EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, June 27, 2014

FLORA MBASHA, KUMBUKA MAANDIKO!

MIMI ni mkristo wa dhehebu la Roma. Mafundisho mengi tunayopewa kuanzia Ubatizo, Komunyo ya Kwanza na Kipaimara, tunafundishwa kuhusu kutenda mema, kupendana wenyewe kwa wenyewe na hata kuwapenda maadui zetu.
Tunaambiwa, akija mtu akakupiga kofi shavu lako la  kushoto, wala hata usimrudishie, bali mgeuzie na upande ule wa kulia na akishakutundika hivyo vibao vyake, muombe Mwenyezi Mungu amsamehe. Tunafundishwa kusamehe, ndiyo maana katika moja ya maandiko yaliyo katika vitabu vya dini, kama Injili na Biblia, kuna mistari inayosema samehe saba mara sabini.

Kwa wale ndugu zangu wasio wakristo, nitaomba niwaombe radhi kwa kuanza na utangulizi huu. Ni kwa sababu leo nazungumza na mtu ambaye wengi wetu tunaamini ni mtumishi wa Mungu. Mtu yeyote anayesambaza neno la Mungu, huwa ni mtumishi wake. Neno zuri la Mungu husambazwa kupitia mihadhara, misa, maombi na hata nyimbo kama Flora Mbasha anavyofanya.
Leo nikiambiwa niwataje waimbaji wa Injili kumi bora nchini, jina la Flora Mbasha litakuwa katikati yao, likigawa kundi moja juu yake na lingine chini yake. Hii ni kwa sababu ni mmoja wa waimbaji wazuri wa muziki huu. Hujisikia furaha ninaposikiliza ujumbe uliomo katika nyimbo zao, ingawa baadhi ya kazi zake huchezeka, lakini ujumbe wake maridhawa hubakia kuwa fumbo.
Familia ya watu wa muziki wa Injili nchini, imepata mshtuko mkubwa wiki chache zilizopita, baada ya waimbaji, ambao ni wanandoa, Emmanuel na Flora Mbasha kupamba vichwa vya habari baada ya kutokea mzozo wa kifamilia kati yao, ambao unadaiwa kusababisha mwanaume kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za ubakaji.
Sitaki kuzungumzia suala lililopo kortini kwa sababu sheria zinakataza, isipokuwa nataka kuzungumza na mdogo wangu Flora kwa sababu alichokifanya katika kipindi chote cha mtafaruku baina yao, hakikupaswa kufanywa naye hasa kwa jinsi alivyofanikiwa kujitengenezea taswira ya kuheshimika mbele ya jamii.
Huwa najaribu kusema mara nyingi, ustaa ambao baadhi yetu hatulali kwa kuutafuta una gharama kubwa. Ukishakuwa mtu maarufu, unajinyima baadhi ya haki zako za msingi, kama vile masuala yako binafsi kubaki kuwa ya kwako.
Ninafahamu Flora, kama mke ana haki ya kukataa baadhi ya mambo kufanyika katika ndoa yake. Sisi tulio katika ndoa tunafahamu, kuna maisha magumu kweli, wakati mwingine mume na mke huweza kukaa hata mwezi mzima bila kuzungumza, lakini kwa sababu ya kuhifadhi matatizo yenu yasitoke nje, mnakaa kimya.
Akija jirani, hawezi kujua kama hamzungumzi kwa namna mtakavyompokea kwa bashasha na kumpa ushirikiano.
Kama kukaa kimya ili mambo hayo yaishe yenyewe kimyakimya mnashindwa, kinachotokea ni kuwafuata ndugu wa karibu, ambao mara nyingi huwa ni wale waliowazidi umri. Mnapeleka tatizo lenu, mnaitwa, mnajadiliana kwa pamoja, mnaondoka na muafaka!
Haya mambo yangeweza kufanywa na Flora, hasa kwa kuwa jamii inamtambua kama mtu mwenye woga na Mungu. Sasa kama mtu anayetakiwa kuwa mfano, anaondoka nyumbani kwake na kwenda kusikojulikana, tena wakati mumewe akiwa katika matatizo, unataka watu wakutazame kwa macho yapi?
Sitaki kusema nani mwenye makosa kati yao, ninachotaka kusema ni kitendo cha Flora kuifanya jamii ione ni kama anayefurahia matatizo yanayomzonga mumewe. Hii siyo sawa, hata kama ndani hatuongei, nje sisi ni kitu kimoja.
Wakati akiwa madarakani, Rais wa Marekani, Bill Clinton aliwahi kukutwa na tuhuma za kumbaka mfanyakazi wa Ikulu, Monica Lewinsky. Katika kipindi chote cha sakata hilo, mkewe Hilary, alikuwa upande wake, hakumuacha, alikuwa tayari kufa naye, kuliko kuongeza petrol kwenye moto. Nani anajua waliishije wakiwa chumbani kwao?
Flora anatakiwa kutambua kuwa kuna ndoa chache sana zinaishi kwa upendo kama tunavyoziona.
Kitu kikubwa tunachopaswa kufanya, hasa kwa mastaa ni kuzilinda ndoa zetu kwa mikono yetu wenyewe.

1 comment:

  1. Sasa hii blog yako ina tofauti gani na Global Publishers? Naomba una-copy huko na ku-paste tu hapa tena hovyo hovyo tu na bila kutoa credit.

    Kweli Shigongo ni mkombozi wa jamii kwani bila yeye wengine haki ya nani mngekufa na njaa hapa mjini. Bila shaka vijihela vya adsense na hayo matangazo hapo juu yanasaidia japo huu ni wizi tu kama wezi wengine...Siku ukienda kanisani basi katubu pia kuhusiana na hii dhambi ya kuiba vitu vya watu mtanadoni hovyo hovyo. Malaya mkubwa!!!

    ReplyDelete

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate