EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 24, 2014

SH. MIL. 60 KUMALIZA MGOGORO WA MBASHA

Stori: Haruni Sanchawa na Shakoor Jongo HABARI zilizotua kwenye meza ya Uwazi juzi zinadai kuwa familia mbili, ya Emmanuel na Flora Mbasha zimeweka kikao kwa siku tatu mfululizo kutaka kuinusuru ndoa ya wawili hao lakini imeshindikana huku pembeni ikidaiwa kwamba ili mambo yakae sawa lazima Mbasha alipe shilingi milioni 60.
Mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili Bongo Flora Mbasha.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, kikao hicho kiliitishwa na baba wa Mbasha kwa kushirikiana na ndugu wengine wa pande zote mbili.
“Mbasha na mke wake, Flora walikutanishwa sehemu fulani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupatanishwa. Kikao kilikuwa kizito, wakubwa wa familia zote walikuwepo lakini Flora alikataa mara tano kurudi kwenye ndoa yake.

UWAZI LAPIGA HODI NYUMBANI KWA MBASHA
Juzi Jumapili, Uwazi lilitia timu nyumbani kwa Mbasha, Tabata-Kimanga jijini Dar na kubahatika kuzungumza na baba na mama wa Mbasha bila kumpata Mbasha mwenyewe.
Mzee huyo aliyejitambulisha kwa jina la Maneno alikiri kuwepo kwa kikao kwa muda wa siku tatu tofauti lakini akasema mambo yalishindikana.
“Mimi nilikuja Dar kutokea Dodoma wiki moja iliyopita baada ya kupata wito wa mwanangu kuhusu mgogoro wa ndoa. Nilipofika hapa, sikumkuta Flora, nyumba ilikuwa tupu.
“Kikao kiliitishwa na pande zote mbili, akiwemo Mchungaji Gwajima ambaye alionekana kusuluhisha mgogoro wao lakini dalili za Flora hazikuonesha kuwa tayari kurudi kwenye ndoa yake,” alisema mzee huyo.
Emmanuel Mbasha.
KUNA MKONO WA MTU
Mzee Maneno aliendelea kusema: “Mimi kama mtu mzima, nilichokiona katika ndoa ya mwanangu kuna mkono wa mtu. Ila sasa ametumia mbinu kubwa sana kumrubuni Flora na yeye kakubali kurubunika.”
MAMA MZAZI NAYE
Kwa upande wake, mama mzazi wa Mbasha, Zulfa Maneno alisema kwake ni masikitiko makubwa kwa sababu mtoto wake alishakuwa na jina kubwa kimataifa na mkewe pia.
Alisema: “Mimi kwenye kikao nilipomwona Flora anakataa ndoa yake mara tano, kila akiulizwa anasema hataki kurudi mpaka mara tano, nikajua hakuna ndoa.
“Ninachojua, mgogoro huo wa ndoa ulitengenezwa kwa makusudi kabisa ili ndoa ivunjike. Ila kama aliamua kumwacha mwanangu angefanya hivyo kwa amani na si visa kama hivi.”
Kuhusu kutakiwa shilingi milioni sitini ili Flora arejee kwenye ndoa yake, wazazi hao walisema hawajui kitu labda kama yanasemwa pembeni.
Baba mzazi wa Emmanuel Mbasha.
KULIKUWA NA MGOGORO Habari zaidi zinadai kwamba, fedha zinazotakiwa kulipwa ni kwa sababu, ndoa hiyo ilikumbwa na mgogoro kabla ya kuibuka kwa madai ya Mbasha kumbaka shemeji yake.
Flora aliwahi kufungukia hilo kwamba, kabla ya kutokea kwa madai ya ubakaji, alitibuana na Mbasha na akaamua kuondoka nyumbani kwenda kuishi hotelini. 
DALILI MBAYA
Kuna madai kwamba, siku ambayo Mbasha alikwenda kujisalimisha polisi (Juni 16, 2014), Flora alipigiwa simu kujulishwa lakini hakutokea kituoni.
Ikazidi kuelezwa kwamba, siku Mbasha anapelekwa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar kujibu madai ya ubakaji, pia Flora alijulishwa lakini hakutokea mahakamani hapo.
Mbali na kupelekwa mahakamani, habari za uhakika zinasema hata pale Mbasha alipokosa dhamana na kupelekwa kwenye Gereza la Keko, Flora alijulishwa, lakini hakufanya lolote.
“Je, kwa hayo yote ni kweli Flora anaipenda ndoa yake? Si jibu lipo wazi kwamba  hakuna ndoa.” alisema mtu mmoja aliye karibu na familia hiyo.
Mama mzazi wa Emmanuel Mbasha.
MBASHA BAADA YA KUTOKA JELA
Ushahidi wa majirani umeweka bayana kwamba, Mbasha alipotoka gerezani na kufika nyumbani kwake, Tabata-Kimanga, Dar, walimfuata na kuangua kilio mbele yake huku wakimpa pole kwa mkasa mzima.
Baadhi ya majirani waliozungumza na Uwazi juzi, walisema kuwa siku hiyo nyumbani kwa Mbasha kulikuwa na dalili zote za kuwepo kwa msiba kwani vilio vilitawala.
MADAI
Mbasha, alipandishwa mahakamani Juni 17, mwaka huu kwa madai ya kumbaka mara mbili shemeji yake (jina tunalo).
Siku hiyo alikosa dhamana na kupelekwa Gereza la Keko ambapo Alhamisi ya Juni 19, mwaka huu alirudishwa tena mahakamani hapo kwa ajili ya dhamana. Kesi yake itaanza kusikilizwa Julai 17, mwaka huu huku ikielezwa kuwa upelelezi umekamilika.  
Kwa mahojiano kamili ya Mzee Maneno, mkewe na Uwazi fungua Global Tv Online kupitia.
CHANZO GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate