EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 3, 2014

ALIYEMTESA HAUSIGELI SIKU 730 AHENYESHWA!


Stori: Haruni Sanchawa na Deogratius Mongela
Mwanamke Yasinta Rwechengura, mkazi wa Boko wilayani Kinondoni, Dar anayekabiliwa na kesi ya kutuhumiwa kumtesa hausigeli wake kwa miaka miwili (siku 730), amejikuta akihenyeshwa mahakamani.Hayo yamemkuta juzi alipofikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Kinondoni kujibu tuhuma zinazomkabili ambapo alikuwa akipokea amri kutoka kwa askari na kumfanya kukosa raha.
Mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi.
Msala huo unagusa hisia za wengi ndiyo maana watu kutoka viunga mbalimbali vya Jiji la Dar walifurika mahakamani hapo kusikiliza mwenendo wa kesi hiyo iliyosomwa mbele ya Hakimu Mkazi, Boniphace Lihamwike.

Akisoma kesi hiyo mahakamani hapo, wakili wa serikali ambaye alikuwa  upande  wa jamhuri, Mohamed Salum alisema anaiomba mahakama hiyo kutotoa dhamana kwa  mtuhumiwa kwa sababu za kiusalama.
Sababu ya pili alisema bado hali ya mgonjwa ni mbaya na amelazwa kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Akipelekwa mahabusu.
Kesi hiyo ambayo inafuatiliwa kwa ukaribu na wanaharakati wa haki za  binadamu, awali ilikuwa inasikilizwa na Hakimu Suleiman Mzava ambaye juzi hakufika mahakamani hapo  kutokana na uhamisho alioupata na badala yake  kesi hiyo ilitajwa kwa Hakimu Lihamwike.
Upande unaomtetea mtuhumiwa huyo uliokuwa ukiongozwa na wakili wa kujitegemea, Msomi Gidion, uliiomba mahakama kumpa mteja wao dhamana lakini ukagonga mwamba.
Hata hivyo, wakili Mohamed aliendelea kuiomba mahakama kwa mara nyingine kutotoa dhamana kwa  mtuhumiwa kwa sababu alizozitoa awali.
Wananchi wakimshangaa
Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, alisema pande zote zilikuwa na hoja akianza na upande wa mtuhumiwa ambapo alitoa ufafanuzi kuwa ni haki  yake ya kikatiba kupata dhamana lakini upande wa jamhuri nao ulikuwa na hoja.
Hakimu huyo alisema kuwa shauri hilo  kwa mara ya kwanza lilianzia kwa hakimu mwingine na ndani ya faili la kesi hiyo hakukuwa na vielelezo vyovyote hivyo kuirudisha kesi hiyo kwa hakimu kiongozi kwa ajili ya kupangiwa hakimu atakayeisikiliza.
Hausigeli aliyedaiwa kuteswa na mtuhumiwa huyo
Baada ya hapo, mtuhumiwa alipandishwa kwenye karandinga na kurudishwa mahabusu kwenye Gereza la Segerea, Dar kuendelea kuhenya hadi atakapopata dhamana huku wananchi waliofika mahakamani hapo wakimshangaa.

CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate