EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, June 12, 2014

SIMULIZI TAMU YA BAHATI BUKUKU

LIPOISHIA WIKI ILIYOPITA Japokuwa nimejitahidi sana kuisahau siku hii lakini moyo wangu umeshindwa kufanya hivyo. Kila ninapotulia, iwe sebuleni au chumbani kwangu, picha ya siku hiyo huwa inanijia kichwani mwangu. Tukio hilo limekuwa kubwa kwangu huku likiendelea kujirudia kama mkanda wa filamu. SHUKA NAYO SASA…
Nilipenda kwenda shule kusoma, na hii ilikuwa njia mojawapo ya kuepuka kufanya kazi za nyumbani, hasa kuosha vyombo kitu nilichokuwa nikikichukia mno.

Japokuwa nilikuwa mtoto mdogo lakini mama alijitahidi sana kuniweka katika mazingira ambayo mtoto wa kike anatakiwa kuwa.

Achukia kuosha vyombo
Kila siku alikuwa akinitaka nioshe vyombo, hii ilikuwa kazi pekee niliyokuwa nikiichukia mno. Kila nilipokuwa nikirudi nyumbani, mama alikuwa akinipa maziwa na kiporo cha jana, nikimaliza kula, alikuwa akiniambia nioshe vyombo nilivyovitumia.

Nilikereka mno lakini sikuwa na jinsi, nilibaki nikilalamikalalamika lakini mwisho wa siku niliosha vyombo mbele yake huku akionekana kuwa na furaha.
AWA KIONGOZI WA KUIMBA
Ijulikane kwamba kuimba ni kipaji nilichozaliwa nacho. Nakumbuka kipindi hicho mimi ndiye nilikuwa kiongozi wa nyimbo mbalimbali tulizokuwa tukiimba shuleni. Sauti yangu haikuwa nzuri, ilikuwa ni ya kukoroma sana lakini kila nilipokuwa nikiimba walimu waliipenda na ilikuwa ni lazima ujue kwamba ‘huyo anayeimba ni Lusako’.

AANZA DARASA LA KWANZA
Baada ya kusoma shule ya chekechea kwa miaka miwili, mwaka 1990 nilitakiwa kwenda kuanza darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Muungano ambayo haikuwa mbali kutoka tulipokuwa tukiishi.

Kama kawaida yangu, siku hiyo niliamka asubuhi sana huku nikiwa na hamu ya kuanza darasa la kwanza. Moyo wangu haukuweza kusahau, bado niliendelea kukumbuka miaka miwili iliyopita ambapo nilishindwa kulishika sikio langu la upande wa kushoto kwa kutumia mkono wangu wa kulia kwa kuupitisha kichwani.
Kwanza kabla ya yote, hapohapo nyumbani, nikajaribu kulishika sikio langu, nikafanikiwa.

ACHEKELEA KUJIUNGA NA SHULE YA MSINGI
Naweza kusema kwamba katika mwaka huo, siku hiyo ndiyo nilikuwa na furaha kupita kawaida. Nilipenda sana shule, kila nilipokuwa nikiwaona wanafunzi wakipita nyumbani huku wakiwa wamevalia sare zao za shule, niliona wivu moyoni.

Leo hii na mimi nilitakiwa kwenda kuanza darasa la kwanza! Asubuhi ya siku hiyo, mama akaniletea sketi na shati huku chini nikivalia soksi za pundamilia.
Sikuwa na sare za shule hivyo siku hiyo nilivalia nguo za nyumbani ila miguuni nilikuwa na soksi hizo za pundamilia. Baada ya kutembea kwa umbali mdogo, nikaelekea shuleni huku nikiongozana na baba, mzee Bukuku.

Watoto waliokuja kuanza shule walikuwa wengi na zoezi lilikuwa lilelile la miaka yote, kushika sikio lako. Wapo walioshindwa ambao walilia kama nilivyofanya miaka miwili iliyopita lakini pia walikuwepo wale waliofaulu na kutakiwa kujiunga na shule hiyo kwa ajili ya kuanza na elimu ya msingi huku nikiwa nimeandikishwa jina jingine na kuitwa Bahati.
                              ***
AANZA MASOMO
Niliipenda masomo, niliipenda shule kwa jinsi majengo yake yalivyokuwa. Yalipendeza na kuvutia sana. Siku hiyohiyo ambayo baba alikuwa amenipeleka shuleni hapo, tukaingizwa darasani na kupangwa, siku iliyofuata, tukaanza masomo huku tukiwa watoto zaidi ya arobaini katika darasa moja.

Kila mmoja alionekana kuwa na furaha kama nilivyokuwa. Hakukuwa na utulivu, kila wakati wanafunzi walikuwa wakipiga kelele, nadhani kwa walimu au kwa watu waliokuwa katika mitaa yenye watoto wengi watakuwa wanalitambua hili, jinsi watoto wanavyopiga kelele zenye kuleta kero.
AONGOZA KWA UTUNDU
Kati ya wanafunzi wote waliokuwa darasani, mimi ndiye nilionekana kuwa mtundu. Kwanza sikutulia sehemu moja, nilionekana kama mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani, muda huu unaweza kuniona hapa na baadaye kuniona kule.

UTUNDU WAMPA UMONITA
Kutokana na utundu wangu wa muda mfupi, hata mwalimu wa darasa hilo aitwaye Rugemilila alipoingia darasani, akanichagua niwe ‘monita’ yaani kiongozi wa darasa lile.

Maisha ya nyumbani yaliendelea kuwa vilevile kwamba kila nilipokuwa nikirudi na kula chakula, mama alinitaka nioshe vyombo. Bado mama alinifundisha mambo mengi huku akitamani sana niwe kama wasichana wengine, nadhani mbele ya maisha yangu aliyaona  kwani kwa kile alichokuwa akikitaka ndicho kimeweza kunisaidia sana kipindi hiki.
AKAMUA NG’OMBE MAZIWA
Kazi zote za nyumbani ambazo alikuwa akizifanya mama, ilikuwa ni lazima na mimi nizifanye. Siku ambayo sikuwa nikienda shule, ilikuwa ni lazima nipike japo chai na kufanya usafi nyumbani hapo huku nikisaidiana naye.

Nyumbani kulikuwa na ng’ombe, kila siku, hata kabla ya kwenda shule ilikuwa ni lazima niamke asubuhi sana, nikamue maziwa na kisha mtu ambaye alikuwa akihusika kwa ajili ya kwenda kuwachunga akiwatoa zizini na kwenda nao machungoni.
ACHUNGA NG’OMBE
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu ya kila siku. Siku ambazo sikuwa nikielekea shuleni, pia nilikuwa nikichukuliwa na kupelekwa machungoni. Nilichukia kazi nyingine lakini hii ya kuwapeleka ng’ombe machungoni niliipenda kwa sababu ilinipa nafasi ya kuondoka nyumbani hapo kwenda kuzurura na ng’ombe hao.

AUZA CHIPSI
Kutokana na utundu niliokuwa nao na ujanja wa hapa na pale, mwalimu wangu wa darasa akanichagua niuze chipsi zake. Wanafunzi wengi walikuwa wakiitamani kazi hii kwani walijua fika kwamba mara unapouza na nyingine kubaki, walimu huwa na kawaida ya kukupa mfuko mmoja ule.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate