KATIKA
Gazeti la Amani Toleo Namba 829 la Septemba 11-17, 2014, kulichapishwa
habari ukurasa wa mbele iliyosomeka: “DIVA: ZITTO NI MUME WANGU.”
Ikikolezwa na dondoo ‘Adai ni mke anayetambulika kisheria’ na ‘Asema
hayuko tayari kuachana naye kirahisi,’ ambayo uongozi wa gazeti
umekusudia kwa nia njema kutoa ukweli juu ya habari hiyo.
Ufafanuzi huu unalenga kumaliza mkanganyiko uliojitokeza hasa baada
ya kuwepo kwa madai kutoka kwa mhusika ambaye ni Loveness Malinzi (Diva)
kuwa, hakuzungumza na gazeti kile kilichoandikwa na kwamba alikuwa
anazushiwa; madai haya aliyawasilisha chumba cha habari kwa njia ya simu
na sehemu kuyaweka kwenye ukurasa wake wa kijamii wa Instagram.
Kama hilo halitoshi, Diva alikana kuzungumza na mwandishi wa habari
hiyo ambapo alisema mazungumzo yao yalihusu mwaliko wa Kipindi cha
Global TV Online ambacho kinarushwa na mtandao unaoendeshwa na Kampuni
ya Global Publishers inayomiliki pia Gazeti la Amani na si vinginevyo.
Malalamiko haya ya Diva yalikuja muda mchache baada ya gazeti kutoka
likiwa na habari hiyo ambapo jopo la wahariri wa Amani kabla ya
kuchapisha habari hiyo walijiaminisha kuwa ni ya kweli kutokana na
taarifa pamoja na vielelezo vya rekodi ya sauti ya mazungumzo
alivyoviwasilisha mwandishi kwenye dawati kuthibitisha kuwa alifanya
mazungumzo na mhusika kuhusiana na msingi wa habari nzima iliyoandikwa.
Kama tulivyoeleza, baada ya habari hiyo kutoka na kipande cha sauti
kuingizwa kwenye Tovuti ya Global Publishers, ndipo yalipoibuka madai
hayo huku baadhi ya wasomaji wakieleza kuwa ile siyo sauti ya Diva; hapo
ndipo uongozi wa gazeti ulipoamua kufuatilia ukweli na kubaini
yafuatayo.
Pamoja na ukweli kuwa Mheshimiwa Zitto Kabwe (Mbunge wa Kigoma
Kaskazini) na Diva wana ukaribu, mazungumzo kati ya mwandishi na
mwanadada huyo kuhusiana na kauli yake ya: “Zitto ni Mume Wangu,”
hayakufanyika na kwamba mwandishi alipika habari na kutengeneza sauti ya
Diva kwa lengo la kuwahadaa wahariri kwa nia mbaya!
Kwa msingi huo sisi kama chombo cha habari makini, kinachosimamia
weledi, kulinda na kuheshimu haki za binadamu; tunachukuwa nafasi hii
kumuomba radhi Diva, Mheshimiwa Zitto, sanjari na jamii kwa ujumla kwa
usumbufu wowote uliosababishwa na habari hiyo.
Aidha, uongozi unapenda kuutangazia umma kuwa, hatua kali za
kinidhamu zimeshachukuliwa dhidi ya mwandishi husika sambamba na onyo
kwa viongozi wote wa gazeti kwa udhaifu uliojitokeza katika habari hiyo.
Tunaomba jamii ielewe kwamba Global Publishers siku zote inasimamia
UKWELI na kamwe hairuhusu kabisa habari za uongo kuandikwa katika
magazeti yake.
Jamii iendelee kutuamini na kushirikiana nasi katika kusimamia weledi
wa uandishi wa habari. Milango ya kukosolewa iko wazi, hivyo kwa mwenye
malalamiko yoyote juu ya habari zetu, iwe ni uongo au kutotendewa haki,
asisite kuwasiliana na viongozi kwa hatua zaidi. Ndimi, Mhariri
Kiongozi, Magazeti Pendwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe
No comments:
Post a Comment