EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 2, 2014

Saa nne za Maximo kudadadeki

KOCHA Mkuu mpya wa Yanga, Mbrazili, Marcio Maximo, jana alianza kazi yake kwa mkwara mzito huku kila aliyehudhuria akionyesha kutikisa kichwa kuikubali.
Wachezaji wa Yanga wakiongozwa na kocha msadizi, Leonado Martins (wa kwanza kushoto) kwenye mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika jana Coco.
Maximo majira ya saa mbili kamili asubuhi alikwishatua kwenye Ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam na kuanza rasmi mazoezi na timu hiyo ya Jangwani na kuwakusanya tena wachezaji wake saa tisa kamili kwenye Uwanja wa Bandari Tandika kwa mazoezi ya takribani saa mbili.

Maximo ambaye amekuwa akifanya mambo yake kisasa, alianza kama kawaida yake huku akiwasimamia wachezaji wake kunyoosha viungo na baada ya hapo kuanza kuwakimbiza.
Wachezaji wa Yanga ambao wengi walikuwa wametoka kwenye mapumziko, walikimbizwa kwa umbali wa kilomita 1.5 mara mbili kwenda na kurudi huku kocha huyo akiungana nao akiwa na kocha wa vijana, Salvatory Edward.
Kocha wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo akisimamia leo Coco Beach.
Maximo alionyesha kuwa yupo fiti pamoja na kwamba umri umeenda baada ya kuanza na wachezaji hao na kumaliza nao mbio bila kupumzika sehemu yoyote ambapo walitumia dakika 30.
Mara baada ya kumaliza kukimbia, wachezaji wa Yanga walitakiwa kupumzika kwa kunywa maji na kunyoosha viungo na kuanza zoezi la kuruka koni na kukimbia mbio fupi ambazo zilichukua dakika 30, msimamizi akiwa ni kocha msaidizi, Leonardo Neiva.
Kama ilivyo kawaida yake, Maximo aliendelea na utani wake huku akichombeza kwa maneno ya Kiswahili; tupo pamoja, harakaharaka, ongeza mwendo, usichoke na mengine mengi.
Baada ya kumaliza kuruka koni, Maximo alionyesha kuridhika na kuwaita pamoja na viongozi wengine waliokuwepo uwanjani hapo na kuzungumza nao.
Coutinho (juu) akifanya mazoezi na beki Yusuf Ngao.
Baada ya mazungumzo kocha huyo aliwakusanya wote na kuomba dua na kutawanyika ambapo aliwapa ruhusu ya kuzungumza na waandishi, lakini yeye akapanda prado lake na kutimka.
Hata hivyo, saa tisa alasiri kocha huyo alilianzisha tena na mastaa wake kwenye Uwanja wa Chuo cha Bandari, Temeke ambapo alianza kwa kuwazungusha uwanja raundi tatu huku kukukiwa na mashabiki kibao.
Mashabiki hao walishuhudia mazoezi mazuri huku kocha huyo akiwataka wachezaji wake kufanya kila kitu kwa uhakika.
Mashabiki waliofurika uwanjani hapo walionekana kushangilia kwa nguvu kubwa kila Mbrazili Coutinho alipokuwa akigusa mpira na wakati Maximo alipokuwa akiwafokea wachezaji wake pale walipofanya vibaya.
Kocha Maximo akimuelekeza jambo mshambuliaji Jerry Tegete.
Mashabiki waliokuwepo uwanjani hapo walionekana kumsifia kocha huyo, huku wengi wakiamini kuwa kama ataendelea hivyo, Yanga itakuwa bonge la timu.
Maximo aliongoza mazoezi hayo kwa ustadi wa hali ya juu, huku msaidizi wake naye akiwa moto kwenye kila kitu ikiwa ni pamoja na kukimbia, kupiga pasi na kukaba.
Hata hivyo, Coutinho kuna muda alidondoka na kuchubuka mguuni, lakini bado aliendelea kukipiga hali iliyowafanya mashabiki washangilia.
Kiungo mpya wa Yanga, Mbrazil, Coutinho (7) akipasha na wenzake.
Mazoezi ya jioni yalikamilika saa 11:45 jioni na kukamilisha saa nne za Maximo za siku ya kwanza, huku Coutinho akifunga mabao mawili.
Wachezaji wa kikosi cha kwanza waliohudhuria mazoezi ya jana ni Juma Kaseja, Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Abdul, Salum Telela, Hussein Javu, Said Bahanuzi, Omega Seme, Rajab Zahiri, Mbuyu Twite na  Saleh Abdallah pamoja na wa kikosi cha pili..
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate