EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 24, 2014

SANGOMA AINYWESHA FAMILIA DAWA

MGANGA mmoja wa jadi, hivi karibuni alikusanya umati mkubwa wa watu baada ya kuinyeshwa dawa familia nzima ya mwanamke aliyemleta kwa lengo la kumfanyia uganga ili kumrejesha mtoto wake aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha mjini hapa.
Mwajuma Bakari Tindwa mwenye umri wa miaka 52, mkazi wa Mwembesongo aliyemleta mganga akiandaliwa dawa ili kumrejesha mtoto aliyepotea.
Tukio hilo lilitokea Jumamosi ya wiki iliyopita baada ya Mwajuma Bakari Tindwa mwenye umri wa miaka 52, mkazi wa Mwembesongo kumleta mganga huyo, Omar Ally ili amrudishe mtoto Omar Abdul Matenda (10), mwanafunzi wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Uhuru, aliyepotea Juni 8, mwaka huu.
...Bi. Mwajuma Bakari Tindwa akinywa dawa hiyo.
Mwajuma aliliambia gazeti hili kuwa mwanaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha na kwa zaidi ya wiki tatu, wamekuwa wakimtafuta bila mafanikio.

...mmoja wa ndugu wa familia akipata dawa.
“Baada ya kumkosa kote huko nilitoa ripoti Kituo cha Polisi Msamvu na kituo kikuu cha polisi nao wamehangaika bila mafanikio, baada ya kujadiliana na familia yangu tuliamua kumchukua huyu mganga ambaye alituhakikishia kumrejesha mwanangu,” alisema.
...Hata mtoto mdogo naye alishiriki kikombe cha dawa kutoka kwa Sangoma.
Alipotakiwa kuzungumzia mazingira ya mtoto huyo kupotea, alisema alikuwa akicheza na mwenzake ambaye pia anaitwa Omar, lakini mwenzake alirudi na kudai rafikiye amepotea kiajabu.
Mganga huyo aliyefika hapo akiwa na timu ya watu wanne, alisababisha umati wa watu kujaa kushuhudia alichokuwa akikifanya, ikiwa ni pamoja na kumchinja paka na kuinywa damu yake, kuchimba shimo mithili ya kaburi nje ya nyumba na kufukia msalaba.
...Timu nzima ya waganga waliofika kutoa huduma kwa Bi. Mwajuma Bakari Tindwa ili kumrejesha mtoto aliyepotea.
Aidha, akitumia kifaa kama darubini, alimulika na kwenda nyuma ya nyumba ambako alichimba na kutoa mapembe mawili, vitu ambavyo hata hivyo, havikuwezesha kurejea kwa mtoto huyo.
Sangoma hao wakiwa na picha za maraisi wa awamu zote tatu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Tulipofika hapa mtoto alikuwa jirani kwa mujibu wa vifaa vyangu, lakini sasa wamempeleka umbali wa mita 250 hivyo kwa sasa tunaingia ndani na kufanya shughuli zetu kwenye nyumba hii na baadaye tutaendelea na kazi ya kumrejesha,” alisema mganga huyo baada ya kuona sura za watu zikiwa kama zinazouliza.
Mganga akifanya vitu vyake kwenye shimo alilochimba nyuma ya nyumba.
Katika hali ya kushangaza, mganga huyo alikutwa akiwa na picha za marais watatu wastaafu, Baba wa Taifa na Ali Hassan Mwinyi sambamba na ya Rais Jakaya Kikwete. Hadi Uwazi linaondoka eneo la tukio, mtoto Omar hakuwa amepatikana.
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate