Mkuu
 wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa akifungua mkutano wa siku ya wadau wa 
Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo la 
mkutano huo ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA 
inavyofanya kazi. Kikao hicho kimefanyika leo Machi 28, 2014 katika 
ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Pembeni ni Mkuu wa Wilaya ya 
Korogwe, Mheshimiwa Mrisho Gambo (kushoto) na Mwenyekiti wa Hamashauri 
ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello 
Bendera (kulia).
Mkuu
 wa Wilaya ya Korogwe, Mheshimiwa Mrisho Gambo akitoa ufafanuzi wa jambo
 mbele ya mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa (kushoto). Pembeni
 ni Diwani wa Kata ya Mgombezi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, 
Afya, Maji na Uchumi, Mheshimiwa Omari Chafesi na Meneja wa Mfuko wa 
Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu 
(kushoto).
Mwenyekiti
 wa Halmashauri ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, 
Mheshimiwa Angello Bendera (kushoto) akiendesha mkutano wa siku ya wadau
 wa Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo 
la mkutano huo ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA 
inavyofanya kazi. Pembeni ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa 
Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji 
Korogwe, Dokta Jerry Mwakanyamale.
Afisa
 Matekelezo na Uratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) – 
Singida, Bw. Issaya Shekifu akitoa uzoefu wake katika moja ya Wilaya ya 
Ilamba, Singida jinsi wananchi wanavyofaidika na TIKA.
Viongozi
 wa Dini wakifuatilia mkutano wa siku ya wadau wa Mfumo wa Afya ya Jamii
 Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo la mkutano huo ilikuwa ni 
kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA inavyofanya kazi.
Wananchi
 wa Mji wa Korogwe wakifuatilia mkutano wa siku ya wadau wa Mfumo wa 
Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo la mkutano huo
 ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA inavyofanya kazi.
Wananchi
 wa Mji wa Korogwe wakifuatilia mkutano wa siku ya wadau wa Mfumo wa 
Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo la mkutano huo
 ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA inavyofanya kazi.
Wananchi
 wa Mji wa Korogwe wakifuatilia mkutano wa siku ya wadau wa Mfumo wa 
Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo la mkutano huo
 ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA inavyofanya kazi.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa akisalimiana na Mjumbe wa Kamati ya Msikiti Mkuu Manundu, Korogwe Mzee Daffa Daffa.
Mkuu
 wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa akisalimia na viongozi wa dini wa 
Halmashauri ya Mji Korogwe mara baada ya kumaliza kufungua mkutano wa 
siku ya wadau wa Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) 
ambapo Lengo la mkutano huo ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza 
jinsi TIKA inavyofanya kazi.
Waheshimiwa
 Madiwani wa Kata mbalimbali za Halmshauri ya Mji Korogwe wakiwa katika 
mkutano wa siku ya wadau wa Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa 
Kadi (TIKA) ambapo Lengo la mkutano huo ilikuwa ni kuchukua maoni yao na
 kuwaeleza jinsi TIKA inavyofanya kazi.
NHIF
 11: Afisa Matekelezo na Uratibu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya 
(NHIF)- Dar es Salaam, Genoveva Vicent akitoa majumuisho jinsi Mfumo wa 
Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) unavyoweza kuwasaidia 
wananchi.
 Mchungaji
 Joseph Mhina wa Kanisa la Anglikana Manundu, Korogwe akitoa shukrani 
kwa wananchi waliofika katika mkutano huo wa wadau. 
Timu
 ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Dar es Salaam 
na Tanga waliokuwa wakiratibu mkutano huo wakiwa katika picha ya pamoja 
na Mkuu wa Mkoa na Wilaya. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason 
Blog.
---
MAAZIMIO YA KIKAO CHA WADAU WA TIKA KATIKA HALMASHAURI YA MJI KOROGWE:-
1.
 Washiriki wote wa kikao wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga 
wamekubaliana kwa kauli moja kukatwa Tshs.10,000 za posho zao kama 
mchango wa TIKA ili kusaidia wazee na wenye mahitaji maalumu.
2. Kila mshiriki awe mwalimu na mhamasishaji kwa wale wote ambao hawakupata fursa ya kuhudhuria kikao hiki cha wadau wa TIKA
3.
 Mfuko wa TIKA ni mali ya wana Korogwe hivyo kila mwananchi mwenye uwezo
 na mfanyakazi achangie kiwango cha Tshs.10,000 kama mchango wa TIKA kwa
 mwaka kwa mtu mmoja.
4. Watendaji wa Mitaa,Kata na halmashauri wawe karibu na wenyeviti wa mitaa katika kuhamasisha jamii kujiunga na TIKA.
5.
 Kuhamasisha wanakorogwe walio nje ya Korogwe kuchangia Mfuko wa TIKA 
kwa kiwango kilichowekwa ili kuuboresha mfuko na kusaidiwa wenye 
mahitaji muhimu na wazee.
6. Wana Korogwe wenye uwezo zaidi kiuchumi waliopo Korogwe waombwe kuchangia mfuko huu ili kuuboresha.
7.
 Kuhamasisha makundi maalumu kujiunga na TIKA mfano walemavu,na 
wawakilishi wao waliohudhuria semina hii wakawe mfano kwa kujiunga na 
TIKA na kuhamasisha wenzao.
8.
 Watendaji wa Kata na Mitaa/Vijiji waitishe mikutano ya hadhara kwa 
ajili ya uhamasishaji na washarikiane na washiriki waliopata 
mafunzo/semina hii.
9. Viongozi wa dini watatumia vikao vya kidini kwa ngazi zote kitaka kuhamasisha jamii na waumini (misikitini na makanisani)














No comments:
Post a Comment