EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 16, 2014

MAMA AMTOA MWANAYE KAFARA AWE TAJIRI!


CHANZO GLOBAL PUBLISHERS
MY God! Hali huenda ikigeuka, wakati jamii inaamini akina baba ndiyo wenye tabia ya kutokuwa na uchungu kwa watoto, imekuwa tofauti kwa mama huyu!Ni mkazi mmoja wa Kijiji cha Mwanamonga, Kata ya Lilambo, Manispaa ya Songea, Kasiana Komba (60) anadaiwa kuuawa na mumewe, Allan Menas Lwambano (76) kisa kikidaiwa mambo ya kumtoa kafara mtoto.
Bwana Allan Menas Lwambano anayedaiwa kumuua mkewe.
Tukio hilo la kuhuzunisha lilijiri usiku wa Agosti 25, mwaka huu ambapo maelezo ya mume huyo yanasema ni baada ya marehemu kumtaka akubali kumuua mtoto wao mmoja (jina tunalo) kati ya saba ili walipe madeni kwa imani ya kishirikina na kufanikiwa katika kipato (utajiri).

RPC wa mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msekela.
ILIVYOKUWA
Ilielezwa kuwa, mwanaume huyo alikataa ombi hilo na mkewe akamwekea mgomo wa kumnyima unyumba hadi pale atakapokubali ombi lake hilo.

MAISHA YA NDOA
Ilidaiwa kuwa, maisha ya wawili hao yakawa ya ‘sitaki nataka’, mume akitaka unyumba mke hataki kwa vile amemkatalia kumtoa mtoto wao kafara wakati yeye mke alishawaambia wenzake (kwenye ushirikina) kuwa, ameamua kumtoa mtoto huyo lakini baba yake hakutaka kufanya hivyo.

SIKU YA TUKIO
“Siku ya tukio usiku, Lwambano alirudi nyumbani na kumkuta mkewe amelala, alianza kumshikashika mwilini kuashiria alimhitaji faragha, ndipo mke huyo alipotoka nje na kuchukuwa mchi wa kutwangia mahindi kwa lengo la kumpiga mumewe.
Kasiana Komba aliyedaiwa kumtoa kafara mtoto wake ili apate utajili.
“Mumewe aliuzuia, akamnyang’anya na kumpiga mkewe kichwani, alianguka palepale na kufariki dunia,” kilisema chanzo.
MUME AHANGAIKA KUUZIKA MWILI
Habari za ndani zinasema kuwa, mume alipobaini ameua aliuchukuwa mwili wa mkewe na kuupeleka nyuma ya nyumba ambako kuna choo na kuuzika huku akipanda migomba juu ili kuzubaisha watu.

WATOTO: “BABA, MAMA YUKO WAPI?”
Agosti 26, mwaka huu, siku moja tu baada ya tukio hilo la kutisha, watoto ambao wanaishi mbali na nyumba hiyo walifika na walipoona hawamuoni mama yao, walimwuliza baba yao: “Baba, mama yuko wapi?”  akawajibu: “Mama yenu ameenda mjini Songea, atarudi.”

WATOTO WAENDA KWA MGANGA
Ikazidi kudaiwa kuwa, Agosti 27, mwaka huu, watoto hao hawakukubaliana na majibu ya baba yao, wakaenda kwa mganga wa kienyeji (jina halikupatikana mara moja) kwa lengo la kupiga ramli ili kujua alipo mama yao.
Waombolezaji wakiwa msibani.
“Mganga baada ya kuangalia ‘king’amuzi’ chake aliwaambia kama wanataka kujua mama yao alipo, warudi wakamchukue baba yao na kumfikisha kwa mganga huyo kwani yeye (baba) ndiye ana siri nzito.
“Watoto hao wakiongozwa na kaka yao mkubwa (Mathias) walimpa baba yao maagizo ya mganga. Ndipo baba huyo naye akawaambia kama wanataka kujua ukweli wa mama yao alipo, waongozane hadi kwa mtendaji wa kijiji akasimulie mbele yake.

MBELE YA MTENDAJI
Septemba 4, mwaka huu, familia hiyo ikiongozwa na baba mtu walifika kwa Mtendaji wa Kijiji cha Mwanamonga, Said Mango na Mwenyekiti wa Kijiji, Maria Kahimba ambapo katika maelezo yake , mzee huyo alikiri kumuua mkewe kwa kumpiga na mchi kichwani.

NUKUU YA MUME
Mzee huyo ananukuliwa hivi: “Nimemuua mke wangu nikamfukia nyuma ya nyumba yangu kwenye choo (watu wakapigwa butwaa).
Polisi wakiwa eneo la tukio.
“Sababu kubwa ya chanzo cha tukio ni mke wangu nilimkatalia ombi lake la kutaka tumuue mtoto wetu mmoja ili alipe madeni ya uchawi na kufanikiwa kimapato.
“Nilimkatalia, akawa ananinyima unyumba. Siku ya tukio nilimlazimisha kunipa unyumba, akakataa akataka kunipiga na mchi, nikamuwahi yeye na kumpiga, akakata roho.”

NANI ANAYEJUA?
Mwanamke mmoja aliyekataa kutaja jina lake, aliliambia Uwazi kwamba, marehemu aliwahi kumlalamikia kuhusu mumewe kugoma kumtoa mtoto wao mmoja kafara ili waweze kupata  mali. Alisema mumewe haoneshi kutaka mabadiliko.

“Alisema namwambia mume wangu tumtoe mtoto mmoja kafara tupate utajiri lakini alisema sitaki kusikia habari hizo, kwani yeye ameridhika na ufukara,” alisema mwanamke huyo akimkariri marehemu.
POLISI WAFUKUA MWILI, WAKUTA UMEHARIBIKA
Baada ya maelezo ya mzee huyo, vilio vilitawala, hakuna aliyeamini kisha familia kwa kushirikiana na wananchi na jeshi la polisi,

walifika nyumbani kwa mzee huyo akaonyesha sehemu aliyomfukia mkewe, polisi wakaamuru mwili huo ufukuliwe ukakutwa umeharibika vibaya, hasa sehemu ambazo mchi ulipiga.
Baada ya polisi na madaktari kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu, waliwaruhusu wanandugu wauzike.

MTUHUMIWA YUKO POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, ACP Mihayo Msikela (pichani), amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya taratibu za kisheria.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate