EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 3, 2014

NDOA YA DIDA KUVUNJIKA; MUMEWE AFUNGUKA MAZITO

SIKU chache baada ya kuvunjika kwa ndoa ya Khadija Shaibu ‘Dida’, aliyekuwa mumewe, Mtangazaji wa TV1, Ezden Jumanne ameibuka na kutoa sababu kuu tatu za kutengena kwao, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.

Khadija Shaibu ‘Dida’ na Mtangazaji wa TV1, Ezden Jumanne wakipozi.
Akizungumza na waandishi wetu katika nyumba aliyohamia kwa sasa, Kijitonyama, Dar, Ezden alisema mgogoro kati yake na Dida ulianza zamani ambapo Dida alikuwa na tabia ya kurudi usiku mnene, Ezden alidai kadiri siku zilivyozidi kusonga mbele, tabia hiyo ilizidi kuonekana ingawa alikuwa akimuonya mara kwa mara.

BIG BROTHER NDIYO TATIZO
Pamoja na sababu hizo, Ezden aliitaja sababu kuu iliyoanza kuzua mgogoro uliosababisha kuvunjika kwa ndoa hiyo ni Shindano la Big Brother Africa linalotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu nchini Afrika Kusini.
‘Dida’ na Bw. Ezden wakati wa harusi yao.
Alisema siku moja mtalaka wake huyo alimweleza kuwa kuna rafiki yake aliyemtaja kwa jina la Furaha amempa mchongo wa kuwa mgeni staa (celebrity guest) ndani ya Jumba la Big Brother na kumuomba ampe ridhaa ya kwenda huko.
Akizidi kumwaga data mbele ya kinasa sauti cha Risasi Mchanganyiko, Ezden alisema:
“Nilimruhusu kwa moyo mmoja ambapo pia aliniomba nimsaidie kumpa uzoefu juu ya lugha ya Kiingereza ili akaendane na kanuni za Big Brother.
Ezden akipozi.
“Kama mume nilimsapoti kwa nguvu zote, siku nyingine kama nikiwa nimerudi nyumbani mapema mimi mwenyewe nilikuwa nikimfundisha ‘tense’ mbalimbali.”
Katika aya nyingine, Ezden alisema kuna siku Dida alimfungukia kuwa hatakwenda Big Brother kama mgeni staa kwani anatakiwa kuingia kama mshiriki na kumwambia kuwa alikuwa akiogopa kumwambia ukweli mapema.
“Nilimkatalia ndipo alipocharuka, huwezi amini alifikia hatua  ya kusema nambania zali lake. Niliumia sana siku ile ikabidi nimuulize kama anaithamini Big Brother kuliko ndoa yake, hakunijibu.
“Kama mume ilibidi niwaulize wazazi na mashemeji zangu kama wamemruhusu Dida kushiriki shindano hilo kama alivyoniambia, walidai aliwaambia kuwa mimi ndiye niliyemruhusu ndiyo maana nao hawakuwa na pingamizi.
'Dida' akiwa ofisi za Times FM.
“Baada ya kuwaelewesha waliniambia hawakupenda mambo hayo ya Big Brother kwa kuwa yana udhalilishaji ndani yake,” alisema Ezden.
Siku ya tukio, Ezden alisema alikuwa akioga bafuni na simu yake ilikuwa kitandani, ghafla Dida alimfuata na kumuuliza kwa nini aliweka password!
“Alipiga kelele mpaka majirani wakaanza kujaa nyumbani kisa ‘password’ niliyoiweka kwenye simu yangu. Nikamuuliza yeye si ndiye aliyesema kuwa kila mtu awe na simu yake! Akaanza kunipa maneno ya kejeli.
“Hapo nikaona heshima yangu inashuka. Kiukweli nilimpiga mpaka nikamuumiza. Baadaye akaondoka kwa hasira kumbe alikwenda kuwachukua ndugu zake.
“Walipokuja tukajitahidi kusuluhisha lakini kila nilipopewa nafasi ya kuzungumza, Dida aliniingilia. Kwa kuwa tulishawahi kukaa vikao vingi sana kabla lakini hakuna tulichoweza kusuluhisha, niliona hakuna  haja ya kuendelea naye,” alisema Ezden na kuongeza kuwa kikao hicho kiliisha kwa ahadi kwamba angetoa talaka kwa Dida ambaye naye alionekana kuikubali.
Ezden alisema, Juni 28, mwaka huu  alimpa Dida talaka tatu na kuongeza kuwa hategemei kurudiana naye wala kuoa hivi karibuni.Kwa upande wake, Dida alipopewa nafasi ya kuzungumza alisema: “Mimi sina la kusema na wala sitaki kulumbana na mtu.”
CHANZO GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate