilia mambo mengi na mwisho kuamua kuachia ngazi.

Afande Sele akiwa na familia yake.

“Nilikuwa nikielezwa mengi kuhusu mke wangu, nilishapigiwa simu na kuambiwa mke wangu anagombaniwa na wanaume usiku klabu lakini huwa mimi siyo mtu wa kuishi kwa hisia, nilivumilia nikiamini atajirekebisha, haikuwa hivyo.
“Japo sikuwa na uthibitisho wa moja kwa moja, lakini nyumbani alikuwa siyo mtu wa kutulia, amekuwa akinizunguka hadi kwa washkaji zangu wa karibu. Kuna jamaa alichoshwa na habari hizo akanifuata na kuniambia hata kama lakini uvumilivu wangu ulizidi,” alisema Afande kwa hisia.
Akiendelea kushusha masikitiko yake mbele ya kinasa sauti cha Risasi Jumamosi, Afande alienda mbele zaidi kwa kusema mbali na mkewe huyo kumsaliti kwa wanaume tofauti wakiwema marafiki zake, ilifika wakati mama Tunda akawa anachukua fedha ndani na kwenda kutumia na wanaume.
Alisema alitumia mwanya wa mkali huyo wa mashairi anapokuwa amesafiri katika shoo mbalimbali na kuachiwa fedha za matumizi pamoja na ujenzi wa nyumba yao mpya, kutanulia.
“We acha tu, yaani fedha za matumizi, ujenzi nilikuwa namuachia lakini cha kusikitisha ni kwamba alizitumia kutanulia, jambo ambalo nililizidi kunitia umaskini na machungu ukizingatia jamii inaniheshimu kama msanii, mbaya zaidi wananchi wamenitaka nigombee ubunge Morogoro Mjini,” alisema Afande.
Akizidi kushusha ‘vesi’, Afande alitiririka kuwa kuna wakati aliwahi kupewa taarifa na rafiki yake mwingine aishie Kurasini jijini Dar ambaye alilamika juu ya mkewe kufika kwa jamaa huyo na kuazima fedha bila kuzilipa.
Kwenye aya nyingine, mkali huyo alisema anakumbuka jinsi alivyoishi na familia yake, mkewe, wanaye Tunda na Ahsante Sanaa lakini hana jinsi kwani ameona bora kuachana kwani umri wake una mruhusu kuoa mke mwingine siku ikitokea.
“Nakumbuka maisha kidogo ya furaha na familia, mama Tunda atabaki kuwa mama wa watoto wangu lakini kamwe hawezi kurudi kwangu kwani itakuwa ni aibu juu ya aibu,” alisema.
Afande aliachana na mama Tunda mwishoni mwa mwaka jana alipotimba jijini Dar katika shughuli zake za kikazi na kumuachia mkewe fedha za ujenzi lakini aliporejea nyumbani Morogoro, alikuta mzazi mwenzake huyo ameondoka nyumbani na kuacha funguo, kila alipompigia simu hakupokea.
Alipoulizwa kuhusiana na shutuma zilizoporomoshwa na Afande, mama Tunda alitiririka:
“Alinipa Sh. milioni 3 za shoo tu, tukanunua vifaa vya ujenzi lakini siyo kwamba nilitanua na wanaume, tena kama ni kumfumania, mimi ndiye nilimkuta na mwanamke alitoka naye Fiesta Dodoma, sikutaka tu kumsema, hizo taarifa anazusha tu.
“Kwanza kuna mambo mengi tu amenifanyia, alikuwa mlevi kwani hadi wazazi wangu walikuwa wakinishangaa sana, sasa na mimi nikaona bora niachane naye,” alisema mama Tunda.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate