EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, September 22, 2014

DIAMOND YAMKUTA TENA UINGEREZA

Stori: Musa Mateja
Ni nuksi, gundu au hujuma? Ndivyo unavyoweza kujiuliza kufuatia tukio lingine baya lililomkuta staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa London nchini Uingereza ikiwa ni siku kadhaa tangu aliposababisha vurugu nchini Ujerumani, Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili ya kilichojiri.
Promota wa Diamond wa Uingereza (Victor Dj-rule).
TWENDE LONDON
Habari kutoka kwa ‘mtu wetu’ aliyeko jijini London zilieleza kwamba Ijumaa iliyopita Diamond alitarajiwa kufanya shoo kubwa kwenye Ukumbi wa LaFace jijini humo lakini mambo yakamwendea kombo na kujikuta akihenyeshwa na polisi kwa kushindwa kufanya shoo hiyo iliyokuwa imetangazwa kupita maelezo.
‘ACHAFUA’ KURASA ZAKE
Kwa siku mbili mfululizo, Diamond alichafua kurasa zake za mitandao ya kijamii kwa kuweka mabango na kuitangaza shoo hiyo kwa fujo za kufa mtu.
DIAMOND AALIKA WATU, AOMBA ACHAGULIWE LISTI YA NYIMBO
Saa kadhaa kabla ya shoo, Diamond alitumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kuwaalika watu kwenye shoo hiyo kubwa huku akiomba wampatie listi ya nyimbo wanazotaka awaimbie, jambo ambalo mashabiki wake walilifanya.

Promota wa Diamond wa Nigeria aliyetapeli ile  shoo ya Ujerumani.
UKUMBINI
Ilielezwa kwamba usiku ulipoingia watu walianza kumiminika ukumbini.
TUKIO
“Unaambiwa watu walisubiri mpaka usiku wa manane hawamuoni Diamond.
“Baadhi ya mashabiki walianza kupiga kelele ndipo uongozi wa ukumbi huo ukawaambia hata wao walikuwa hawajalipwa fedha za ukumbi.
“Ilipofika alfajiri, baadhi ya mashabiki walitaka kufanya fujo ndipo uongozi wa ukumbi ukaamua kuwarudishia viingilio vyao kwa sababu Diamond alifuatwa hotelini, akagoma kwenda ukumbini hadi alipwe chake kwanza,” kilisema chanzo chetu kilichohudhuria ukumbini humo.
TOFAUTI NA UJERUMANI
Tofauti na Stuttgurt, Ujerumani ambako mashabiki walifanya uharibifu mkubwa, mashabiki wa London waliamua kuwa wapole tu na kurejea majumbani mwao na hasira walizozimeza vifuani huku polisi wakifanya kazi ya ziada kutuliza ghasia.
Sehemu ya meseji za Diamond kwenye instagram
DIAMOND MIKONONI MWA POLISI
Baada ya upepo kutulia, ilisemekana kwamba polisi walimfuata Diamond hotelini na kumpeleka kituoni ambako alitoa maelezo yake.
Ilielezwa kwamba Diamond aliwaambia polisi kuwa promota alishindwa kumlipa fedha yake hivyo asingeweza kufanya shoo ya bure.
DIAMOND MITANDAONI
Diamond alimtupia lawama promota huyo ambapo mara tu baada ya kutoka kituoni aliandika kwenye kurasa zake za kijamii:
“Tafadhali ndugu zangu wa UK (Uingereza)!!!….kuweni makini sana na promota huyu (Victor – Dj Rule) mnaposikia kaandaa shoo, party au hafla yoyote…ni vyema kuziepuka na kutohudhuria kabisa kwa sababu ni tapeli…. si unajua aisifiae mvua imemnyeshea… basi mie nimeloa kabisa.”
Mkali wa Bongo Fleva 'Diamond' aliyeachwa katika hali ya sintofahamu na mapromota matapeli.
DIAMOND ATAFUTWA
Baada ya kunyetishiwa mkanda mzima, Jumamosi iliyopita, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Diamond ambapo alipopatikana alikuwa tayari ametua nchini Ujerumani kwa ajili ya ile shoo ya bure aliyotakiwa kuifanya ili kulipiza ile iliyoharibika.
Staa huyo alikiri kukutwa na mkasa huo na kuwatahadharisha wasanii wengine wa Bongo kuwa makini:
“Jamani kama ni kuniabisha, kweli wameniaibisha lakini ndiyo kwanza napata mzuka wa kufanya kazi kwa bidii.”
BABU TALE ANASEMAJE?
Kutoka kwa Diamond, gazeti hili lilimgeukia meneja wake, Babu Tale ambaye hakuambatana na Diamond akakiri kuwa ishu kama hizo zinawaharibia sana.
MPANGO WA KUMMALIZA?
Kwa mujibu wa wadau waliokuwa na maswali mengi bila majibu hasa ishu ya kuwepo kwa mkataba, kuna mpango wa kummaliza Diamond kimataifa hasa barani Ulaya kwani ameshakwenda Marekani mara nyingi na kufanya shoo nyingi bila matatizo kama hayo.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate